Philo_Sofia
Member
- Oct 4, 2023
- 60
- 94
Maisha ni mambo yote tunayofanya. Ni shughuli zote za uchumi na utafutaji wa fedha na mali, na kadhalika. Haya yote ni muhimu, na ni ya lazima kwa ukuaji na maendeleo ya mtu.
Lazima watu wafanye kazi, wazalishe, watengeneze na wauze. Wakabiliane na matatizo na changamoto. Waijenge dunia na waendelee. Lakini katika haya yote, sio kwamba hayo ndio mwisho. Mwisho wako ni uzima. Kumbe mtu ni uzima. Kwa hiyo, uzima ni bora na muhimu kuliko maisha.
Uzima ni uhai. Ni Roho. Ni nishati. Ni akili. Ni nguvu. Ni moyo. Ni pumzi. Ni kile kinachobaki hai. Ni kile kinachoendelea kuwepo baada ya mwili kufa na kuharibika.
Maisha si kwa ajili ya maisha yenyewe. Maisha ni kwa ajili ya uzima, ni kwa ajili ya uhai. Maisha yako hayapaswi kuharibu uzima wako. Kama kwa maisha yako umeharibu uzima wako, umeharibu vilevile maisha ya wengine. Hayo sio maendeleo, sio amani, ni uharibifu.
Maisha sio lengo lako la mwisho wala lengo la binadamu. Lengo lako ni uzima, lengo la binadamu ni uhai. Shughuli zako kama zinaharibu uhai, unaharibu uzima wako. Maisha yako lazima yakuongoze kulinda uzima wako; kwa sababu maisha yako ndio yataamua vile uzima wako utakuwa.
Lazima ukabiliane na maisha, lakini ujue kwamba maisha sio lengo lako la mwisho. Lengo lako la mwisho, ni uzima. Baada ya maisha kuna uzima, ambao uzima huo unategemea wewe uliishije. Maisha yako yalikuwaje.
Wafundishe rafiki zako, kwamba baada ya maisha hapa duniani kuna uzima. Huu ndio unaobaki na ndio unaokuwa hai. Wambie waangalie maisha yasije yakaharibu uzima wao. Kwa maana maisha ni uzima na maisha yanaharibu uzima.
Lazima watu wafanye kazi, wazalishe, watengeneze na wauze. Wakabiliane na matatizo na changamoto. Waijenge dunia na waendelee. Lakini katika haya yote, sio kwamba hayo ndio mwisho. Mwisho wako ni uzima. Kumbe mtu ni uzima. Kwa hiyo, uzima ni bora na muhimu kuliko maisha.
Uzima ni uhai. Ni Roho. Ni nishati. Ni akili. Ni nguvu. Ni moyo. Ni pumzi. Ni kile kinachobaki hai. Ni kile kinachoendelea kuwepo baada ya mwili kufa na kuharibika.
Maisha si kwa ajili ya maisha yenyewe. Maisha ni kwa ajili ya uzima, ni kwa ajili ya uhai. Maisha yako hayapaswi kuharibu uzima wako. Kama kwa maisha yako umeharibu uzima wako, umeharibu vilevile maisha ya wengine. Hayo sio maendeleo, sio amani, ni uharibifu.
Maisha sio lengo lako la mwisho wala lengo la binadamu. Lengo lako ni uzima, lengo la binadamu ni uhai. Shughuli zako kama zinaharibu uhai, unaharibu uzima wako. Maisha yako lazima yakuongoze kulinda uzima wako; kwa sababu maisha yako ndio yataamua vile uzima wako utakuwa.
Lazima ukabiliane na maisha, lakini ujue kwamba maisha sio lengo lako la mwisho. Lengo lako la mwisho, ni uzima. Baada ya maisha kuna uzima, ambao uzima huo unategemea wewe uliishije. Maisha yako yalikuwaje.
Wafundishe rafiki zako, kwamba baada ya maisha hapa duniani kuna uzima. Huu ndio unaobaki na ndio unaokuwa hai. Wambie waangalie maisha yasije yakaharibu uzima wao. Kwa maana maisha ni uzima na maisha yanaharibu uzima.