Maisha niliyonayo natamani hadi kufa

Maisha niliyonayo natamani hadi kufa

Pole sana ndugu. Ninakuelewa sana hasa hapo kwenye madeni. Hii hali ilishanitokea mwaka 2012 nikaona dunia ipo mabegani mwangu. Nilienda kwa mganga nikaishia kupoteza hela na kutofanikiwa kabisa. Nakumbuka niliishia kugombana na mganga. Nikajaribu kwa mama fulani mchungaji wa kilokole naye tukashindwana kwa sababu hata kile kidogo nilichokuwa napata anataka nimpe kama sadaka na mbaya zaidi alitaka nitoe mchango wa pesa mingi kununua vifaa vya muziki vya kanisa lake. Kwa upande wangu kilichonisaidia ni kuhamia DSM na kuanza kujitafuta from the scratch. Nilikuwa winga Kkoo kwa miaka miwili hadi pale nilipopata unafuu wa maisha.

Kuhusu madeni kaa chini na wanaokudai uwaeleze hali halisi uliyo nayo na kwaomba wakupe muda zaidi. Huenda pia kuna wanaoweza kukusamehe deni. Ila jitahidi uepuke madeni mapya. Kama wewe ni mwanaume jichanganye mtaani piga kazi yoyote ya halali ili mradi mkono uende kinywani. Vibarua vya ujenzi, kilimo na yoyote ile inayopatikana piga. Ukiwa Dar nenda Kkoo asubuhi kama mfanyakazi utapata dili kule.

Kutaka kujiua sio sahihi. Jipe muda kwanza. Kuwa mvumilivu.
 
Be strong as a man
Wenzio wapo ICU na wana magonjwa mazito lakini bado wana matumaini ya kuishi.
Ukijiua ni hasara kwako na wazazi wako.
Bado Una nafasi.
Jieleze kwa kina wewe ni nani elimu yako,uzoefu wako kazi utapata tu.
Maisha ni uvumilivu.
 
Pole sanaa mkuu

Tembelea watoto yatima, hawakatazi kwenda tu kuwaangalia na kuongea nao kwenye vituo vyao hata kama hauna pesa

Tembelea wagonjwa mahututi mahospitalini, tembelea waanga wa ajali tofauti tofauti mahospitalini au majumbani kwao ukaongee nao na utapata imani juu yao

Kuna watu hawana mikono wala miguu wanaishi kwa kuomba tu mabarabarani jaribu kuwatembelea watakuadithia changamoto zao bila hata kuwapa msaada wa kipesa, watakukaribisha na watakupa ushirikiano wa kimaongezi

Tembelea watu waliopata ulemavu palee tu walipozaliwa na hawajapata kuinuka maisha yao yote hapa duniani wasioweza hata kujisogeza wanategemea wauguzi ndugu wazazi wawasogeze na kuwapa huduma zote

Watakukumbusha kumshukuru M/Mungu na kutojikatia tamaa,
 
Pole sana ndugu. Ninakuelewa sana hasa hapo kwenye madeni. Hii hali ilishanitokea mwaka 2012 nikaona dunia ipo mabegani mwangu. Nilienda kwa mganga nikaishia kupoteza hela na kutofanikiwa kabisa. Nakumbuka niliishia kugombana na mganga. Nikajaribu kwa mama fulani mchungaji wa kilokole naye tukashindwana kwa sababu hata kile kidogo nilichokuwa napata anataka nimpe kama sadaka na mbaya zaidi alitaka nitoe mchango wa pesa mingi kununua vifaa vya muziki vya kanisa lake. Kwa upande wangu kilichonisaidia ni kuhamia DSM na kuanza kujitafuta from the scratch. Nilikuwa winga Kkoo kwa miaka miwili hadi pale nilipopata unafuu wa maisha.

Kuhusu madeni kaa chini na wanaokudai uwaeleze hali halisi uliyo nayo na kwaomba wakupe muda zaidi. Huenda pia kuna wanaoweza kukusamehe deni. Ila jitahidi uepuke madeni mapya. Kama wewe ni mwanaume jichanganye mtaani piga kazi yoyote ya halali ili mradi mkono uende kinywani. Vibarua vya ujenzi, kilimo na yoyote ile inayopatikana piga. Ukiwa Dar nenda Kkoo asubuhi kama mfanyakazi utapata dili kule.

Kutaka kujiua sio sahihi. Jipe muda kwanza. Kuwa mvumilivu.
Safi.sana mkuu umempa.ushaur.mzuri.sana

Nje ya mada mkuu.si njoo huku tujiunge kimtoa mkolon mweus.il vijana kama hawa tuwatengenezee fursa MBALIMBALI.kupunguza.vjna wasio na ajira maana serikal tawala imeshindwa kutatua tatizo.la ajira
 
Nimesoma attachment zako ambazo mwanajukwaa mwenzetu ametuma zilizonanyuzi ulizoziandika ila nimeelewa jambo kuna ,maisha mtu anahamasisha watu wapambane kusonga mbele ila yey kama yeye amekta tamaa ya kusonga mbele .
Kitu naona hapa anaona anaondoka ila hajakata tamaa kuwa unatakiwa kusonga hata ikiwa kuna watu unaishi nao hata ikiwa wabaya anatuachia ujumbe sisi tunaobakia
TUSIKATE TAMAA
 
Safi.sana mkuu umempa.ushaur.mzuri.sana

Nje ya mada mkuu.si njoo huku tujiunge kimtoa mkolon mweus.il vijana kama hawa tuwatengenezee fursa MBALIMBALI.kupunguza.vjna wasio na ajira maana serikal tawala imeshindwa kutatua tatizo.la ajira
Mkuu kuitoa CCM madarakani haitomhakikishia kijana fursa kama huyo kijana mwenyewe hataamua kufungua macho na kuziona fursa. Mimi nimeishi Kenya na Zambia ambako kunatajwa kama sehemu zenye demokrasia ya hali ya juu ila cha kushangaza fursa ni chache kuliko Tanzania. Vijana wa huko wana maisha magumu zaidi. Hawa viongozi wa upinzania wanachopigania ni wao kuingia madarakani na kufakamia keki ya taifa kama ambavyo wamekuwa wakiwatuhumu viongozi wa sasa. Ninakushauri endelea kuiunga mkono CCM na sera zake huku ukipiga vita baadhi ya viongozi wake ambao hukengeuka.
 
Maisha yangu yalipo nikama yamenikalia. Nimesoma ila masomo hayajanisaidia.nina maden kibao atamengin sijalipa.

Na tena mimi tuh ndio mtoto wa pekee kwetu nyumbani.baba na mama wote waniangalia. kiujumla nmechoka ata sion faida ya kuishi bora niendee zangu kaburin nikapumzike.

Maisha kwang ni machung sio matamu.saiv nafikiria ni mbinu gani ntakayo tumia nifike ahera mapema.

dawa ya tatizo ni kukabiliana nalo.

USICHOKIJUA UKIFA KWAKUJIUA UTAJUTA.

kwanza utarudishwa kisha utapewa maisha magumu .ara tatu ya uliyo yakimbia.

BI ADAMU HUA TUNATAWALIWA KIROHO USIJARIBU KUJIUA UTATESEKA SANA.

{ kama ulisha wahi kuota ndoto ya kutisha na un ahangaika kuji nusuru ila kila ukijaribu unashindwa. Basi hivyo ndivyo itakavyo kua baada ya kujiua.

{ halafu hao wanao kutegemea hiyo ndo zawad unataka kuwapa ?. kwakweli wewe ni mjinga kichwani hamna kitu suluhu ni kupambana kujiua ?. }


UKIFELI SANA JIUZE GAWA HATA VINYEO TU UPATE MTAJI.
 
Back
Top Bottom