Maisha mazuri ni yapi?

Maisha mazuri ni yapi?

bcsolution

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2013
Posts
394
Reaction score
177
Katika Dunia hii BINADAMU anahangaika asubuhi, mchana na usiku, ukimuuliza kwa nini? Anasema anatafuta maisha.. Maisha gani? atajibu maisha mazuri, ya namna gani? Atajibu nataka: Gari, nyumba, mke/mme mzuri, nk.. Sasa mbona kuna watu wana kila kitu lakini hawana raha katika Dunia hii?

Hebu tujiulize je maisha mazuri ni yapi?

La hasha ngoja nikupe siri ya kuwa na maisha mazuri=ni kuridhika na hali halisi ulo nayo, kuwa na hofu ya Mungu, kuishi vizuri na watu, kusamehe walokukosea, kuwa na Upendo na utu.. Hii ndo siri ya maisha mazuri.. Mungu akujalie hivi vyote...

Ewe MJA kumbuka, staili uliyoingia nayo duniani ndiyo hiyo hiyo utakayo ondoka nayo duniani. Ulikuja duniani ukilia na siku ya kuondoka duniani watalia.

Ulikuja duniani huna nguo wakakuvisha na utaondoka duniani huna nguo pia watakuvisha. Ulikuja duniani ukaogeshwa na utaondoka duniani watakuosha. Ulikuja duniani huwezi kutembea ukabebwa na utaondoka duniani huwezi kutembea utabebwa. Zinduka ewe mja, tubu haraka . Dunia ni chumba cha mtihani.

MUNGU aliumba Ardhi na Mbingu, Miti na Wanyama wala Hakujisifia lakini alipoumba kiumbe mzuri kama WEWE alijisifia na akasema "NIMEMUUMBA MWANADAMU KATIKA UMBO LILILO BORA"
 
Fahamu kuwa mwanadamu haridhiki hata siku moja. Ndio maana kila kukicha hutafuta.Na kusingekuwa na kifo,ungekuta hadi leo huu Adam na Eva still wana hustle.
 
we tatizo lako umekata tama na maisha una anza kulia lia tu neno lenyewe limesema tafuteni nanyi mtapata
tembelea blogs ya amka mtanzania ufurahiye
 
Umekata tamaa...mapema sana bro...keep on strugling...mambo itakuwa poa..tu..wake up..man
 
pia kwa kuongezea maisha mazuri ni pale unapokuwa na peace of mind mkuu.
 
Maisha mazuri ni pale utakapoishi pasipo wasisiwasi wa kesho! Kitu ambacho mwanadamu wa damu na nyama hato kaa akipate kwenye dunia hii. Thus why maasi na kuchanganyikiwa kote walkonako wanadamu wa dunia hii ya leo wamejikuta wanahamu ya kupata ila wapi.... Habari njema ni hizi maisha mazuri kwa dfn yangu hapo juu mwanadamu atayapata atakaporudi kwa njia ya muumba wake anae jua kusudi la maisha yake hapa duniani. To make thingz cplicated without jesus in you no life purpose to you.... Asomae na afahamu......
 
Back
Top Bottom