Maisha lazima yaendelee

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Mar 1, 2016
12,695
31,498
Sikiliza akili kubwa kama ifuatavyo:

Dunia hii imejaa mitihani mingi sana yaani tangu unazaliwa mpaka unarudi six feet under;

Utakabiliana na mambo mengi, kwa kuchagua au kwa lazima;

Utapoteza wapendwa na wapenzi wako;

Utaumwa na kuugua maradhi yanayotibika na yasiyotibika;

Utashutumiwa na kusingiziwa mambo ambayo haujafanya;

Utapigwa fitina, majungu na pengine kuchukiwa bila sababu ya msingi;

Utavunjwa moyo na uwaaminio na pengine utakata tamaa kabisa; na

Wakati mwingine utakosa hela, utakosa marafiki na kukosa amani na kujutia maisha yako.

Lakini akili kubwa inakuambia, maisha lazima yaendelee, huo ndiyo uanadamu, na hauko peke yako wote tunapita kwenye njia hiyo. Simama piga moyo konde, yote yatapita. Endelea kuamini siku utakapo kosa changamoto hizo hapo juu, basi kimbia hospitalini kuangalia kama umekufa au uko hai.

Kama unabisha, andamana.
 
Ila amini usiamini mkuu hayo yote uliyoyaeleza hapo kwa wengine ni hadithi tuu na hiyo yote ni kutokana na watu wao wa karibu walivyowatengenezea mazingira rafiki, kuna watu wanaponda raha kila kukicha hawajui kitu kinaita shida wala Chuki na inakua hivyo hadi mwisho wa maisha yao

Note but: ukielewa Dunia umeelewa maisha na watu wake.
 
Ila amini usiamini mkuu hayo yote uliyoyaeleza hapo kwa wengine ni hadithi tuu na hiyo yote ni kutokana na watu wao wa karibu walivyowatengenezea mazingira rafiki, kuna watu wanaponda raha kila kukicha hawajui kitu kinaita shida wala Chuki na inakua hivyo hadi mwisho wa maisha yao

Note but: ukielewa Dunia umeelewa maisha na watu wake.
Mkuu, pesa na raha siyo tiba ya hayo mambo tajwa hapo juu. Hakuna watu wenye stress kama matajiri
 
Aaaah mimi nazungumzia wategemezi wao ambao wamezaliwa ktk familia hizo za kitajiri, hebu fikiria mtoto wa Bakheresa anaijua njaa au shida? Ukiwa na pesa hautazongwa na hayo makandokando indeep
Mkuu, shida inaweza ikaanzia ata kati yao wenyewe, yaani watoto wenyewe na ndugu zao wakazinguana na maisha yasinyooke kama unavyofikiria
 
Back
Top Bottom