Nimefanya kazi kwenye makampuni mengi ya uchimbaji madini, kwa miaka takribani mitano bila kujenga nyumba, kila nilipofika nyumbani kwa ajili ya likizo baba alikuwa ananiuliza swali ambalo lilikuwa linanichoma moyo sana....!
Mwanangu vip ushaanza ujenzi? Kwa masikitiko nilikuwa sina jibu la kumpa,
Kilichokuwa kinaniuma zaidi ni wenzangu nilianza nao kazi na wengine walikuja nyuma yangu walikwisha anza ujenzi, nilikuwa naumia sana ndani ya nafsi yangu bila kumweleza mtu, kwa sasa nilishaanza ujenzi na nipo kwenye lenta, Mungu ashukuriwe.