Maisha hayasimami, ni lazima yaendelee

Maisha hayasimami, ni lazima yaendelee

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,350
Umefanikiwa kujenga kibanda cha vyumba viwili, chumba chako ni master bedroom na chumba cha pili ni cha kawaida. Unapata uhamisho, kwa sababu za kiusalama unamtafuta kijana wa kukaa. Chumba chako unafunga.

Kijana anakuta nyumba full furnished na king’amuzi juu, flat screen “60. Unamaliza mshahara kila mwezi na nje ana ki sehemu cha kupanda mihogo, viazi vitamu na mchicha. Hata kuku ameanza kufuga kwenye kibanda alichojenga.

Baada ya miaka miwili unarudi unamkuta anaishi na mwanamke na wamepata mtoto na kuna dada anawasaidia ulezi. Dada amewekewa godoro sebuleni. Chumba chako hawajagusa.

Hujakaa vizuri mtoto analetwa na kwa heshima wamempa jina lako. Maisha ya kijana ilibidi yaendelee akiwa amepata kibarua. Kijana ni muaminifu lakini unaona nyumba imekua ndogo. Utachukua uamuzi gani?
 
Namtafutia room ya Bei nafuu namlipia Kodi ya mwaka mzima na Kama Nina uwezo namtafutia kibarua
 
Kama una uwezo mpangie chumba sehemu nyingine
 
Ataendelea kukaa hapo mpaka atakapokuwa amejipanga na kuamua kuhama.
 
Nitampa ofa ya kumlipia chumba kwa miezi 6 kipindi anaweka mambo yake sawa.
 
Kwa mr
Umefanikiwa kujenga kibanda cha vyumba viwili, chumba chako ni master bedroom na chumba cha pili ni cha kawaida. Unapata uhamisho, kwa sababu za kiusalama unamtafuta kijana wa kukaa. Chumba chako unafunga.

Kijana anakuta nyumba full furnished na king’amuzi juu, flat screen “60. Unamaliza mshahara kila mwezi na nje ana ki sehemu cha kupanda mihogo, viazi vitamu na mchicha. Hata kuku ameanza kufuga kwenye kibanda alichojenga.

Baada ya miaka miwili unarudi unamkuta anaishi na mwanamke na wamepata mtoto na kuna dada anawasaidia ulezi. Dada amewekewa godoro sebuleni. Chumba chako hawajagusa.

Hujakaa vizuri mtoto analetwa na kwa heshima wamempa jina lako. Maisha ya kijana ilibidi yaendelee akiwa amepata kibarua. Kijana ni muaminifu lakini unaona nyumba imekua ndogo. Utachukua uamuzi gani

Umefanikiwa kujenga kibanda cha vyumba viwili, chumba chako ni master bedroom na chumba cha pili ni cha kawaida. Unapata uhamisho, kwa sababu za kiusalama unamtafuta kijana wa kukaa. Chumba chako unafunga.

Kijana anakuta nyumba full furnished na king’amuzi juu, flat screen “60. Unamaliza mshahara kila mwezi na nje ana ki sehemu cha kupanda mihogo, viazi vitamu na mchicha. Hata kuku ameanza kufuga kwenye kibanda alichojenga.

Baada ya miaka miwili unarudi unamkuta anaishi na mwanamke na wamepata mtoto na kuna dada anawasaidia ulezi. Dada amewekewa godoro sebuleni. Chumba chako hawajagusa.

Hujakaa vizuri mtoto analetwa na kwa heshima wamempa jina lako. Maisha ya kijana ilibidi yaendelee akiwa amepata kibarua. Kijana ni muaminifu lakini unaona nyumba imekua ndogo. Utachukua uamuzi gani?
Huyo jamaa atakuwa one in a million, kwa ule uaminifu wake nitajilipua nimpangie chumba Kisha nimlipie Kodi ya mwaka mzima na pia nitampa mtaji akaanzisha biashara Yake huko.
 
Nyie mnaosema nitampangishia nyumba nimlipie miezi sita ... wengine mtamnunulia kiwanja....hyo hela utaitoa wapi aisee ya kupangisha na kununua kiwanja? umejenga vyumba viwili Ina maana mshahara wako Ni laki mbili
Kwa hyo direct huyo jamaa utamtoa ndukiii

Binafsi ningemuachia nyumba nirudi kwa baba na mama
 
Mpangie chumba na sebule miezi 6

Mpe godoro kitanda jiko la mkaa unga mchele vyombo kidogo vya kuanzia maisha

Aende akapambane


Halafu ukihama si upangishe tu nyumba kuepuka kero kama hizo
 
Nyie mnaosema nitampangishia nyumba nimlipie miezi sita ... wengine mtamnunulia kiwanja....hyo hela utaitoa wapi aisee ya kupangisha na kununua kiwanja? umejenga vyumba viwili Ina maana mshahara wako Ni laki mbili
Kwa hyo direct huyo jamaa utamtoa ndukiii

Binafsi ningemuachia nyumba nirudi kwa baba na mama

yaani umuachie nyumba yako wewe ukajibane kwa wazazi
 
Back
Top Bottom