Mahusiano ya mbali ni balaa

Mahusiano ya mbali ni balaa

Tuachane unafiki na tuongee ukweli.

Mke kufanya kazi na kuhamishwa ni balaa sana bora asiwe na kazi au afanye karibu na mumewe.
 
Mwanandoa anayehamia mkoa mwingine kikazi akaweka doa kwenye ndoa anamaanisha kwamba alikuwa anaishi na mwenzake kinafiki. Yafaa adumishe ndoa yake kwa mbinu zozote zile bila kutumia uhamisho kama kisingizio cha kuhatarisha uhai wa ndoa.
Mimi hili swala la umbali huwa nalikataa kabisa. Hizi ni tabia tu za watu, umbali has nithing to do nazo.
Hizi justifications za kiuana harakati hizi ambazo zinamlemaza na kumdekeza mwanadam ndiyo zinazoibomoa jamii na dunia.
Huko tuendako wanaotetea umbali watakuja kutuaminisha kwamba, ni sahihi kwa wafungwa kulawitiana sababu wametengwa na hawaruhusiwi kuonana na wanawake, yaani hawapewi fursa ya kufanya mapenzi.
 
Mimi kama nimeolewa sichepuki ila haya mengine unaweza kukuta uko muaminifu unavumilia ukimngojea mwenzio kumbe unayeteseka kwa ajili yake kila siku anapata huduma.
🤣 Subiria uolewe kwanza, hata walioolewa walikuwa na akili kama hizi before!
 
Mkuu, trust me, long distance relationship haina tatizo.
Kuna long distance relationship na mahusiano ya mbali😃.
Long distance ni mahusiano na aliyepo nje ya nchi. Haya huwa hayana changamoto kivile.
Na mahusiano ya mbali ni yule aliyepo mikoani, yaani upo kikazi Tunduru au Namtumbo au Sikonge halafu shemeji yetu umuache Dar😃, hii huwa inafeli hii, yaani inaenda.
Hahahahahah kwamba mtu akiwa uzunguni hawezi kupigwa bolo ila akiwa hapa umatumbini ni dakika 0 tu? 🤣🤣🤣 That doesnt make sense mtu wa hovyo ni wa hovyo tu hata akiwa marekani.
 
Siku mkikutana ndio mwanzo wa kuanza kugeuza geuza simu juu chini🤣 na kuwekeana nywila za kwenda. Mala kupaisha ndege 😀😀😀!!!

Wabongo hamna kitu tunaweza fanya kikamilifu ukiacha kifo tu.
Mapenzi ya mbali ni kichocheo maradufu kwa wapenzi kuchepuka na hii inapelekea mahusiano kuvunjika mana kila mtu anakuwa bize na michepuko yake huko alipo

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Kwa afya, usalama na ustawi wa akili yako wakati mwingine inabidi kuishi mbalimbali hasa Kama upendi makuu na ulikosea kuoa au kuolewa.
Kumbuka uchumba ni feki life ndoa ni maisha halisi.Huwezi feki ndoa.
Tabia ya mtu huwezi ijua bila kuishi na mtu.
 
Wote mliopo kwenye Mahaba mazito humu, ndani ya mwezi huu siri zenu zitafichuka na Mtaachana wote...
Rubish
 
Mahusiano ya mbali tuwaachie umoja wa mataifa.....wabongo wanafki sana...yaliyonikuta ni makubwa
 
Mahusiano ya mbali yanachangamoto nyingi hasa suala la uaminifu.Umbali huu unawezasababishwa na kazi Mfano mhusika mmoja anafanya kazi Kilimanjaro mwingine yupo mtwara.Kuonana ni miezi kadhaa hadi mwka.Hii inaleta changamoto kwani wanamahusiano hawa wasipoweza kudhibiti hisia wanawezajikuta wanamahusiano juu ya mahusiano.Kudhibiti hisia yataka moyo na mungu.
=====================================================Kuna mhusika mmoja alimuibukukia mke wake kwa kumshtukiza akakuta viatu vya mwanaume mwingine na koti kuuliza akaambiwa ni vyako nilikununulia hajakaa sawa akakuta mwenye navyo anaingia bila hata ya hodi ati anauliza huyu nani du stor ni ndefu nitatafuta muda niwape uhondo wa kilichoendelea lakini itoshe kusema kukaa pamoja na mwenza ni jambo jema hata lisipoweza kufanya kazi kwa 100% lakini litapunguza kwa kiasi suala la uchepukaji na kupunguza magongwa ya zinaa mtaani.
Yani mwenye mali ndio anauliziwa huyu nani,inaonyesha jamaa hapo ndio kwake na wewe ni mvamizi...
 
Ni unafiki niliachana na demu week tu mwamba kawekwa Dp
 
Nipo kwenye ndoa.

Watu mnadanganyana tu hapa. Ndoa ya mbali ni ngumu sana.

Me wife Aki safiri wiki moja tu nateseka vibaya mno. Eti ndo maisha yetu yote akae mbali tunaonana kwa mwaka mara 2? Hakutakua na ndoa hapo.

Tulishakubaliana na wife akihamishwa kikazi anaacha kazi, ataendelea kusimamia miradi na business zetu hapahapa.

Siwezi ku risk ndoa, familia, malezo ya watoto sababu ya kazi
 
Kuna hao waliokuwa na ndoa yao, mume mkoa huu na mke mkoa ule. Walidumu miaka na miaka.

Baadaye walikata shauri mume amfuate mke wake mkoa ule ili waishi pamoja, na walifanikiwa.

Baada ya kuanza kuishi pamoja miezi kadhaa tu ndoa ikavunjika.
Grave mistake. Huwezi kuishi mbali na mke for years halafu utegemee kwamba mnaweza ku cohabit mambo yakaenda mswano tu. Sio kwa wabongo naowajua 🤣
 
Back
Top Bottom