Bazobonankira
Senior Member
- Jan 18, 2007
- 120
- 61
Wasalaam,
Kidogo ningependa kupata msaada katika hili. Kumekuwa na tetesi na hata mara nyingine ushahidi wa waziwazi au wa kimazingira juu ya kuwepo uhusiano wa kimapenzi kati ya waandishi wa habari na watoa habari wao.
Binafsi, sidhani kama ni jambo jema kimaadili, hasa ya uandishi wa habari. Wapo wanaoamini kuwa uhusiano huu si tatizo, alimradi tu unakurahisishia kupata habari. Pia wapo wanaoamini kuwa huku ni kuidhalilisha taaluma na wadau wote! Wapo waliodiriki kutembea na mawaziri, wakurugenzi wa idara nyeti, wakuu wa wilana au mikoa, wanasiasa mashuhuri na wengine hata viongozi wao makazini au katika taasisi shirikishi.
Wadau mnasemaje?
Kidogo ningependa kupata msaada katika hili. Kumekuwa na tetesi na hata mara nyingine ushahidi wa waziwazi au wa kimazingira juu ya kuwepo uhusiano wa kimapenzi kati ya waandishi wa habari na watoa habari wao.
Binafsi, sidhani kama ni jambo jema kimaadili, hasa ya uandishi wa habari. Wapo wanaoamini kuwa uhusiano huu si tatizo, alimradi tu unakurahisishia kupata habari. Pia wapo wanaoamini kuwa huku ni kuidhalilisha taaluma na wadau wote! Wapo waliodiriki kutembea na mawaziri, wakurugenzi wa idara nyeti, wakuu wa wilana au mikoa, wanasiasa mashuhuri na wengine hata viongozi wao makazini au katika taasisi shirikishi.
Wadau mnasemaje?