Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 12,151
- 44,071
Nimesikiliza na kutazama kwa makini mahojiano kamili kati ta Rostam Aziz na Tido Mhando ambayo yamerushwa hewani kupitia Azam Tv (UTV) kuanzia mida ya saa tatu usiku mpaka mida ya saa nne na dakika kadhaa usiku huu (tarehe 5/9/2025). Na bila kumumunya maneno, mahojiano yale yalikuwa ni maigizo ya kisanii (full staged), yaani Tido Mhando 'ametumika' kufanya coverage, maswali yaliandaliwa na majibu yakaandaliwa na wahusika walifanya mazoezi ya pamoja ya mahojiano, ushahidi ni huu hapa.
1. Mahojiano hayakuwa live na yalikuwa na vipande vingi vilivyokatwa katwa na kuungwa ungwa kiufundi baada ya kuhaririwa kabla ya kurushwa hewani.
2. Maswali yote Tido alikuwa akiyasoma kwa mtitiriko kutoka kwenye notebook yake na Rostam alikuwa akiyajibu kwa mtiririko huku akionyesha kama anayajua maswali yote na mtiririko wake.
3. Kuna maswali kadhaa hayakuwa relevant kabisa na lengo la mahojiano yale lakini yaliulizwa kimakusudi ili kumpa Rostam public sympathy and positive attention (kwa mfano suala la bima ya Afya, utoaji misaada kwa jamii nk).
4. Katika maswali yote ya msingi ambayo Tido aliuliza hakuna hata swali moja Tido aliamua kumbananisha Rostam katika kona ya kumchimba. Yaani jibu la msingi la Rostam lilishindwa kuzaa swali la kukera kutoka kwa Tido Mhando. Kwa kifupi kabisa, Tido Mhando alilidhishwa na kila jibu la Rostam katika swali la msingi.
5. Kuna maswali mengi sana ya kimsingi ambayo Tido alikwepa kabisa kumuuliza Rostam Aziz. Ni kama vile Rostam alitaka kuulizwa yale maswali ambayo angependa tu kuulizwa na sio vinginevyo. Kwa mfano, utata wa kifo cha Magu nk.
NOTE:
Kwa wataalamu wa tasnia ya uandishi wa habari wakichunguza haya mahojiano wanaweza kumtazama Tido kama mwandishi asiyekuwa na chembe ya sifa za uandishi wowote wa habari ukiwa utamlinganisha na mwanafunzi yoyote wa ngazi ya cheti aliyejiunga na chuo cha uandishi wa habari na kukaa darasani nusu mwezi kujifunza uandishi wa habari. It was a poor interview!
1. Mahojiano hayakuwa live na yalikuwa na vipande vingi vilivyokatwa katwa na kuungwa ungwa kiufundi baada ya kuhaririwa kabla ya kurushwa hewani.
2. Maswali yote Tido alikuwa akiyasoma kwa mtitiriko kutoka kwenye notebook yake na Rostam alikuwa akiyajibu kwa mtiririko huku akionyesha kama anayajua maswali yote na mtiririko wake.
3. Kuna maswali kadhaa hayakuwa relevant kabisa na lengo la mahojiano yale lakini yaliulizwa kimakusudi ili kumpa Rostam public sympathy and positive attention (kwa mfano suala la bima ya Afya, utoaji misaada kwa jamii nk).
4. Katika maswali yote ya msingi ambayo Tido aliuliza hakuna hata swali moja Tido aliamua kumbananisha Rostam katika kona ya kumchimba. Yaani jibu la msingi la Rostam lilishindwa kuzaa swali la kukera kutoka kwa Tido Mhando. Kwa kifupi kabisa, Tido Mhando alilidhishwa na kila jibu la Rostam katika swali la msingi.
5. Kuna maswali mengi sana ya kimsingi ambayo Tido alikwepa kabisa kumuuliza Rostam Aziz. Ni kama vile Rostam alitaka kuulizwa yale maswali ambayo angependa tu kuulizwa na sio vinginevyo. Kwa mfano, utata wa kifo cha Magu nk.
NOTE:
Kwa wataalamu wa tasnia ya uandishi wa habari wakichunguza haya mahojiano wanaweza kumtazama Tido kama mwandishi asiyekuwa na chembe ya sifa za uandishi wowote wa habari ukiwa utamlinganisha na mwanafunzi yoyote wa ngazi ya cheti aliyejiunga na chuo cha uandishi wa habari na kukaa darasani nusu mwezi kujifunza uandishi wa habari. It was a poor interview!