Mahari shilingi milioni 5?

Mahari shilingi milioni 5?

kuna mbaba alilewa akalopoka anataka mahari IST
Tulicheka sana..demu alijiskia vibaya mshua ndo ivyo.
 
Milioni 5?Duuuuh!naona kama kukomoana jamani!Yani zote hizo ni mahari au mtaji wa biashara?
Mkuu huyu ukishamlipia mahari akija hakuna uzazi wa mpango anafyatua tu nakufyatua tu unamuambia akuzalie watoto 15 akihoji unamuambia kwani kuna balance ya mahari sijalipa?
 
Kawaida kwa zamani,ila karne hii mahari kubwa hivyo,duuuh vidume tugonge tu ili kupata watoto
 
Unalipa milioni tano alafu unaozeshwa mtumba ambao masela flani wamepima sana oilnl
 
Huyo bi harusi mtarajiwa yupoje? Hebu tuwekee picha kama unayo,mayb anaendana na hiyo milion 5.
 
Wakubwa mbona mnalalamika saana aseeh. Huku
Tunatoa
ng'ombe minimum 10
Mbuzi minimum 32
Bado wale wa kula honeymoon minimum mbuzi 4
Sherehe unaweza kuchinja mbuzi wa 3 na ng'ombe 1. Matumizi mengine m1

Na ukitoa wachache ni bonge la shame kwa ukoo na rika lako. Ila sasa sisi mkizinguana kwenye ndoa unaruhusiwa kudai mahari yako yote kama binti wapo vizuri wanarudisha kama hawapo vizuri unamuuzia mwanaume mwingine
 
Leo nimemsikia mtu mmoja akisema kuwa ndugu yao anaejiandaa kuoa, amepangiwa mahari ya shilingi milioni tano. Na kwamba ndugu wameamua kuchangishana ili walipe mahari hiyo kumsaidia ndugu yao.

Kilichonifanya niilete mada hii hapa kwa majadiliano ni kuhusu kiwango hicho cha mahari, ambacho kwangu nakiona ni kikubwa sana. Je, hiyo si ni sawa na kumfanya binti kama bidhaa kweli.


Kama ni mpaka wachangishane ndugu maana yake huyo mtu ni masikini na hyo 5M yake yaweza fanyika mtaji na mwanamke kama hataki kuja kwa mahali ya laki tano akae kwao,aache uoga,siku hzi hakuna mahali za kukomeshana kwa mwanamke mwenye wazazi wanaojua maisha yakoje
 
Back
Top Bottom