Mahakama ya Kadhi ni nini?

Mahakama ya Kadhi ni nini?

Mahakama ya kadhi tayari inatambulika Tanzania Zanzibaro,ambao wanapinga ni wakristo wa Tanganyika ambao wao ni tofauti na Wakristo wa nchi zingine za Africa mashariki ambazo zina mahakama ya kadhi na raia wake wanaishi kwa amani na upendo.
 
Je, kwa sasa Rais angekuwa Mkristo ingekuwaje?
Watanzania tuamke tuache mambo ya Upumbavu, mahakama ya kadhi itasaidia kuondoa ufisadi Tanzanioa? Watoto wetu watapasoma Bora kama sisi tulivyosoma huko nyuma? Mahakama itabadili Katiba ya kipumbavu ambayo inapigiwa chepeo kwa sasa?
Kila Taifa leo hii imejikita kwenye maendeleo na si ktk Udini. Waislamu, Wakristo na wengineo tuungane kulitetea Taifa letu ambalo linatafunwa na wachache kwa maslahi yao.
Isitoshe hao wanaotaka hii Mahakama wengi wao hawajui kama ni mfuko wa Serikali ndo itaendesha hizi Mahakama, sasa je, Serikali itafaidika na nini kupitia mahakama hizi?
 
Kwa wale wanaofanya kazi, hasa walioajiriwa ni rahisi kukata pesa zao, wale wafanya biashara wapeleke michango yao wenyewe kwa sababu Mahakama ni kwa ajili yao
unajua kukata pesa ya mtu bila ruhusa yeye kuridhia ni kosa au hujui naomba nikuulize kwa nini mnatumia nguvu nyingi sana katika kutaka hizi mahakama wakati uwezo wa kuziongoza hamna.
 
Mahakama ya kadhi tayari inatambulika Tanzania Zanzibaro,ambao wanapinga ni wakristo wa Tanganyika ambao wao ni tofauti na Wakristo wa nchi zingine za Africa mashariki ambazo zina mahakama ya kadhi na raia wake wanaishi kwa amani na upendo.

Nchi ipi inayoishi kwa amani na upendo A.Mashariki?
 
Mahakama ya kadhi tayari inatambulika Tanzania Zanzibaro,ambao wanapinga ni wakristo wa Tanganyika ambao wao ni tofauti na Wakristo wa nchi zingine za Africa mashariki ambazo zina mahakama ya kadhi na raia wake wanaishi kwa amani na upendo.
labda inatambulika huko misikitini kwenu tuuuu.
 
unajua kukata pesa ya mtu bila ruhusa yeye kuridhia ni kosa au hujui naomba nikuulize kwa nini mnatumia nguvu nyingi sana katika kutaka hizi mahakama wakati uwezo wa kuziongoza hamna.

Mkuu, hii nchi ina majanga mengi mno ila watu ndo kwanza wanatafakari Udini, Hivi wakipewa hizo Mahakama hawaoni ndio sababu ya Udini kupamba moto zaidi?
 
Mkuu, hii nchi ina majanga mengi mno ila watu ndo kwanza wanatafakari Udini, Hivi wakipewa hizo Mahakama hawaoni ndio sababu ya Udini kupamba moto zaidi?
mkuu wanahangaika bure nani atawapa hizo mahakama serikali haina dini .Pinda aliwadanganya ili apate zile kura za NDIYO katiba ya ccm baada ya hapo hakuna kitachofanyika tena .
 
Watu wengi wanaojadili hasi hili swala wana mitazamo miwili. Mtazamo wa kwanza ni chuki za kiimani na mtazamo wa pili ni ujinga wa kutokujua nini mahakama ya kadhi na majukumu yake kwa nchi kama yetu ya Tanzania.Ukiwa upo kwenye mtazamo wa kwanza, upo sahihi kwa sababu hilo ni jambo ambalo lipo moyoni mwako na kama huwezi kupambana na ashki za moyo wako basi litaendelea kuwepo tu kama vumba la samaki wa maji ya ngama.Na kama upo kwenye mtizamo wa pili basi ni kuendelee kuongeza kiwango cha ujinga kujadili na kulitolea maoni jambo ambalo huma elimu au ufahamu nalo.
Hakuna hoja yoyote hapa. Unakwepa ukweli wa kilichopo kwenye uzi, unatoa maelezo yasiyo na hoja bali hisia.
 
ujinga wako ni kuwa hujajua kiini cha malalamiko, tatizo sio hiyo mahakama tatizo ni serikali kuhusishwa
Huyo mashodi haelewi. Ukihusisha serikali maana yake wananchi wote wanalazimishwa kufuata imani moja katika nchi. Hajaelewa kilichopo kwenye uzi.
 
wakina nani hao , swala halijakubaliwa na wala halitopitishwa , zaid ya JF kuna sehemu nyngne umewakuta watu wakijadili ama hata kulikumbuka?

Manyang'au ni CCM wanaotafuta kura kwa kulazimisha kila mtu kushiriki ibada ya imani nyingine kwa lazima.
 
wakina nani hao , swala halijakubaliwa na wala halitopitishwa , zaid ya JF kuna sehemu nyngne umewakuta watu wakijadili ama hata kulikumbuka?
Manyang'au ni viongozi wa CCM waliofilisika na kujawa na tamaa ya kung'ang'ania madaraka wanaotafuta kura kwa kulazimisha kila mtu kushiriki ibada ya imani nyingine kwa lazima.
 
mkuu wanahangaika bure nani atawapa hizo mahakama serikali haina dini .Pinda aliwadanganya ili apate zile kura za NDIYO katiba ya ccm baada ya hapo hakuna kitachofanyika tena .

Harafu hawa jamaa wanadanganyika kwa kijinga sana, angalia hata leo USA na Allies wake wanavyowanyanyasa.
 
Dawa hapa nchi igawanywe wkristo warudi kanda ya ziwa na kati waislam waende pwani hakuna jinsi ccm inataka Kura za waislam!
 
Wewe unakatwa kodi kwa ajili ya kuendesha mahakama ya kazi i mean kazi sio kadhi unajua?
Hii ni mahakama ya kazi,hizi kazi ni za akina nani?
Unakatwa kodi kwa kwa kuendesha baraza la usuluhishi fair competition tribunal ambayo wafanya biashara wakubwa tu linawahusu..wewe unanufaika nini la kodi unayokatwa kuendesha hizo mahakama na mabaraza?
Ni kwa namna gani hili ni tatizo?
Unadhani waislam hawachangii chochote kwenye misamaha ya kodi inayopata makanisa?
Unasema msamaha wa kodi halafu unasema "wanachangia",yaani wewe hujui hata maana ya msamaha
..akili yako na ubongo wako imejaa ukungu mzito huoni wala huwezi kufikiria zaidi ya hapo..upo upo tu kama zuzu flani
Naona hapa wewe ndio zuzu,kama unabisha tupe maelezo kuhusu haya .....!!
 
Wewe unakatwa kodi kwa ajili ya kuendesha mahakama ya kazi i mean kazi sio kadhi unajua? Unakatwa kodi kwa kwa kuendesha baraza la usuluhishi fair competition tribunal ambayo wafanya biashara wakubwa tu linawahusu..wewe unanufaika nini la kodi unayokatwa kuendesha hizo mahakama na mabaraza? Unadhani waislam hawachangii chochote kwenye misamaha ya kodi inayopata makanisa?..akili yako na ubongo wako imejaa ukungu mzito huoni wala huwezi kufikiria zaidi ya hapo..upo upo tu kama zuzu flani

Wewe njoo na hoja zinazoeleweka na siyo kuja na hoja zisizokuwa na msingi. Kwanza kama ni misamaha sasa waislam wanachangia nini kwenye hiyo misamaha? Zaidi ni kwamba taasisi inayoongoza kwa kusamehewa kodi kubwa ni taasisi zilizo chini ya Agha Khan hao ni wakristu au makanisa? Pili hayo mabaraza uliyoyataja kama fair competition commission je ni ya kikristu? Huko wote wenye migogoro ya kibiashara huwa wanaenda huko bila kujalisha dini. Sanifu hoja zako vizuri na urejee hapa
 
Watu wengi wanaojadili hasi hili swala wana mitazamo miwili. Mtazamo wa kwanza ni chuki za kiimani na
Code:
[SIZE=4][COLOR=#0000ff]mtazamo wa pili ni ujinga wa kutokujua nini mahakama ya kadhi[/COLOR][/SIZE]
na majukumu yake kwa nchi kama yetu ya Tanzania..

sababu zako zote mbili sio kweli wengi wao wanawaza kodi zao, kwanini mtake kadhi halafu igharamiwe na kodi ya Mkristo wakati hafaidiki na chochote kutoka kwenye hiyo kadhi,
NASHAURI MAHAKAMA YA KADHI IANZISHWE LAKINI MJIGHARAMIE WENYEWE.
Pili hapo kwenye red sio kweli kwani Tanzania haina dini ila watu wake ndiyo wana dini. FULL STOP.

halafu usini quote mana sitakujibu
 
Jana nilimuona yule bwana anayeendesha kipindi cha kiislamu chanel ten akidadavua vilivyo umuhimu wa mahakama ya kadhi na kujaribu kuwatoa watanzania hofu kuhusu jambo hili. Nilikubaliana naye kwa kiasi kikubwa kwani alikuwa na hoja zenye mantiki fulani.

Ila mahali aliponitia wasiwasi ni pale aliposema kwamba muswada wa kuanzisha hii mahakama uliopo bungeni sasa haupaswi kuacha mwanya wowote wa kuruhusu mwislamu kuwa na hiari ya kuchagua kupeleka kesi za mirathi, ndoa talaka, na mengine kama hayo kwingine kokote zaidi ya katika mahakama za kadhi. Kwamba iwe ni lazima kwa waislamu wote kupeleka kesi zao hizo kwa kadhi.

Hili litakuwa jambo la ajabu kidogo kama litatokea kwa sababu sio waislamu wote wanaihitaji mahakama ya kadhi. Mfano Wasunni kwa kiasi kikubwa wanaipinga mahakama hii. Pia wapo waislamu wengi wasingependa kesi zao zihukumie huko kwa kadhi. Sasa kusema kwamba sheria inatakiwa ilazimishe waislamu wote kupeleka kesi zao za miradhi, ndoa, talaka, n.k katika mahakama ya kadhi si kuingilia uhuru wa watu?

Inaonekana hili pendekezo limetokana na ile hofu ya malalamiko kwamba italazimika mahakama za kadhi ziwepo na hapo hao zile za kawaida zilizokuwa zinashughulikia mambo ya waislamu ziendelee kuwepo ili ku"accomodate" wale waislamu wasiopenda kupeleka kesi zao katika mahakama za kadhi ambazo kimsingi zitakuwa chini ya Bakwata. Hapa ninaongelea ishu ya gharama ambazo serikali itabidi ibebe kuendesha mahakama hizo. Kwa hiyo kukwepa hoja ya ghrama za kuendesha mahakama mbili zinazoshughulikia mambo yaleyale labda ndio hoja hii ikaletwa.

Hivyo basi ni muhimu huu utata kuondolewa kabla ya kufikria mambo mengine. Yaani, je ni sahihi kuwalazimisha waislamu hata walio madhehebu mengine kupeleka mashauri yao katika mahakama za kadhi kama shekhe alivyoshadidia jana chanel 10? na kama waislamu wanatakiwa kuwa huru kuchagua mahakama je gharama si zitakuwa mara dufu? (Hapa assumption ni kwamba serikali itakubali kugharamia mahakama za kadhi).
 
Harafu hawa jamaa wanadanganyika kwa kijinga sana, angalia hata leo USA na Allies wake wanavyowanyanyasa.
mkuu hawa waislamu wanaotaka mahakama za kadhi hawajui madhara yake wapo kama bendera fuata upepo wanatetea ujinga na utumwa .
 
Back
Top Bottom