Siku za hivi karibuni kumetokea mjadala mzito kuhusu mahakama ya Kadh.Napenda kuchukua nafasi hii kuwomba wana JF bila ushabiki tujadili hili.Kwanini watu wengi hasa Wakristo wanahofu na mahakama ya kadh
1.Watanzania tumelelewa kwa upendo,ukabila na dini zetu siyo utambulisho wa Mtanganyika.Hivyo watu wengi wasiyo Waislamu wanona hii italeta utengano kati yao.Wakristo na Waislamu wanfaidiana,wanategemeana kwa kila kitu.Wanafikiri ikiwa Mahakama hii itaanzishwa watawakosa ndugu zao Waslamu.Ni sawasawa mtu umeoa mke alafu uone kuna sheria inatungwa ya kusukumia mbali uhusianao huo.
2.Ndugu zetu wanafikiri Wakristo ni Wakatoliki tu,ndo maana asubuhi ya leo nimemsikia shehe maarufu hapa nchini akiwa Chanel Ten akisema Wakristo wanafaidika na sheria za nchi hii ambazo zimerithiwa toka kwa Waingereza yaani COMMON LAWS.Kwa taarifa yake( kama yumo humu JF aje asome hapa,)anapashwa kujua hili.Mkristo ni nani?Mristo ni yule anayeenenda kama Kristo.Ingawa hatuwezi kuwa kama Kristo kwa asilimia 100 lakini Kristo anatukamilisha siku hadi siku,imani moja kwenda nyingine.Utamtambuaje mtu kuwa huyu ni Mkristo?ni Yule anayeifuata sheria ya Kristo.Yesu Kristo anasema mtu akinipenda atazishika amri zangu.Biblia inaendelea kusema kuwa mtu akishika yote akajikwaa katika moja anakuwa na hatia mbele za Mungu wa Wakristo.Tanzania ina Wapentekoste karibu million 11,hawa hizi Sheria zinazoitwa COMMON LAWS haziwahusu kabisa.Mfano moja kwa nini haziwahusu ni talaka.Talaka ni kati ya mahitaji yanayowasukuma Waislamu kupata mahakama hii ili washughulike ki-imani tatizo hili.Wapetekoste wanaamin kuwa ni mke mmoja na mme mmoja mpaka kifo kiwatenganishe.Mke mmoja na Mme mmoja si lazima wafanye sherehe Kanisan,wakishakubaliana na wazazi wa pande zote mbili basi ndoa uwa imefungwa tayari.Siyo lazima kuvaa Shera,ndoa ya kwanza ya Baba yetu Adam hawa kuvaa Shera.Ndiyo maana ukijiunga na Upentekoste kuna malipizo ya ndoa.Kama unaishi na mke ambaye si wako unamwacha unamrudia wa kwanza hata kama alishaolewa kwingine,zungumza na Mungu akurejeshee mke wako.Hiyo ndo kanuni.Walimuuliza Yesu wakati alipokuwa hapa Dunia
kuwa Musa aliwapa sheria ya talaka,aliwajibu 'alifanya hivyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao tangu mwanzo Mungu hakupenda hivyo,ni mke mmoja mpaka kifo kinawatenganisha.Ukiruhusu talaka wewe siyo Mkristo.
Tukisha yajua haya sasa twende kwenye hoja yenyewe.Waislamu wanatolea mifano mingi nchi za Rwanda,Kenya na Uganda kuwa wana Mahakama ya Kadhi,huu si mfano mzuri,tunaona wenzetu walivyo na shida na misigano katika maisha yao,yanayotokea huko kila mtu anyajua.Umoja wetu umetengenezwa na waasisi wa Nchi hii,ndiyo maan Tanzganyika haina dini(Secular State) Viongozi walisisitiza hili tangu mwanzo ili kuleta umoja na usatawi wa Taifa hili.Mkiwa na nchi yenye mfumo kama wa Tanganyika inabidi kila mmoja akubali kupoteza baadh ya mambo fulani.Sawa sawa umeoa mwanamke anatabia zake kila mmoja napoteza mambo yake ya msingi ili kujenga familia yenye umoja.
Pia Zanzibar inahusishwa na mfano kuwa wao wamewezaje kuwa na Mahakama ya Kadhi?Zanzibar karibu 99.9%(ingwa sina uhakika na asilimia hizi) ni Waislamu,sehemu kama hii jambo la Mahakama ya kadh ni rahisi kutekelezwa.Wote tunajua ni jinsi gani wakati wa mfungo wa ramadhani wakrist wanavyopata shida huko nafikiri kila mmoja anjua yaliyo watokea.
Mwisho na kabla ya mwisho mbona swala la Mahakama ya kadhi hupata msukumo mkubwa wakati raisi anapokuwa Mwislamu?
Mwisho kabisa,wana zuoni wa Kiislamu watufafanulie tuelewe sisi ndugu moja,Wakristo wengi wanamsoma Katika Kitabu Kitakatifu Biblia kuwa kadh ni mtu mbya.Palikuwa na kadh katili asiyependa watu....Wakawapeleka kwa kadhi wakachapwa viboko..,kabla ujapelekwa kwa kadhi akakutupa gerezani.nk
Tujadili