Greenwhich
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 1,337
- 968
Taarifa zilizotufikia hivi punde ni kwamba kesi iliyokuwa inamkabili mbunge wa Jimbo la Arusha Godbless Lema imefutiliwa mbali na mahakama leo jijini Arusha baada ya Jamhuri kupeleka maombi ya kufuta kesi hiyo.
Kesi hiyo ilifunguliwa kwa shinikizo la mkuu wa mkoa wa Arusha Magessa Mulongo kwa madai kwamba Lema alichochea vurugu kwenye chuo cha Uhasibu Arusha na pia Lema anadaiwa kumtukana mkuu huyo wa mkoa.
Lema anadaiwa kutamka maneno kwamba..Mkuu wa mkoa anakuja kama anaenda Send-off..Maneno ambayo polisi wanadai yalichochea uvunjifu wa amani.
Mahakama imefutilia mbali kesi hiyo kwa madai kwamba Lema hana kesi ya kujibu.
Kama kawaida umati wa wafuasi wa CHADEMA ulifurika mahakamani na kushangilia kwa nguvu mara baada ya hukumu hiyo.
Kesi hiyo ilifunguliwa kwa shinikizo la mkuu wa mkoa wa Arusha Magessa Mulongo kwa madai kwamba Lema alichochea vurugu kwenye chuo cha Uhasibu Arusha na pia Lema anadaiwa kumtukana mkuu huyo wa mkoa.
Lema anadaiwa kutamka maneno kwamba..Mkuu wa mkoa anakuja kama anaenda Send-off..Maneno ambayo polisi wanadai yalichochea uvunjifu wa amani.
Mahakama imefutilia mbali kesi hiyo kwa madai kwamba Lema hana kesi ya kujibu.
Kama kawaida umati wa wafuasi wa CHADEMA ulifurika mahakamani na kushangilia kwa nguvu mara baada ya hukumu hiyo.