Mahakama nchini Sudan imewahukumu Maafisa Usalama kifo kwa kumtesa na kumuua mwalimu

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Ahmad al-Khair, 36, alikufa wakati ameshikiliwa na maafisa hao baada ya kukamatwa wakati wa maandamano ya kumtoa Rais Omar al-Bashir madarakani.

hii ni moja ya kuhumu za mwanzo kabisa kutolewa mara baada ya machafuko ya kuleta utawala wa demokrasia nchini Sudan.

Hakimu anasema kuwa hukumu hizo za kifo ni sehemu ya kutoa funzo.

Baada ya hukumu Jaji aliwauliza kaka wa l-Khair kama anataka polisi hao wasamehewe , lakini alikataa na kusema anataka wauwawe.

Mwanasheria wa upande wa watetezi anasema kuwa atakata rufaa.

Pia mahakama imegundua kuwa Ahmad Al-Khair alipigwa na kuteswa hadi kufa na maafisa wakati amekamtwa kwenye eneo la utesaji huko jimbo la Kassala.

Chini ya rais aliyeondolewa madarakani Bashir, hukumu ya kifo ilipitishwa na watu wawili kuuwawa.

Kesi ya Ahmad Al-Khair imejizolea umaarufu mkubwa Sudan na kifo chake kilizua hasira kali kwa waandamaji. idadi kubwa ya watu walikusanyika kusikiliza kesi hiyo nje ya mahakama katika mji pacha na mji mkuu wa Khartoum.

Takribani watu 170 waliuwawa wakati wa maandamano dhidi ya Serikali. Bashir aliondolewa madarakani na jeshi baada ya kupata madaraka miaka 30 iliyopita kwa njia ya mapinduzi.

Bashir Mapema mwezi uliopita alihukumiwa miaka miwili kwa kosa la rushwa, mahakama iliamua awekwe kwenye kituo cha kijamii kwani umri wake ni mkubwa sana kukaa jela.
 
Ahmad al-Khair, 36, alikufa wakati ameshikiliwa na polisi baada ya kukamatwa wakati wa maandamano ya kumtoa Rais Omar al-Bashir madarakani.

hii ni moja ya kuhumu za mwanzo kabisa kutolewa mara baada ya machafuko ya kuleta utawala wa demokrasia nchini Sudan.

Hakimu anasema kuwa hukumu hizo za kifo ni sehemu ya kutoa funzo.

Baada ya hukumu Jaji aliwauliza kaka wa l-Khair kama anataka polisi hao wasamehewe , lakini alikataa na kusema anataka wauwawe.

Mwanasheria wa upande wa watetezi anasema kuwa atakata rufaa.

Pia mahakama imegundua kuwa Ahmad Al-Khair alipigwa na kuteswa hadi kufa na maafisa wakati amekamtwa kwenye eneo la utesaji huko jimbo la Kassala.

Chini ya rais aliyeondolewa madarakani Bashir, hukumu ya kifo ilipitishwa na watu wawili kuuwawa.

Kesi ya Ahmad Al-Khair imejizolea umaarufu mkubwa Sudan na kifo chake kilizua hasira kali kwa waandamaji. idadi kubwa ya watu walikusanyika kusikiliza kesi hiyo nje ya mahakama katika mji pacha na mji mkuu wa Khartoum.

Takribani watu 170 waliuwawa wakati wa maandamano dhidi ya Serikali. Bashir aliondolewa madarakani na jeshi baada ya kupata madaraka miaka 30 iliyopita kwa njia ya mapinduzi.

Bashir Mapema mwezi uliopita alihukumiwa miaka miwili kwa kosa la rushwa, mahakama iliamua awekwe kwenye kituo cha kijamii kwani umri wake ni mkubwa sana kukaa jela.
johnthebaptist USSR
 
Back
Top Bottom