GE2025 Mahakama Kuu yapigilia msumari uamuzi kufichwa kwa mashahidi wa Jamhuri katika kesi ya Tundu Lissu

GE2025 Mahakama Kuu yapigilia msumari uamuzi kufichwa kwa mashahidi wa Jamhuri katika kesi ya Tundu Lissu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo Jumanne Agosti 12, 2025 inatarajiwa kutoa uamuzi kuhusu mapingamizi ya upande wa utetezi katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, yanayolenga kupinga matumizi ya mashahidi wa siri.

Katika mapingamizi hayo, upande wa utetezi unapinga mashahidi kutoa ushahidi bila mshitakiwa kuwaona moja kwa moja, na badala yake kusikia sauti pekee. Utetezi umedai kuwa utaratibu huo unakiuka haki za mshitakiwa kupata utetezi wa haki.

Kesi hiyo itasikilizwa mbele ya Jaji Elizabeth Mkwizu.





=========================
Mahakama Kuu yapigilia msumari uamuzi kufichwa kwa mashahidi wa Jamhuri katika kesi ya Lissu

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo, Jumanne, Agosti 12, 2025, imetupilia mbali mapingamizi ya upande wa utetezi wa Tundu Lissu katika kesi ya marejeo (judicial review) iliyolenga kupinga matumizi ya mashahidi wa siri.

Katika mapingamizi hayo, upande wa utetezi ulipinga uhalali wa mashahidi wa siri katika kesi ya kuchapisha taarifa inayomkabili Tundu Lissu katika Mahakama ya Kisutu, ambapo Jamhuri iliwasilisha ombi la kuficha baadhi ya mashahidi.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji Elizabeth Mkwizu, huku upande wa Lissu, kupitia Wakili Dkt. Rugemeleza Nshala, ukieleza kutoridhishwa na uamuzi huo.



 
uonapo hapo limeshindikana na likaenda ya rufani wakapindua ndo ushindi wa lisu hanyongwi endapo gvt ina mpango wa kunyonga

hawakawii kumhukumu mbeleni huko unatoka msamaha lisu anapewa condition kutojihusisha na siasa washenzi sana hawa
 
Back
Top Bottom