Magufuli duniani Leo

Magufuli duniani Leo

britanicca

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
17,187
Reaction score
41,678
Mwanzoni Rais wetu alipendwa sana na mpaka baadhi ya nchi zikatamani kumuazima akatawale kule kwa siku kadhaa au miezi kadhaa, hii ilileta picha kwamba ama Magufuli alikuwa anafanya vema mwanzoni au aliazna na vipaumbele ambavyo ni matataizo sugu ya nchi nyingi duniani mfano rushwa na uwajibikaji,

Tuwe wakweli Mpaka wapinzani wa hapo Tanzania akina mbowe na Lipumba walisema kwamba Magufuli anatekeleza ilani yao hafanyi ya kwake,

Zitto kabwe akafika hatua akasema sasa nchi ina rais kwa kweli,

Pale Kenya na nchi baadhi zilizoedesha uchaguzi baada ya Magufuli kuingia madarakani walitamani hata wale wanaenda kuwachagua wawe katika viatu vya Magufuli,

Pro Lumumba mpaka akaanzisha neno maarufu la Magufulification of Africa
Pale Autralia na Madagascar ilikuwa maandamano yakitaja kwamba tunataka kuwa na kiongozi kama Magufuli,

Ulaya walisema kuna kanchi kameibuka huko afrika kana Rais anaitwa Magufuli,

Magufuli Magufuli Magufuli aal over the world then

Je kuna jinsi alitafsiriwa vibaya mwanzoni baadae wakagundua kwamba siyo, au labda ameyafanya mazuri wakayazoea ikaonekana jambo la kawaida?
Au bado anakubalika kwa wale mnaotembea tembea huko?

BADO DUNIA INAMUONA MAGUFULI KAMA MWANZO? KAMA SIYO UNAHISI NINI KIMESHUSHA UMAARUFU HUO? NA JE ANGEFANYA NINI ILI ANEDLEEE KUAMINIKA KWA KILA MTU?

Kwakweli alianza vizuri sana ukitilia maanani kwamba uadilifu ndio karata iliyomuibua kutoka kusikojulikana
Ila nadhani kuna watu wanamshauri vibaya kwamba anaweza tatua matatizo ya wananchi kutumia shortcuts za maneno ya kisiasa badala ya kuyatatua matatizo kama yalivyo
Kuna uwezekano vile vile hali ya kutoaminiana (wenye mikia na waliokatwa)na makundi ktk chama kumemfanya sasa ajenge usuhuba na watu ASIOFANANA NAO

Mengi yanakuja
 
Anza kwa kujichunguza mwenyewe kama kweli bado unamsifia kama ilivyokuwa mwanzo au umeanza kuziona dosari? Kama kuna dosari unaziona ziweke wazi hapa tuzijadili.

Binafsi huwa sina imani na mwanasiasa kwa sababu huwa wanapenda sifa tu; utendaji kwa ajili ya wengine ni asilimia kidogo.
 
Anza kwa kujichunguza mwenyewe kama kweli bado unamsifia kama ilivyokuwa mwanzo au umeanza kuziona dosari? Kama kuna dosari unaziona ziweke wazi hapa tuzijadili.
Binafsi huwa sina imani na mwanasiasa kwa sababu huwa wanapenda sifa tu; utendaji kwa ajili ya wengine ni asilimia kidogo.
Sifa nyingi huwa zinajinconcentrate mwanzoni mwa utawala na siku uchaguzi unapokaribia.
 
Magufuli amefifia machoni kwa wazungu baada ya kuwakamata wezi wa dhahabu na makinikia pale bandarini. ndio walipoanza kumchukia na kutumika kwa vibaraka wa ndani (Mbowe, Zito, Tundu Lissu n.k.) kumchafua zaidi ili mataifa yamuone hafai.
 
Na mkuu mtoa hoja kipimo kizuri kitaonekana live atakapokuwa anaingia uwanjani,lazima MC atatamka jina lake halafu tutasikia nini wazawa wata react towards him,president Mugabe pamoja na yote alikuwa anafunika kwa mashangilio kila alipokuwa akitambulishwa na hopefull enca Afrika wataionyesha live hii ghafla ili nasi tulioko huku Lingusenguse tuyaone yanayojiri pale kwenye uwanja wa Loftus Versfeld ndani ya Jacaranda city.
 
Kuna watu walidhani ni nguvu ya soda, hii ngoma iko vile vile hadi 2025, Magufuli ni yule yule juzi, jana, leo na hata...

Mimi nimeshauri hivi
P
 
Zitto Kabwe nje baada ya Magufuli kutoa hotuba maarufu bungeni nadhani ulimsikiliza baadaye
Ni kweli mkuu mpaka wapinzani walimshambulia sana Zito kwa kuongea yale maneno
Hata namba moja alipoenda Kigoma Zito alitoa Sifa kede kede,
Kila siku nasema ww na yule mbatizaji umemuacha mbali sana
 
Kuna watu walidhani ni nguvu ya soda, hii ngoma iko vile vile hadi 2025, Magufuli ni yule yule juzi, jana, leo na hata...

Mimi nimeshauri hivi
P
KABISA NASIMAMA NAWEWE
 
Kwakweli alianza vizuri sana ukitilia maanani kwamba uadilifu ndio karata iliyomuibua kutoka kusikojulikana
Ila nadhani kuna watu wanamshauri vibaya kwamba anaweza tatua matatizo ya wananchi kutumia shortcuts za maneno ya kisiasa badala ya kuyatatua matatizo kama yalivyo
Kuna uwezekano vile vile hali ya kutoaminiana (wenye mikia na waliokatwa)na makundi ktk chama kumemfanya sasa ajenge usuhuba na watu ASIOFANANA NAO

Mengi yanakuja
 
Back
Top Bottom