Mkuu attachment yako in road width tu hamna roadreserve!
Mh ulivyojenga hoja yako inatia mshaka sana. Unataka tuamini kuwa Maghufuli ana kinyongo na wakazi kuanzai ubungo hadi kibaha kitu ambacho siwezi kuamini kirahisi angalia kauli hii:[ Na ili kuhakikisha wananchi kati ya Ubungo hadi Kibaha wanakosa haki yao kabisa kwa ubabe wake wa kawaidia aliingia katika ardhi na makazi halalai ya wananchi chini ya sheria zilizotungwa na bunge bila ya kushirikisha ngazi za Mkoa, Wilaya, Manispaa, Tarafa, Kata wala Serikali za Mitaa na mpaka sasa hataki majadiliano ya iana yoyote yanayohusu haki za wananchi hawa. Je huu ndio mfano wa kiongozi bora mnayemtaka? Viongozi kama hawa Mwalimu Nyerere alisema hawafai hata kupewa Ujumbe wa ]
Hivi wakati maghufuli anaagiza kupanda mawe na mabango yanayoonyesha road reserve ni 120m Je hakuna sheria iliyomwongoja na kwamba alikuwa anabuni tu mwenyewe? Je unaujua mpango mzima wa fly overs utakavyokuwa na kuwa MT10 tu zinatosha.
Hata hivyo, siwezi ku argue kwenye sheria kwani zinahitaji utafiti wa kutosha.
Mi namsupport Magufuli 100% asipoendesha zoezi la bomoabomoa, maeneo yote Dar yatageuka kuwa kebara slams!! huku kwetu sinza watu wamejenga kwenye open space na kuta zao wamevuka mipaka na kushrink barabara zote za mitaa. its really difficult, imagine mtu anajenga gorofa kwenye open space njia za kupita hakuna. Magufuli akaze buti. The problem I see with JK ni mwoga na I think he's scared that Magufuli will overshadow him, atafunikwa!!
Kubomoa sio shida sana ila fidia ni muhimu pia, haiwezekani watu wanajenga mpaka makazi yanakamilika halafu miaka mingi tuu wanalipa kodi zote including kodi ya majengo gafla unasema makazi si halali then bomoa bila malipo. Ninachofahamu huyu jamaa sasa hivi yupo kwenye ntoke vipi ili azidi kujiandaa na kuchaguliwa 2015Mi namsupport Magufuli 100% asipoendesha zoezi la bomoabomoa, maeneo yote Dar yatageuka kuwa kebara slams!! huku kwetu sinza watu wamejenga kwenye open space na kuta zao wamevuka mipaka na kushrink barabara zote za mitaa. its really difficult, imagine mtu anajenga gorofa kwenye open space njia za kupita hakuna. Magufuli akaze buti. The problem I see with JK ni mwoga na I think he's scared that Magufuli will overshadow him, atafunikwa!!
Huwezi kutatua matatizo hayo kwa kutumia sheria feki kama anavyofanya Magufuli
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?
Mambo yake Maghufuli anayafanya hadharani vilevile. Kila anakoenda na Tv mgongoni!Hivi kwa nini kwa wakati mmoja Raisi na PM wanamwandama Magufuli katika utendaji wake tena hadharaniiiii????????????????????????????
Hivi mnamjua Magufuli Jimboni kwake?
Nyie magufuli mnanjadili katika dhana ya utendaji wake kitaifa lakini katika ngazi ya jimbo mtu huyu ni mchafu kupitia kiasi .
Mfano :Mafgufuli aliteka viwanja chato,akajenga majumba mtaa mzima,kanisa,hotel nk kisha akashinikiza Serikali ili Jimbo la chato kujitenga kutoka Biharamulo ili iwe wilaya na Halmshaurui inayojitegemea ,Akafanikiwa.Sasa watumishi wa Halmshauri ya Chato wakapanga kwake.
Hivyo hadi sasa idara zote za halmshauri ya chato zinapanga kwake pamoja na kuishi hata Waziri mkuu alipofika chato alilama Kwenye nyumba zilizo na hasdhi kama ikulu(mali ya magufuli).
Kwa ufupi Serikali nzima katika hslmshuri ya chato inapanga kwa Magufuli.
Inawezekana alitafuta kwa uwezo wake lakini si msafi kama wengi wanavyodhani .
Kwa siku za usoni nitaanzisha thread mpya kuhusu huyu Bwana.
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?
Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?
Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?
Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?
Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?
Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:
a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.
b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.
Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:
a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.
b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.
my two cents plus the other fifty
Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:
a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.
b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.
my two cents plus the other fifty