Magufuli avuruga mchoro wa Lowassa na CHADEMA!

Magufuli avuruga mchoro wa Lowassa na CHADEMA!

Jamani ccm mna mambo ! Huo mchoro Lowasa aliuweka meza au kabati ipi mpaka magufuli aufikie na ku uvuruga?mbona hampendagi kauli za kujenga nikuwasha moto tu kila siku ili kumchafua tu Lowasa ? Sasa huko kujipendekeza kutoa hongera na wengine nao wakuvalie Bango ? Manake tunaelewa kilichopo kati ya hawa !. Mtakua mbele kwa mabaya hadi lini? Kwanini atoe pongezi kwa ajili ya kuzima moto wa Lowasa,asitoe tu pongezi ya kawaida ? Wewe ni nani wake mpaka akueleze kua anazima moto wa Lowasa ? Hakika mbea hana likizo,likizo yake ni kaburi ! Huoni hata woga kuzua jambo baya kama hili ? Akisema mpinzani chochote ni uchochezi,lazima apimwe mkojo akiwa rumande !.lakini nyie mnaweza kuvuruga nchi mtakavyo nakuchonganisha mwanzo wa nchi hadi linakotua jua ,na majirani wa nchi ruksa.sasa mmesha chokoza uislamu tusubirini kifuatacho baada ya tafakari yao.sisiemu,mtakufa lini tupumue sisi wanyonge ?
Mungu tuviringishie hili jiwe la kusagia lili tuvaa shingoni,ukalitose baharini, utukomboe,nakuamini mfalme,Amen.

Sent using Jamii Forums mobile app
CCM ni mzaliwa wangu wa kwanza asema BWANA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawezi kumshinda Jakaya, jamaa alimtumia Lowassa na kamkata ugombea uraisi 2015.
Hyo haikua Mara ya kwanza Lowassa kukatwa hvyo cdhan kma kuna fitna kwa JK bt ypo mambo meng CCM wanayajua khs mheshimiwa ndo mana hawampi kiti cha urais. JK was very fair kumpa uwaziri mkuu cheo ambacho hakuna aliyewah kumpa na kma Nyerere angalikua hai cdhan kma angekipata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani hii habari niya umbeya! Umejuaje nia ya Magu na hata ya EL? Una ushahidi gani zaidi ya kufanya umbeya? Achana nazo! Ningeshangaa sana kama Magu asingekuwa wa kwanza kumpongeza Uhuru
Jamaa "junya" la kisiasa wala lisikusumbue!
Katika kampeni za kugombea urais nchini Kenya.LOWASSA na CHADEMA
walitaka kutumia tetesi zilizokuwepo kuwa Magufuli anamuunga mkono Raila Odinga.

Hivyo nao katika kulipiza uchungu wa kushindwa uchaguzi wakasema WATAAMUUNGA mkono Uhuru Kenyatta ili Magufuli asikie naye uchungu.

Lakini cha kushangaza ni kuwa Rais Magufuli AMETUMA haraka salamu za PONGEZI kwa rais Kenyatta kwa KUCHAGULIWA tena kwa MUHULA wa pili wa utawala wake. Mara tu zilipotangazwa.

Na hivyo KUSAMBARATISHA KABISA mbinu za KUNGONISHA kati ya Serikali ya Tanzania na Kenya. Huku akiwaacha Chadema na Lowassa WAKISHANGAA wasijue nini cha kufanya.

Ikikumbukwa Lowassa alitoa waziwazi kauli yake na chama chake kuwa kinamuunga mkono Kenyatta(.....) NIA kubwa ilikuwa ni kwamba Rais Magufuli aonekane kuwa HAMPENDI Uhuru Kenyatta. Na pia aonekane kama ni Kiongozi asiyejua mambo ya
Utawala,
Protokali na
Diplomasia.

Lakini kwa HEKIMA na USHAURI aliopata akaamua kumpongeza Uhuru kenyatta HARAKA sana na kuwaacha CHADEMA na Lowassa wakishangaa tu wasijue nini cha kufanya.

Maana walikuwa wakifikiri Rais Magufuli ANGEJIKOKOTA kwa muda mrefu KUMPONGEZA Kenyatta katika ushindi wake.

Rais Magufuli aliangalia picha kubwa kati ya URAFIKI na MASLAHI ya NCHI. Na akachagua MASLAHI ya nchi/National Interests badala ya URAFIKI.
kwa Hilo tunampongeza sana.

ITABIDI basi Lowassa and Co. KURUDI kwenye drawing table/ Meza ya KUCHOREA maana MCHORO wao Magufuli AMEUVURUGA na sasa ni HISTORIA.
Hongera Magufuli kwa Hehima hiyo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ha! Ha! Ha! Leo mnamruka mkenya pekee aliyefika Chato kumpongeza Magufuli !
Alifika Chato kama best friend...angeshinda Magufuli angempongeza kama best friend na kama Rais wa Kenya.
 
Kumbe mtu kutoa pongezi hadi ushauriwe naomba kuwajua waliomshauri kutoa pongezi
 
Kumbe mtu kutoa pongezi hadi ushauriwe naomba kuwajua waliomshauri kutoa pongezi
Wewe unafikiri kazi ya kuongoza TAIFA ama kujibu taifa ama kwenda vitani, ama kutoa MAAMUZI yeyote yanayohusu taifa hutolewa bila KUSHAURIANA? Asiyejua maana haambiwi maana.
Ndo kunakuwaga hivyo duniani kote ukishika kiti kama chake. Ndo maana kuna watu wanaoitwa washauri wa masuala mbali mbali.
 
Wewe unafikiri kazi ya kuongoza TAIFA ama kujibu taifa ama kwenda vitani, ama kutoa MAAMUZI yeyote yanayohusu taifa hutolewa bila KUSHAURIANA? Asiyejua maana haambiwi maana.
Ndo kunakuwaga hivyo duniani kote ukishika kiti kama chake. Ndo maana kuna watu wanaoitwa washauri wa masuala mbali mbali.
Kwa iyo pongezi ni za taifa au pongezi ni zake binafs
 
Kiukweli chadema walipaswa waangalia moja tu, uchaguzi utaendeshwaje na wampongeze aliyeshinda kihalali.

Cha ajabu wamefuta reference au chachu ambayo walipaswa kuitumia iwapo upinzani wangeshinda kenya.
 
Back
Top Bottom