Mode,
Hii mada ni ya kisheria naomba sana imekuja huku ambako ni maalumu kwa ajili ya sheria na mahakama, maana huku ndiko tatizo linalokoeleweka
////////////////////////////////////////////////////
Kumbe ucheleweshaji wa kesi kwa mahakama ya kazi kunamkera Rais. Katika hotuba yake leo ameahidi kwamba analijua tatizo hili na ndiyo maana ameteua majaji wapya kumi.
Hakika mahakama hii imeemelemewa maana ni mahakama yenye majaji wawili tu nchi nzima yaani Lilian Mashaka na Aisha Nyerere.
Si kwamba majaji hawa wawili hawana uwezo. Hapana. Wana uwezo mpana na haitashangaza mmoja wao au wote wawili siku moja ukasikiwa wamepandishwa kuwa majaji Mahakama ya Rufaa.
Kinachosumbua ni kwamba kesi za ajira zimekuwa nyingi na kuna wanaosema kwamba Mahakama ya Kazi ndiyo ya pili kwa wingi wa kesi nyingi ikifuatiwa na ile ya Ardhi.
Katika hali hii, mtu anayejijua hana haki ataipenda kwa sababu mkosa haki mbinu yake ya kwanza mahakamani huwa ni kuhakikisha anachelewesha kesi ndipo zije mbinu zingine.
Hivyo, kama kuna uonevu wowote kazini, unashindwa kuushughulikia kwani hata ukienda Mahakamani, utshinda kesi lakini ukweli ni kwamba utatumia si chini ya miaka mitatu. Kwa kifupi ni kwamba Mahakama ya Kazi ilikuwa imeshaanza kutokuwa tegemeo.
Siyo kwamba wanahongwa. Bali kesi zinachelewa kiasi cha kukatisha tamaa.
Tunalieleza hili kwa sababu kila mmoja huku mitandaoni ni mfanyakazi, hivyo kila mmoja wetu ni mtuhumu au mtuhumiwa mtarajiwa wa hii Mahakama ya Kazi.
Hata ukichapa kazi vipi, usidhani uko salama. Bado yanaweza kutokea mazingira wenzako wakakuonea wivu na majungu wakakusababisha ukaacha au kufukuzwa kazi kwa uonevu (harrasment).
Sasa katika hali hii, mkombozi au tumaini pekee ilikuwa ni Mahakama ya Kazi (High Court Labor Division). Lakini kama hali ndiyo ile iliyopo la ucheleweshaji wa kesi basi serikali lazima ijue kwamba morali na uzalendo utakosekana.
Hebu tafakari, serikali inapenda kila mmoja awe mzalendo sehemu yake ya kazi. Sasa jiulize, hivi ukiwa mzalendo sana kwenye sehemu yako ya kazi utaishia wapi? Je, utapendwa na mabosi wako? Je, utachukiwa na mabosi wako?
Kw amfano, wafanyakazi waliokuwa kwenye madini wakiona makinikia yakisafirishwa, unadhani hawakuwa wazalendo wakaangali tu yanaibiwa?
Tulihoji wafanyakazi wale wanakuambia makinikia yameibiwa huku wakiona tena wanasema yalikuwa yanalindwa na bunduki ya SMG.
Sasa tukawahoji wafanyakazi wale kwamba kwa nini hakumuwaambia mabosi wakmba wanaharibu uchumi, wakajibu, unataka nifukuzwe kazi, utanilisha wewe?
Wafanyakazi wale wanasema kweli. Hali ni hivyohivyo popote unapofanyia kazi. Mwajiri kama anakwepa kodi na unaona, je, utamwambia kwamba nilipe mshahara wangu vizuri lakini usikwepe kodi. Je, unaweza kufanya hivyo?
Huwezi. Kwa nini? Kwa sababu utafukuzwa kazi. Halafu ukishafukuzwa kazi, serikali haitambui kwamba uligombana na mabosi wako kwa sababu ya uzalendo na kuupigania uchumi wa taifa ili.
Basi, ahueni ingekuwa inakuja kama Mahakama ya Kazi itafanya kesi yako iishe haraka. BAdala yake Mahakama ya Kazi utachelewa kupata haki yako, ingawa utaipata.
Ndugu zangu, je katika hali kama hii, utarudia mchezo wa kuwa mzalendo? Hapana. Utaishia kufanya wanachofanya wenzako. Wenzako watafanya utumbo, tena utumbo unaoiumiza nchi, na wewe itabidi uige tu kuvumilia au na wewe ufanye utumbo ili ulinde ajira yako.
Mtu anaweza kuweka pingamizi (PO) ambalo anajua halina nguvu lakini anajua pingamizi litachukua si chini ya miezi minane. Baada ya PO ndipo inakuja kesi ya msingi inayochukua si chini ya miezi mingine minane hata kama atashindwa.
Huyu tayari ameshafurahi kesi kuchelewesha kwa miezi 16. Athari za kucheleweshwa kesi ni mbaya zaidi kwa mwenye haki na ni furaha kwa anayejijua hana haki.
Hapo ndipo tulipofikia. Inawezekana serikali na Mahakama ya Kazi hili hawajaliona. Sasa leo Rais Magufuli kaliongelea hili kwamba anatambua kuna tatizo la kuchelewesha kesi za ajira.
Mitandao ilipaswa kulijadili hili kwa sababu kila mmoja ataguswa. Tena kipindi hiki vyuma vimekaza kila mmoja ni mhanga unaweza kuathirika na Mahakamani haki ukachelewa kuipata kiasi kwamba unapoipata haina faida tena.
Kama Rais anaona kwamba ameteua majaji kumi, hatudhani kama watapelekwa Mahakama ya Kazi. Tunaamini msongamano uko hata mikoani na makahakama zingine. Rais ikibidi ateue majaji wengine kumi.
Pale Mahakama ya Kazi panahitajika majaji kama saba hivi. Sasa wanapobaki majaji wawili tu, matokeo yake ndiyo haya.
Pamoja na kuw ana hao majaji wawili tu, bado hutokea tatizo jingine analoliweza Mungu tu.
Yupo pale Jaji mmoja mara kadhaa kesi zake zinaahirishwa kwa sababu ya kuumwa au kuhudhuria matibabu hospitalini. N jaji mchapakazi kwelikweli, muadilifu kwelikweli lakini ni kweli pia amekuwa akisumbuliwa na maradhi.
Hata ukimuona unaona dalili za kusumbuliwa maradhi na sanasana unamhurumia tu. Ukimkosa kwa sababu kaenda hospitali, kesi zke zote za siku hiyi zinaahirishwa wakati mwingine kwa miezi miwili. Jaji mgonjwa!
Hatuwezi kuendelea namna hii. Tunasisitiza, pale Labour Court pawe na majaji kama sita hivi siyo wawili tu. Majaji wawili hawawezi kusimamia kesi za ajira za nchi nzima.
Tunashukuru Rais Magufuli kuliona hilo ni tatizo na akalitaja mbele ya Sikukuu ya Wafanyakazi. Tunasubiri Jaji Mkuu alione hilo ni tatizo, tunasubiri Mahamakaa ya Kazi nayo ilione hili ni tatizo.
Na watanzania mitandaoni, tulione hili kuwa ni tatizo na kulipigia kelele. Tumesema, hata ukiishi kitakatifu vipi, bado kila mmoja wetu ni mtuhumu au mtuhumiwa mtarajiwa hivyo tushinikize haki ipatikane mapema tuwe na imani zaidi na Mahakama ya Kazi (Labour Court)
////////////////////////////////////////////////////
Cc
Petro E. Mselewa, Mtendaji wa kaya, Skillionare, Rola, Mushobozi, Skilionare, Dangote the advocate, Bikra, Mtambuzi, Gaijin, Mwita Maranya, suluta, othuman dan fodio, Amos Enock, stroke.
Hii mada ni ya kisheria naomba sana imekuja huku ambako ni maalumu kwa ajili ya sheria na mahakama, maana huku ndiko tatizo linalokoeleweka
////////////////////////////////////////////////////
Kumbe ucheleweshaji wa kesi kwa mahakama ya kazi kunamkera Rais. Katika hotuba yake leo ameahidi kwamba analijua tatizo hili na ndiyo maana ameteua majaji wapya kumi.
Hakika mahakama hii imeemelemewa maana ni mahakama yenye majaji wawili tu nchi nzima yaani Lilian Mashaka na Aisha Nyerere.
Si kwamba majaji hawa wawili hawana uwezo. Hapana. Wana uwezo mpana na haitashangaza mmoja wao au wote wawili siku moja ukasikiwa wamepandishwa kuwa majaji Mahakama ya Rufaa.
Kinachosumbua ni kwamba kesi za ajira zimekuwa nyingi na kuna wanaosema kwamba Mahakama ya Kazi ndiyo ya pili kwa wingi wa kesi nyingi ikifuatiwa na ile ya Ardhi.
Katika hali hii, mtu anayejijua hana haki ataipenda kwa sababu mkosa haki mbinu yake ya kwanza mahakamani huwa ni kuhakikisha anachelewesha kesi ndipo zije mbinu zingine.
Hivyo, kama kuna uonevu wowote kazini, unashindwa kuushughulikia kwani hata ukienda Mahakamani, utshinda kesi lakini ukweli ni kwamba utatumia si chini ya miaka mitatu. Kwa kifupi ni kwamba Mahakama ya Kazi ilikuwa imeshaanza kutokuwa tegemeo.
Siyo kwamba wanahongwa. Bali kesi zinachelewa kiasi cha kukatisha tamaa.
Tunalieleza hili kwa sababu kila mmoja huku mitandaoni ni mfanyakazi, hivyo kila mmoja wetu ni mtuhumu au mtuhumiwa mtarajiwa wa hii Mahakama ya Kazi.
Hata ukichapa kazi vipi, usidhani uko salama. Bado yanaweza kutokea mazingira wenzako wakakuonea wivu na majungu wakakusababisha ukaacha au kufukuzwa kazi kwa uonevu (harrasment).
Sasa katika hali hii, mkombozi au tumaini pekee ilikuwa ni Mahakama ya Kazi (High Court Labor Division). Lakini kama hali ndiyo ile iliyopo la ucheleweshaji wa kesi basi serikali lazima ijue kwamba morali na uzalendo utakosekana.
Hebu tafakari, serikali inapenda kila mmoja awe mzalendo sehemu yake ya kazi. Sasa jiulize, hivi ukiwa mzalendo sana kwenye sehemu yako ya kazi utaishia wapi? Je, utapendwa na mabosi wako? Je, utachukiwa na mabosi wako?
Kw amfano, wafanyakazi waliokuwa kwenye madini wakiona makinikia yakisafirishwa, unadhani hawakuwa wazalendo wakaangali tu yanaibiwa?
Tulihoji wafanyakazi wale wanakuambia makinikia yameibiwa huku wakiona tena wanasema yalikuwa yanalindwa na bunduki ya SMG.
Sasa tukawahoji wafanyakazi wale kwamba kwa nini hakumuwaambia mabosi wakmba wanaharibu uchumi, wakajibu, unataka nifukuzwe kazi, utanilisha wewe?
Wafanyakazi wale wanasema kweli. Hali ni hivyohivyo popote unapofanyia kazi. Mwajiri kama anakwepa kodi na unaona, je, utamwambia kwamba nilipe mshahara wangu vizuri lakini usikwepe kodi. Je, unaweza kufanya hivyo?
Huwezi. Kwa nini? Kwa sababu utafukuzwa kazi. Halafu ukishafukuzwa kazi, serikali haitambui kwamba uligombana na mabosi wako kwa sababu ya uzalendo na kuupigania uchumi wa taifa ili.
Basi, ahueni ingekuwa inakuja kama Mahakama ya Kazi itafanya kesi yako iishe haraka. BAdala yake Mahakama ya Kazi utachelewa kupata haki yako, ingawa utaipata.
Ndugu zangu, je katika hali kama hii, utarudia mchezo wa kuwa mzalendo? Hapana. Utaishia kufanya wanachofanya wenzako. Wenzako watafanya utumbo, tena utumbo unaoiumiza nchi, na wewe itabidi uige tu kuvumilia au na wewe ufanye utumbo ili ulinde ajira yako.
Mtu anaweza kuweka pingamizi (PO) ambalo anajua halina nguvu lakini anajua pingamizi litachukua si chini ya miezi minane. Baada ya PO ndipo inakuja kesi ya msingi inayochukua si chini ya miezi mingine minane hata kama atashindwa.
Huyu tayari ameshafurahi kesi kuchelewesha kwa miezi 16. Athari za kucheleweshwa kesi ni mbaya zaidi kwa mwenye haki na ni furaha kwa anayejijua hana haki.
Hapo ndipo tulipofikia. Inawezekana serikali na Mahakama ya Kazi hili hawajaliona. Sasa leo Rais Magufuli kaliongelea hili kwamba anatambua kuna tatizo la kuchelewesha kesi za ajira.
Mitandao ilipaswa kulijadili hili kwa sababu kila mmoja ataguswa. Tena kipindi hiki vyuma vimekaza kila mmoja ni mhanga unaweza kuathirika na Mahakamani haki ukachelewa kuipata kiasi kwamba unapoipata haina faida tena.
Kama Rais anaona kwamba ameteua majaji kumi, hatudhani kama watapelekwa Mahakama ya Kazi. Tunaamini msongamano uko hata mikoani na makahakama zingine. Rais ikibidi ateue majaji wengine kumi.
Pale Mahakama ya Kazi panahitajika majaji kama saba hivi. Sasa wanapobaki majaji wawili tu, matokeo yake ndiyo haya.
Pamoja na kuw ana hao majaji wawili tu, bado hutokea tatizo jingine analoliweza Mungu tu.
Yupo pale Jaji mmoja mara kadhaa kesi zake zinaahirishwa kwa sababu ya kuumwa au kuhudhuria matibabu hospitalini. N jaji mchapakazi kwelikweli, muadilifu kwelikweli lakini ni kweli pia amekuwa akisumbuliwa na maradhi.
Hata ukimuona unaona dalili za kusumbuliwa maradhi na sanasana unamhurumia tu. Ukimkosa kwa sababu kaenda hospitali, kesi zke zote za siku hiyi zinaahirishwa wakati mwingine kwa miezi miwili. Jaji mgonjwa!
Hatuwezi kuendelea namna hii. Tunasisitiza, pale Labour Court pawe na majaji kama sita hivi siyo wawili tu. Majaji wawili hawawezi kusimamia kesi za ajira za nchi nzima.
Tunashukuru Rais Magufuli kuliona hilo ni tatizo na akalitaja mbele ya Sikukuu ya Wafanyakazi. Tunasubiri Jaji Mkuu alione hilo ni tatizo, tunasubiri Mahamakaa ya Kazi nayo ilione hili ni tatizo.
Na watanzania mitandaoni, tulione hili kuwa ni tatizo na kulipigia kelele. Tumesema, hata ukiishi kitakatifu vipi, bado kila mmoja wetu ni mtuhumu au mtuhumiwa mtarajiwa hivyo tushinikize haki ipatikane mapema tuwe na imani zaidi na Mahakama ya Kazi (Labour Court)
////////////////////////////////////////////////////
Cc
Petro E. Mselewa, Mtendaji wa kaya, Skillionare, Rola, Mushobozi, Skilionare, Dangote the advocate, Bikra, Mtambuzi, Gaijin, Mwita Maranya, suluta, othuman dan fodio, Amos Enock, stroke.