Magufuli anapogeuka mtetezi wa mafisadi

Magufuli anapogeuka mtetezi wa mafisadi

1466840016161.jpg
 
Ndani ya zile week 8 za mwanzo tulidhani huyu kweli atakuwa mwiba hata kwa mafisadi wastaafu heee miezi 8 baadae amesema atafukia madhambi yao yote na atayabeba yeye....wao wapumzike kwa amani! Nadhani sasa zile mbwembwe zimeisha rasmi! Hawezi tena kushangaa.....maana alikuwa anashangaa kila kitu na kila amri za waliomtangulia!! Ndio mwisho wake sasa nae business as usual na auto pilot! Kwisha
 
Mnyika, lissu na lema waanze kuwapeleka maana wao ndiyo walituambia kuwa lowasa ni fisadi na wanaushahidi 8years walituaminisha hvyo, sumaye alikubali kuhusu uuzwajwi wa nyumba za serikali na alikiri,
Yule aliyeanzisha mahakama na awapeleke. Tumsikie anayewaita mafisadi leo kisha tumwombe awapeleke mahakamani.
 
Ndani ya zile week 8 za mwanzo tulidhani huyu kweli atakuwa mwiba hata kwa mafisadi wastaafu heee miezi 8 baadae amesema atafukia madhambi yao yote na atayabeba yeye....wao wapumzike kwa amani! Nadhani sasa zile mbwembwe zimeisha rasmi! Hawezi tena kushangaa.....maana alikuwa anashangaa kila kitu na kila amri za waliomtangulia!! Ndio mwisho wake sasa nae business as usual na auto pilot! Kwisha
Mshangao umeisha. Ameelewa sasa. Kuanzia sasa atafanya kama walivyokuwa wakifanya wao. Somo limeeleweka. Hakuna kushangaa tena.
 
Chadema ni bora mngejikita kuhoji ni kwa nini Mbowe aliuza chama chenu???

Naamini bila mbowe kuuza chama msingekengeuka kiasi hiki.

Leo mnapinga kila kitu na kujidai mnadai democrasia wakati ndani ya chadema hamna hata tone la democrasia.
 
Mbona hata wewe Magufuli anakulinda kuhakikisha unaishi kwa amani na utulivu kwani umefanya makosa.


Inamaana tukiskia mfanyabiashara wa M-Pesa kauawa Mwanza au Watu wanaibiwa benki na kuuawa amani ya mahufuli imekwama?
 
Maajabu hayamuishi rais wetu Magufuli. Niliipoona mswada wa mahakama ya mafisadi unapelekwa bungeni nikajua kinachofuata ni kubadili kipengere cha katiba kuwaondolea kinga marais wastaafu ili mahakama ya mafisadi iwamulike Rais mstaafu mzee Mkapa na Mzee Kikwete.

Na hata nikaamini kwa kile kiapo cha wabunge wa CCM kupambana na mafisadi, wataweka hoja hiyo ya kubadili kipengere cha katiba ili ukweli ujulikane dhidi ya Mkapa na Kikwete. Ajabu Rais Magufuli anawakingia Kifua tena kwenye majukwaa kwamba atawalinda wasihofu. Kauli ya kusema atawalinda ni kuhalasha makosa yao.Unawezaje kumlinda mtu asiye na makosa?

Magufuli ndugu yangu dunia inakutazama jinsi unavyojichanga kwenye hii vita ya Mafisadi. Wewe mwenyewe umekuwa ukikili mizigo mizito ulioachiwa na Kikwete

Si ajabu wewe ni mmoja wa mwanachama aliyenusurika katika ile club ya usiku waliouliwa watu hamsini USA
 
Mbona hata wewe Magufuli anakulinda kuhakikisha unaishi kwa amani na utulivu kwani umefanya makosa.
Kwani huyo Magufuli amegeuka kuwa Mungu? Acha kupotosha wewe Magufuli hana ulinzi wowote kwa mwanadamu. Ni Mungu tu mwenye uwezo huo. Usiwe kipofu wa akili wewe
 
Magufuli anajichanganya sana. Anasema nchi ilikuwa shamba la bibi na kwamba huko serikalini kulikuwa na madudu ya ajabu halafu hapohapo anasema atawalinda na kuwatetea hao viongozi walioifanya nchi shamba la bibi! Ajabu sana!
 
Maajabu hayamuishi rais wetu Magufuli. Niliipoona mswada wa mahakama ya mafisadi unapelekwa bungeni nikajua kinachofuata ni kubadili kipengere cha katiba kuwaondolea kinga marais wastaafu ili mahakama ya mafisadi iwamulike Rais mstaafu mzee Mkapa na Mzee Kikwete.

Na hata nikaamini kwa kile kiapo cha wabunge wa CCM kupambana na mafisadi, wataweka hoja hiyo ya kubadili kipengere cha katiba ili ukweli ujulikane dhidi ya Mkapa na Kikwete. Ajabu Rais Magufuli anawakingia Kifua tena kwenye majukwaa kwamba atawalinda wasihofu. Kauli ya kusema atawalinda ni kuhalasha makosa yao.Unawezaje kumlinda mtu asiye na makosa?

Magufuli ndugu yangu dunia inakutazama jinsi unavyojichanga kwenye hii vita ya Mafisadi. Wewe mwenyewe umekuwa ukikili mizigo mizito ulioachiwa na Kikwete

Anajichanganya kwa kutopima maneno yake kabla ya kuongea, Kiongozi makini upima ulimi wake kabla ya kutamka
 
Hamna siasa mpaka 2020!


Hivi tukimaliza sikukuu za Krismasi au Pasaka huwa hatuendi tena kanisani au kusali mpaka sikukuu zingine tena?Vyama vingi vipo kwa mujibu wa katiba ya nchi na kufanya siasa za kila siku ndo jukumu kubwa kwao.
 
Maajabu hayamuishi rais wetu Magufuli. Niliipoona mswada wa mahakama ya mafisadi unapelekwa bungeni nikajua kinachofuata ni kubadili kipengere cha katiba kuwaondolea kinga marais wastaafu ili mahakama ya mafisadi iwamulike Rais mstaafu mzee Mkapa na Mzee Kikwete.

Na hata nikaamini kwa kile kiapo cha wabunge wa CCM kupambana na mafisadi, wataweka hoja hiyo ya kubadili kipengere cha katiba ili ukweli ujulikane dhidi ya Mkapa na Kikwete. Ajabu Rais Magufuli anawakingia Kifua tena kwenye majukwaa kwamba atawalinda wasihofu. Kauli ya kusema atawalinda ni kuhalasha makosa yao.Unawezaje kumlinda mtu asiye na makosa?

Magufuli ndugu yangu dunia inakutazama jinsi unavyojichanga kwenye hii vita ya Mafisadi. Wewe mwenyewe umekuwa ukikili mizigo mizito ulioachiwa na Kikwete
Nashauri kwanza ulete hayo mashitaka yasiyo na shaka uone kama hatua hata za kubadili hiyo katiba haitafanyika.Ni mataifa mengi tu yamefanya hivo baada ya kupata mashitaka yasyo na shaka. yalete uone
 
Nashauri kwanza ulete hayo mashitaka yasiyo na shaka uone kama hatua hata za kubadili hiyo katiba haitafanyika.Ni mataifa mengi tu yamefanya hivo baada ya kupata mashitaka yasyo na shaka. yalete uone
kabla ya kusema lete,sikiliza kwanza kauli ya magufuli na katiba uone kama kuna uponyo
 
Back
Top Bottom