Ndg zangu kwa kadri siku zinavyopungua kuelekea uchaguzi mkuu 2010, mama Magreth Sitta juzi 27/12/2008 alifanya vituko katika uchaguzi mkuu wa UWT mkoa wa Tabora katika ukumbi wa Mirambo Sekondari, Mh huyo akiwa anatumia nguvu nyingi kuhakikisha mmoja wa wagombea anashinda nadhani ili aweze kumsaidia katika maandalizi yake ya kjugombea ubunge viti maalumu mkoa wa Tabora, vituko vya kibosile huyo viliambatana na kusimamisha mabasi yaliyokuwa yamebeba wajumbe na kugawa fedha bila woga kati ya 5000 na 10,000 kwa wajumbe na kumwombea kura mtu aliyekuwa amemuandaa Bi Sekasua ambaye hata hivyo alishindwa vibaya, tatizo langu hapa hivi hawa viongozi wanapokaa majukwaani na kuhubiri haki, utawala bora, kupiga vita rushwa huwa wanamaanisha nini hasa? Pole sana mama Sita tunakusubiri kwa hamu sana Tabora 2010, ili tuweze angalau kumalizia vibanda vyetu japo najua matokeo ya UWT mkoa yatakuwa yameweka kitu fulani akilini mwako