Maggid ana nini na CDM?

Hivi katika hali yoyote ile ambayo unafikiria; unadhani CCM wana nai ya dhati ya kuamini kuwa wanataka ya kuleta umoja ndani ya kambi ya upinzani.... Kwenye hii makala ungetuonyesha basi angalau hata mchakato wenyewe kuanzia kamati ya kanuni ilipopata barua kutoka NCCR na CUF
 
Wakuu huo ni mtazamo wa Maggid kama akili yake inavomtuma na chama cahke pia... Na pale anaposema kuwa wabunge wa cdm watazomewa hiyo ni obvious, wana ccm watawazomea sababu hawataki kuambiwa ukweli kama Maggid alivyowazomea kwa upeo wake finyu wa siasa!! Haki hata siku moja haiombwi pale inapo-compromise na ulaji wa anayetakiwa kutoa haki hiyo!! Maggid kua, siasa za kubembelezana africa hazifanyi kazi:twitch:!!!
 
Wewe ungefanya la busara ukaweka CV yako usimshusie hadhi ilhali wewe mwenyewe huna busara na ujumbe wako unadhihirisha hayo! Nina wasiwasi na elimu yako mkuu.................


Safi sana mtu wa Zanzibar, naona wewe ndio msemaji wa Majid na ni mmoja kati ya wanaoamini kuwa kitendo cha Chadema kutoka nje ya Ukumbi wa Bunge kupisha upigaji kura wa Azimio wasiloliafiki si cha kiungwana.Ninawasiwasi na uelewa wako kwa hilo ndugu yangu. Naona unataka elimu yangu, nakwahidi kama siku ukiweka thread ya kunijadidli mimi hapa JF kuhusu elimu yangu nitaiweka hadharani, kwa sasa si lazima kwani hii thead inahusu kumjadili Majid Mjengwa. Kama unahitaji zaidi nitembelee physically, napatikana

Echtensten 1103 AA
146
Amsterdam Zuidoost
Amsterdam
Netherlands.
 
Maggid na Shossi,

Tatizo la wengi humu JF ni kwamba ni wapenzi damu wa Chadema na kukiwa na criticism zenye kuwaumbua Chadema hun'gaka na kutoa maneno ya kejeli ili kumdiscredit yule aliyetoa mada aonekane mpuuzi. Hii ni dalili kuwa either mtoa hoja amewaambia ukweli au mna chuki na mtoa hoja. Sasa binafsi mtazamo ambao ni bias huwa siupendi maana huchangia kupelekea kwenye bias conclusion na wrong interpretation. Chadema nawaambia tena fikra za mwenyekiti zidumu ni mfumo hauna tofauti na CCM na hilo litapelekea chama kufa na kama sio kupotea kabisa. Ni vizuri mkajichunguza na kujipima kwani hata wale waliokuwa wanawaunga mkono kwa mbali hawatakuungeni mkono tena 2015. Waswahili hunena ukiumwa na nyoka hata nyasi zikitikisika mtu hukimbia vilevile mtu akisikia tena Chadema baada ya kuwachukia hatasikiliza hata hoja gani inazungumzwa. Sasa ushauri wangu kwenu wawili ni kwamba toeni hoja kwa misingi unayoitambua wewe ndio maana ya kuitwa msomi lazima uwe na misimamo unayoiamini. Kuna watakaokubaliana nayo na wengine kuipinga but mwisho wa siku ujumbe umefika.

Ndugu,
Hebu soma utetezi wake mweneyewe Majidi kabla ya kutushambulia wana CHADEMA......
 
Majid said:
........Na changamoto za kisiasa hazikimbiwi, hukabiliwa kwenye majukwaa ya kisiasa. Wabunge wa CHADEMA hawakuwa na sababu za msingi za kutoka nje ya bunge. Badala yake, wangepambana kwa hoja ndani ya Bunge. CHADEMA si wanajua, kuwa hatma ya jambo lile lilikuwa ni kupigiwa kura. Kwamba wangeshindwa. Ni sehemu ya mapambano ya kisiasa

Majid haelei approcha na mbinu za kisiasa.

Wafanyakazi kugoma sababu fulani fulani sio kukimbia wala sio kwamba hawajui njia muafaka za kuwakilisha maoni yao. hatua hii ya kugoma inafikiwa sababu njia zote nyingine zinakuwa zimeshindakana na upande mwingine kuonekana haujali

Wananchi wa Misri kuandama kumpiga mubarak kisheria za misri ni kosa kubwa na walivunja sheria na ni utovu wa nidhamu .kwa serikali iliyochaguliwa kihalali . S ijui Majidi atasemaje mabadiliko ya wanachi yaliyoletwa na huku wakipuuzia amri ya serikali halai waliyochagua wenyewe .

Majid anaonekana kuwa na jibu anaposema
......Badala yake, wangepambana kwa hoja ndani ya Bunge. CHADEMA si wanajua, kuwa hatma ya jambo lile lilikuwa ni kupigiwa kura. Kwamba wangeshindwa. Ni sehemu ya mapambano ya kisiasa.


  • Je CCM kwa kuwa wana wabunge wengi wakisema na wakipitisha hoja mfano kila albino nchini auwawe itakuwa kosa kwa vyama kutoka nje ya bunge. Je itakuwa kosa kwa wananchi kuandamana just bcs CCM wana wabunge wengi na ?

  • Je majid anajua jambo lililo wafanya chadema kutoka nje limepigiwa kelele miaka mingapi

  • Je majid anadhani jambo lililowafanya chadema watoke si jambo la msingi?

  • je Majid ataandika nini wabunge wa Chadema CUF, NCCR wakitoka nje kupinga malipo ya Dowans
 
habariyanyu,mwaferiana,mufwanga.nimewasalimia kilugha ili kuwaonyesha uchungu nilio nao kwa taifa.
kwanza kabla ya kuingia kwenye mada niwatahadharishe katika hili la majid huyu bwana mimi simjui ila nilipojaribu kusoma makala zake nilikuwa napata shida kidogo,nikaamua kuacha.
huyu kijana ni mwandishi wa habari wa vyombo vya bwa rostam azizi.naomba tumjadili bosi wake kwanza.huyu mtu hana huruma kwa nchi yetu amefanya mengi tu yasiyo ya kizaledo nitaorodhesha machache ili kama kuna mwenye kujua zaidi atuorodheshee ili kama tunamhukumu mwandishi wake tumhukumu kwa haki.
1.inaaminika ndiye mmiliki wa kagoda iliyokwapua mamilioni benki kuu.
2.alikuwa mmiliki wa richmond pamoja na best zake.
3.ni mmiliki wa dowans pamoja na best zake,sitawataja kwani wanafahamika na kila asiye fisadi.
4............................
5..........................
sasa kwa mtu hatari kwa taifa kiasi hiki anawezaje kumiliki vyombo vya habari waandishi wakawa huru.alijaribu kulihonga kanisa likamshtukia hela yake ikarudishwa.nina wasiwasi hata misikiti na taasisi za kiislamu ameshajaribu kuhonga[kwa tabia yake ya kuwapambanisha watz kwa maslahi yake bila kujaliathari na sina uhakika kama alifanikiwa kwa waislamu] sasa mtu hatari kama huyu unategemea nini juu wa magazeti yake.

majid hawezi kuipenda cdm kwa vyovyote kwani cdm ndiyo inayofichua maovu yote ya huyu bwana.
sasa ushauri wa bure kwa bwana majid mabomu aliyotega huyu bosi wake anajua kuna siku yatalipuka na nina uhakika ameshatafuta na uraia wa mahali pa kukimbilia sasa majid aamue moja kutafuta na yeye mahali pa kukimbilia au aamue kukaa na nguvu ya uma.
yote kwake nirahisi kwani kama ameoa mzungu kupata uraia huko ni rahisi na kama akibaki na nguvu ya uma atakuwa amesaidia na wanyalukolo na watz kwa ujumla.huo ndio ukweli wa mambo sitegemei bwana magid na wapambe wake wanishambulie nje ya hoja .
nawakilisha
 
Wengi wa waandishi wa habari nadhani na huyu ni mmojawapo walifeli sekondari div 4 au 0 wakaunga unga. Hivyo uandishi wa habari usio na msimamo ndio tabia yao. Mjengwa hana tofauti na Kibonde.
 
Ili watu washirikiane lazima kuwa na sababu. Na sababu kuu ni kuwa wanaoshirikiana lazima kila mmoja awe anapata faida zaidi kuliko ambao anapata kabla ya kushirikiana. Sasa CHADEMA wao wanaona hawatapata faida yeyote katika kushirikiana, lakini CUF, NCCR and others wanaona watapata faida zaidi. Kwa hali hii CHADEMA hawawezi kukubali ushirikiano kwani hakuna faida kwao.

Hili ni jambo simple hata wewe Majid ukitaka kufanya ushirika na mtu mwingine lazima ungalie unapata nini cha ziada kwenye huo ushirika. La sivyo utakuwa tu unatoa msaada wa kumwinua mwingine bila wewe kufaidi chochote. Kibao zaidi huyu mtu unayetaka kumsaidia ni mshindani wako.

Lakini kwenye siasa hakuna kumwinua mwingine kwani siasa ni ushindani. Ndio maana kila chama kilicho na mbunge pale bungeni kiliwasimamisha wagombea wao kwenye majimbo ili kushindana, kulikuwa hakuna ushirikiano kule wakati wa kupiga kura. Sasa kama vyama vilishindana wakati wa kupiga kura na kikatoa kimoja kimeshinda kwa kiasi cha kuwa na nguvu ya kufanya mambo yake chenyewe ndani ya bunge kwa muujibu wa kanuni zilizopo inakuwaje leo waambiwe washirikiane wale wale walikuwa wanashinda nao kwenye uchaguzi?.

Inabidi tukumbuke kwenye siasa pale kila chama kinapoamua kwenda kwenye uchaguzi peke yake, vyama vyote vinakuwa kwenye ushindani. Hii ina maana kila chama kinaona chama kingine ni mpinzani wake. Kwa hiyo kama vile CCM inavyoona vyama vingine ni vya upinzani, na kwa CHADEMA nao vyama vingine vyote ikiwemo na CCM ni vya upinzani. Tunaachani na matumizi ya neno upinzani linavyotumika hapa Tanzania, ili tuwe na maana pana zaidi ya upinzani ambao ni kila mwenye kushindana ni mpinzani wa mwingine.
 
sijaona chochote cha maana alichosema. Chadema wame-make a statement kwa kutoka. Sasa yeye kama hapendi ni shida zake. Siku izi kila mtu anayeweza kushika peni na kuandika anaandika!
 
Muachane tu ni mganga njaa ni kama bendera.Hao wanaomtunza wakifirisika anahamia kwingine hamna haja ya kumpa umaarufu tumpotezee tu
 
Makindi, yote uliyoyaandika ni UONGO MTUPU, umeyaandika bila chembe ya haya. Hata hivyo, naheshimu uhuru wako wa kujieleza. Umefika mahali unaandika kuwa nilitoa msimamo kuwa ni kwa nini nitampigia kura JK! Kama una ushahidi wa hilo uweke hapa hadharani, ukishindwa useme tu samahani kama una chembe za uungwana.

Niliyoyaandika ni maoni yangu. Niliandika nikijua nachochea mjadala na si wote watakaokubaliana nami. Ni kawaida, mie mpenzi wa Simba, kuna hata Simba wenzangu wanaonichukia.

Mwaka juzi kulikuwa na sakata la mchezaji Athumani Iddi kufungiwa na TFF kucheza soka kwa vile Simba hawakumpa kibali cha uhamisho. Simba walisema wako tayari kumwona Athumani Idi akiuza ndimu kuliko kumruhusu kurudi Yanga. Niliandika makala kwenye gazeti la Sayari kumtetea Athumani Iddi. Niliweka bayana kuwa, kuwa nilikuwa mpenzi wa Simba lakini kwa lile nilisimama upande wa Athumani Iddi.

Siku ile nilipigiwa simu nyingi na kutumiwa sms za WanaSimba wenzangu wenye hasira. Ikafika hata mmoja wa viongozi wa Simba alinipigia na kuniambia; " Maggid wewe si Simba mwenzetu, ni kondoo uliyevaa ngozi ya Simba!"

Na juzi usiku nimeshambuliwa vikali na Redio Imaan ya Morogoro. Nimeambiwa maneno mengi ikiwamo kuwa mimi mnafiki, mchochezi , na kuwa natumiwa kupambana na Waislamu. Kisa? Niliandika kwenye Raia Mwema kuwa redio hiyo inachochea uhasama kati ya Wakristo na Waislamu!

Tatizo langu ni kuandika mawazo yangu kwa uhuru. Ndio maana naamini, kuwa kuna CHADEMA wanonichukia, lakini kuna wanaonipenda pia. Hivyo hivyo kwa CCM, CUF, Waislamu, Wakristo na wengineo. Lakini naamini pia, kwa jinsi nilivyo, wote hao wanaweza pia kuniheshimu. Ni matumaini yangu.

Ndugu majjid, ni ngumu sana kwa watu kukuelewa msimamo wako. You are a flip-flop. Unauma na kupuliza kama (ashakum!) panya.Matokeo yake huna unaemtetea (wanyonge vs wenye mabavu). Kila mara unasema huo ni mtizamo wako, hiyo ni sawa. Lakini mwandishi wa habari ana hadhira (audience)! Kama una mtizamo usiojali hadhira, basi andika na usome mwenyewe chumbani kwako! Nadhani uhuru wa kufikiri na kutoa mawazo una mipaka na unaendana na tamaduni na desturi. Ndo maana ukija na hoja ya kutaka washoga waweze kuolewa na watambuliwe rasmi na sheria za TZ leo, unaweza ukakosa hadhira!
 
Ndugu zangu wanaJF' sikilizeni -
Kwanza majidd ajaangalia CDM wamejikwaa wapi, na kwanini wamejikwaa? Ila yeye amekwenda
straight walipoangukia. Kwahiyo kama yeye kweli ni mchambuzi makini wa kisiasa angeanzia na pale
walipojikwaa na siyo walipoangukia.
Pili sehemu yoyote duniani lazima ukutane na watu wanaopinga uhalisia wa mambo,hasa kwenye
mabadiliko ya kisiasa. Hivi ni nani asiyejua kuwa ccm kwa sasa haina mvuto na haipendwi tena na majority
ya watanzania? NI nani asiyejua kuwa chama cha cuf kimekaa kinzazibarzanzibar kwa faida ya Zanzibar tu?
Kwahiyo watu kama kaka Majidd,Shossi,Topical,Malaria sugu,Jeykey wa ukweli nk. Huwa sina mda wa kubishana
nao! Na hawawezi kunikatisha imani yangu ya kuwa oneday ccm itakufa na kuzikwa rasimi na kupotea ktk uso wa
dunia, na chama cha upinzani kinachokubarika na waTanganyika wengi kikitinga ikulu hiyo siku.
Zambia,malawi na Kenya kulikuwa na vyama nyoka mfano wa hiki ccm, Je leo viko wapi? Imebaki historia tu.
Huwa nashindwa kuelewa hawa watu wasiona alama za nyakati! maana upepo wa dhuruba kali unaokuja kwa kasi
kutoka KUSI hata iweje ccm hawawezi kuuzuia ng'o. Ukweli ni kwamba Wabara tumeichoka ccm na sasa tunachamachetu
mbadala. Kwahiyo mtupige,mtuvunje,mtukatekate vipande,mtuburuze,mtuhuwe nk. Hatudanganyiki na haturudi nyuma
kamwe mpaka kimeeleweka. -Nawasilisha
 
OH my God, Bakama Bange. Nini tena huyu jicho la tatu. Kwa ufupi reality ambayo ni objective per se tena katika mambo haya ya manenomaneno na views ni ngumu. Jamaa yuko biased yeye ni kushoto kulia kushoto kulia.... ahghhhhhh. Nashauri JWTZ wachukue nchi hii fasta watu kama hawa wawe wamerudi sweden kwanza, Mbona kwa Kagame safi tuu, ukileta ufisadi gun tu ahhg
 
Hakuna doubt kwamba demokrasia is the best revenge lakini katika nchi za dunia ya tatu ambako hakuna teknolojia ya kutosha, elimu, uvumilivu, upeo mkubwa wa uelewa, maendeleo ya viwanda na hata pia maadili ya kijamii, demokrasia imekuwa leseni ya kuabuse one another. Watu wa Tanzania wame experience hili uchaguzi wa 2010.

Sasa waandishi wetu wa habari wamekuwa part ya class ambayo inazidi kudidimiza demokrasia. Journalistic hypocrisy inaingia katika waandishi wetu wa habari. It’s free only to condemn our own politicians, Mjengwa criticizes our CDM politicians for their support towards a true clean democracy.

Journalists should be professional and expert in economics, international relations and parliamentary affairs. The majority of the existing journaists are only expert in asking questions, deriding the politicians and taking sides (bigger the bahasha ndivyo utakavyokuwa well supported)
 
Mkuu maggid umemjibu huyo bwana lakini hujajibu hoja nyingi na za msingi,umeongea kwa ujumla mno kuhusu misimamo yako lakini tunataka ujibu hoja za mada uliyoibua,zimetolewa hoja nzuri tu hebu tumia busara na elimu yako kuzijumuisha na kutoa majibu yakueleweka na si mifano ya simba na yanga tunazungumzia siasa na mwelekeo wa taifa hili Maggid.
 
Hivi nani kasema busara ni kutokutoka nje? Na ccm na cuf wanataka Chadema wawe na "busara" kutokutoka nje, kwani lengo la Chadema ni kujionesha kwa ccm na cuf kwamba wana busara? Halafu ccm na cuf wakishafurahishwa na tabia ya Chadema iweje?
 
Huyu jamaa ni opportunist, mara yupo Kwanza jamii, mara global publishers, mara JF. Kinachonishangaza ni kwamba anapuliza huku na kule. Waandishi wa namna hii ni hatari sana. Nashukuru watanzania wamekomaa kuweza kuchuja pumba na mchele.
 
mnataka watu wote wafikiri kama nyinyi. It is not healthy. na mnapalilia udictator wa mawazo.
 
Mkuu twende taratibu kidogo, kusema kwamba Majjid anaona kwa jicho la tatu ni kututukani sisi kwamba ni mambumbu hatuoni mbali, na unamweka Maggid kwenye hadhi ya umungu kwamba yeye hawezi kukosea, hapana mkuu wote humu tuna akili timamu na hatutompa mtu yeyote au niseme sitompa mtu yeyote nafasi ya kufikiri kwa niaba yangu. Maggid ni binadamu na huwa anakosea na ananunulika vilevile ushahidi upo japo hapa sio mahakamani na kama anabisha ajitoze sasa hivi kwenye hii thread nilimlipuwe sasa hivi
ONYO: KAMA UNAISHI NYUMBA YA VIOO USIMCHOKOZE KICHAA. TUMO HUMU KWA SURA MBALIMBALI. KARIBU MAGGID.

Nilichokisema ni kiwa Maggid ana uhuru wa kutoa mawazo yake na si lazima awafurahishe CDM au CCM hii ni kuwa anapoandika akaikosoa CDM ategemee kutukanwa na kusakamwa na wana CDM wa hapa JF na nje hali kadhalika akiwaandika vibaya CCM au CUF hawatamwachia.
 
Back
Top Bottom