GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,556
- 108,897
Tunapokuwa tunakuja humu Jamvini ( JamiiForums ) na kutoa mawazo yetu ya ' Kitaalam ' kabisa ambayo huwa hayalengi ' ushabiki ' wa upande wowote ule bali huwa tunasimamia ' uhalisia ' katika kutokana na kubobea Kwetu katika kufuatilia mambo ya dunia muwe mnatuelewa.
Kwa takribani nusu mwaka sasa kama hata siyo mwaka kamili Magazeti pendwa ya ' Udaku ' yanayomilikiwa na Mtu ' mjanja mjanja ' Erick Shigongo ya Kiu, Ijumaa na mengineyo yamekuwa yakija na taarifa za Kuizihaki nchi ya Marekani kwa kuipendelea nchi ya Korea ya Kaskazini ( DPRK ) huku kila mara wakisema kuwa Marekani itapigwa na mara nyingine waliandika Marekani ' ndembendembe ' na mengineyo mengi tu.
Kila siku nimekuwa nikisema kuwa kwa sasa hakuna nchi yoyote duniani ambayo ' Kijeshi ' inaweza ikapambana au hata tu kuitisha Marekani na kama zipo basi jua tu ya kwamba inachokifanya hizo nchi ni Kujambisha tu / Kupiga Mkwara ila kiukweli hata wenyewe wanajua kuwa ' mziki ' wa Marekani hawauwezi na hauwezekaniki.
Hatimaye sasa Yule Yule Mtu ambaye alikuwa ni Kipenzi cha Magazeti ya Shigongo na waliyekuwa wakimtumia kama ' Nguzo ' yao Kuu ya Kibiashara hasa baada ya kugundua Udhaifu mkubwa wa Watanzania wengi katika kufuatilia mambo ya Kimataifa Kiongozi wa Korea Kaskazini amesalimi amri kwa Marekani na sasa ameomba kuonana na Rais wa Marekani mwezi May ili afanye nae mazungumzo ya kumuomba ' Msamaha / Radhi ' kwa yote aliyokuwa akiyasema na mikwara yake mbuzi kwa Marekani.
Hivi kama Mataifa yanayosifika kwa Vita Urusi na Iran na yenyewe yameufyata kwa Marekani huyo ' Mpuuzi ' wa Korea Kaskazini angeweza kufanya lolote kwa Marekani? Ama hakika hatua hii ya Kiongozi wa Korea Kaskazini kuomba ' po ' kwa Marekani imemuumbua mno Shigongo na Magazeti yake ya ' Udaku ' na sasa sijui kuanzia siku zijazo watakuwa wanakuja na taarifa gani kwani walikuwa wakiitumia mno ' mikwara ' mbuzi ya Kiongozi wa Korea Kaskazini ili wauze Magazeti yao.
Ni vyema sasa na Wao ( Magazeti ya Shigongo ) watuombe radhi upesi kama siyo haraka akina siye tuliobarikiwa akili na maono kwani ni mapema sana tulijua kuwa Korea Kaskazini kuna mahala tu tena padogo ' watategwa ' na Marekani na watapaingia na kweli wamepaingia na sasa wanajuta na wanahaha kuwalamba miguu Marekani.
Marekani haina ' Mbabe ' duniani.
Nawasilisha.
Kwa takribani nusu mwaka sasa kama hata siyo mwaka kamili Magazeti pendwa ya ' Udaku ' yanayomilikiwa na Mtu ' mjanja mjanja ' Erick Shigongo ya Kiu, Ijumaa na mengineyo yamekuwa yakija na taarifa za Kuizihaki nchi ya Marekani kwa kuipendelea nchi ya Korea ya Kaskazini ( DPRK ) huku kila mara wakisema kuwa Marekani itapigwa na mara nyingine waliandika Marekani ' ndembendembe ' na mengineyo mengi tu.
Kila siku nimekuwa nikisema kuwa kwa sasa hakuna nchi yoyote duniani ambayo ' Kijeshi ' inaweza ikapambana au hata tu kuitisha Marekani na kama zipo basi jua tu ya kwamba inachokifanya hizo nchi ni Kujambisha tu / Kupiga Mkwara ila kiukweli hata wenyewe wanajua kuwa ' mziki ' wa Marekani hawauwezi na hauwezekaniki.
Hatimaye sasa Yule Yule Mtu ambaye alikuwa ni Kipenzi cha Magazeti ya Shigongo na waliyekuwa wakimtumia kama ' Nguzo ' yao Kuu ya Kibiashara hasa baada ya kugundua Udhaifu mkubwa wa Watanzania wengi katika kufuatilia mambo ya Kimataifa Kiongozi wa Korea Kaskazini amesalimi amri kwa Marekani na sasa ameomba kuonana na Rais wa Marekani mwezi May ili afanye nae mazungumzo ya kumuomba ' Msamaha / Radhi ' kwa yote aliyokuwa akiyasema na mikwara yake mbuzi kwa Marekani.
Hivi kama Mataifa yanayosifika kwa Vita Urusi na Iran na yenyewe yameufyata kwa Marekani huyo ' Mpuuzi ' wa Korea Kaskazini angeweza kufanya lolote kwa Marekani? Ama hakika hatua hii ya Kiongozi wa Korea Kaskazini kuomba ' po ' kwa Marekani imemuumbua mno Shigongo na Magazeti yake ya ' Udaku ' na sasa sijui kuanzia siku zijazo watakuwa wanakuja na taarifa gani kwani walikuwa wakiitumia mno ' mikwara ' mbuzi ya Kiongozi wa Korea Kaskazini ili wauze Magazeti yao.
Ni vyema sasa na Wao ( Magazeti ya Shigongo ) watuombe radhi upesi kama siyo haraka akina siye tuliobarikiwa akili na maono kwani ni mapema sana tulijua kuwa Korea Kaskazini kuna mahala tu tena padogo ' watategwa ' na Marekani na watapaingia na kweli wamepaingia na sasa wanajuta na wanahaha kuwalamba miguu Marekani.
Marekani haina ' Mbabe ' duniani.
Nawasilisha.