Toa mfano wa upotoshaji !
Ok Sir,
Gazeti la Risasi 9th july 2011,lilikuwa na habari "BIBI KIZEE AFUMANIWA NA MUME WA MTU" then the same gazeti tarehe 12th july 2011 likatoa taarifa"KUMBE BIBI KIZEE ALIYEFUMANIWA NI MLOKOLE"sasa ukisoma taarifa hii ya pili inaonesha kuwa taarifa ya kwanza haina ukweli na muandishi hakuwepo eneo la tukio bali alipelekewa picha na stori aiendike...
kwa upande wangu naona ni udhalilishaji mkubwa uliofanyika kwa mama yule(Bibi Kizee)..Sio hiyo tu,sikumbuki tarehe ngapi ila ni mwezi uliopita ni gazeti la mwananchi (kama sijakosea) lilitoa taarifa ya mchungaji mmoja kuvuruga ndoa ya muumini wake,siku chache baadae gazeti hilohilo likatoa taarifa ya kukanusha taarifa ya awali kwamba sio sahihi,lakini kwa namna moja ama nyingine kuna usumbufu ambao atakuwa ameupata muhusika kutokana na habari hiyo..
Hiyo ni mifano michache najua ipo mingi,thats why nikauliza taratibu/kanuni/sheria zinasemaje?au miiko ya uandishi inaruhusu kuchapisha taarifa ambayo bado haijathibitishwa??