Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Wakuu salama?
Hivi umeshawahi kukutana na gari la kuzoa taka lenye hali nzuri? Magari yote ambayo nimewahi kukutana nayo yanakuwa yameisha, yana hali mbaya, kutu kila pahala, yametoka, na yanajikokota kwelikweli kutoka eneo moja kwenda eneo jingine!
Kwanini magari haya yanaruhusiwa kufanya kazi katika hali hiyo? Yaani ni kama upo na bomu, hata ukajigonga tu bahati mbaya likakuchana na msala! Uwajibikaji kwenye suala zima za uzoaji taka ni 0 sifuri, utafikiri hakuna watu wanaosimamia eneo hilo.
Ni kwamba wanaopewa tenda hawapewi standard ya vifaa wanavyotakiwa kutumia kukamilisha kazi hiyo, hapo hujaongelea mazingira na vifaa wanavyotumia wazoaji taka wenyewe, huu utakuwa mjadala wa wakati mwingine.
Kwanini magari haya yanaruhusiwa kufanya kazi?
Hivi umeshawahi kukutana na gari la kuzoa taka lenye hali nzuri? Magari yote ambayo nimewahi kukutana nayo yanakuwa yameisha, yana hali mbaya, kutu kila pahala, yametoka, na yanajikokota kwelikweli kutoka eneo moja kwenda eneo jingine!
Kwanini magari haya yanaruhusiwa kufanya kazi katika hali hiyo? Yaani ni kama upo na bomu, hata ukajigonga tu bahati mbaya likakuchana na msala! Uwajibikaji kwenye suala zima za uzoaji taka ni 0 sifuri, utafikiri hakuna watu wanaosimamia eneo hilo.
Ni kwamba wanaopewa tenda hawapewi standard ya vifaa wanavyotakiwa kutumia kukamilisha kazi hiyo, hapo hujaongelea mazingira na vifaa wanavyotumia wazoaji taka wenyewe, huu utakuwa mjadala wa wakati mwingine.
Kwanini magari haya yanaruhusiwa kufanya kazi?