Mafuriko Dar, mvua kali ikiambatana na radi yanyesha, umeme wakatwa

dah nijambo la kumuomba sana Mungu atusaidie kwani haya ni majanga tu ambayo hata tukitupia lawama upande mmoja matatizo yote bado tunakuwa hatujaliangalia kwa mapana yake! Unajua hata nchi zilizo endelea nako huwa majanga kama haya yanatokea na hata kama sijasahau kuna nchi moja majuzi tu hapa imekuwa katika majanga ambayo hayana tofauti sana na haya japo kuwa yakwao yalikuwa makubwa kiasi kwamba watu wengi zaidi walipoteza maisha, nijuavyo mimi kiuchumi tuko nyuma kiasi nikashawishika kuona kwamba nchi hizo kiuchumi zimetuacha na katika swala zima la majanga hazikufanya chochote zaidi ya kumuomba Mungu awasaidie hivyo basi watanzania tumuombeni Mungu atusaidie ili hali kama hii isijirudie lakini pia tuwe na utamaduni wakuyapokea matatizo tukaona niyakwetu na tukatafuta njia ya kuyatatua kuliko kukaa na kuanza kuhamishia wengine, Mungu ibariki Tanzania.
 
Yaani hiki kitengo naona kimekufa kabisa hakina disaster plan kama ipo basi kwenye makabrasha. Wananchi hawafahamu nani wa kuwasiliana naye kwenye janga hili la mafuriko. Hawajajitokeza kwenye vyombo vya habari kuwataarifu wananchi hatua gani za dharula wachukue, wapi waende kwa sasa, serikali ina mkakati gani wa uokoaji kwa wale waliozingirwa na maji.

.....Serikali taahira ndivyo ilivyo.
 
Andy Capp,wakati nyumba inaungua,kwanza aliokoa crate la beer halafu ndio akarudi kumuokoa mke wake
chi-e-andy-capp-7.jpg
 
Tatizo kubwa linalosababisha mafuriko Dar ni hii Serikali taahira (Hapana tuna ma-DR na ma-prof ) ambayo pamoja na kuliona tatizo hili kila mwaka lakini hadi hii leo haijachukua hatua yoyote (si kweli tumeongeza posho juzi juzi tu) ile muhimu kuhakikisha Jiji linatengewa fungu kubwa la pesa ili kujenga drainage system (kwa ajili ya nani? sasa barabara zisipoharibika tutakula wapi, unonekana wewe si mtanzania) ambayo itaweza kuhimili ongezeko kubwa la wakazi wa jiji na pia kuzuia kabisa mafuriko (Bila kuacha hivyo uwezi kupata misaada kutoka nje, nina waiwasi na uelewa wako wa mambo hapa nchini) kama haya yanayosababishwa na mvua kubwa hata za muda mfupi tu.

Juzi tu wametumia Shilingi bilioni 64 "kusherehekea" miaka 50 ya uhuru (Ndio matumizi mazuri hayo ulitaka tununue madaftari, madawati, dawa, mishahara ya watumishi wa uma, nk? Uelewa wako wa mambo unanitia shaka sana). Imagine pesa kama hizi zingeamuliwa kutumika katika kujenga drainage system ya nguvu (hatutapa misaada, hujaelewa nini?) ili kuondoa kabisa tatizo la mafuriko katika jiji la Dar....Kupanga ni kuchagua...hii ndiyo ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya iliyoahidiwa na msanii.

Bila hivyo unafikiri nini si tutakuwa wabunge ombaomba? Hizi pesa nizakutuwezesha sisi wabunge ili tuweze kufanyakazi kwa nafasi bila kujali wanafunzi wanakaa chini, bararabara moshi- Segera haina repea, draineji zimetulia au la, haspitali kuna dawa au la, madaraja yakivunjika tutatumia elkopta shida nini? Cha msingi hapa ni kipaumbele tu, posho kwanza.
 
poleni wana-dar
ila hatuna vikosi vya uokoaji wa dharura?ivi vile vikosi vya wanamaji siku ya sherehe za uhuru?au bado wanajipanga tusubiri
ila dar miundo-mbinu ni noumer yani nyumba zimebaba,mitaro midogo,barabara feki yani tabu tupu

tuna vikosi na zana za kupambana na waandamanaji.
 
Ni siku ya pili sasa kumekuwa na mvua kubwa sana zinazoendelea kunyesha katika Jiji la Dar es Salaam na kusababisha mafuriko makubwa. Wengi tumekuwa tukiilaumu serikali kutokana na kutokuwa na mfumo mzuri wa kutiririsha maji pindi mvua zinaponyesha.

Lakini lazima tutizame na ukubwa wa mvua zenyewe. Tumeshuhudia mabonde yenye mito mipana kama ule wa msimbazi yakifurika maji, ni miundo mbinu ya aina gani ambayo ingeweza kudhibiti hali hii, au kukabiriana na mvua za ukubwa kama huu.

Lazima tujue kuwa wakati mwingine kunakuwa na majanga yasiyodhibitika. Naamini kuwa Japan ni nchi iliyoendelea kwa kiwango cha juu, lakini yakitokea mafuriko hali huwa mbaya pia na watu hugeuka kuwa wapiga mbizi kama samaki, Taifa kubwa kama Marekani nalo limewahi kupigwa na vimbunga ambavyo husababisha mvua kubwa na mafuriko ya kutisha, nao hali huwa tete pamoja na nguvu zao kubwa kiuchumi.

Tuache kutoa lawama kwa kila kitu kwa sababu za kisiasa. Labda anayepaswa kulaumiwa hapa ni Mungu pekee iwapo kama tukianza kutafuta wa kumtupia lawama. Huu ni wakati wa kushirikiana kuwasaidia wale walioathirika na kadhia hii.

Hatujui, pengine usiku wa leo linaweza kutokea kubwa kuliko hili. Au hali kuwa shwari na kurudi katika hali yake ya kawaida.
 
Boss, katika hali kama hiyo mtu unabeba kile unachoona kinakufaa.

Na tambua kuwa katika hali ya kiwewe kama hii akili pia huwa haifanyi kazi kwa utulivu.
Na wakati mwinmgine kutokana na mazingira unalazimika kuchukua chochote ambacho utaweza kukifikia kwa mazingira uliyopo
 
Naunga mkono hoja kwa style ya wabunge wa CCM wanavyokubali hoja za serikali yao mjengoni
 
Tatizo si kudhibiti majanga, bali jinsi ya kubaliana na athari zake. Idara ya Hali ya hewa ilishatabiri kuwepo kwa mafuriko, serikali ilijiandaa vipi kukabiliana na hali hiyo. sasa hivi kuan watu wapo juu ya mapaa ya nyumba kwa zaidi ya saa 10, hapahapa dar, hakuna chombo cha uokozi kilichopwafikia.

Nilikuwa pale Jangwani leo na watu walichokuwa wanakisema kwa nguvu ni 'miaka 50 ya uhuru... mmetuonyesha masilaha mazito mazito lakini mnashindwa kuokoa maisha yetu, hizo silaha zinatusaidia nini?' Sijui ukisikia kauli kama hizo kutoka kwa wananchi unapata picha gani?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom