USSR
JF-Expert Member
- Jul 15, 2015
- 9,896
- 22,664
Unaweza kusema ndio mvua kubwa tangu tuanze mwaka 2020 na imeanza kwa kasi kubwa tangu saa kumi usiku na bado inapiga, nimepita mitaa ya Mlandizi, Kibaha, Mbezi Mwisho, Ubungo hadi nafika katikati ya Jiji mvua inatwanga tu.
Njia zote zimejaa maji na hasa pale Jangwani na maeneo mengi, hii sikuisikia jana TMA wakiitangaza nadhani hawakuiona kwenye rada zao.
Pia mvua hii imeungana na radi kubwa kiasi cha wale ambao hawakuzoea kuwatisha kiasi na miale ya radi.
Vipi mtaani kwako kuko salama? Hakuna maafa?
Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani jijini Dar imefungwa baada ya maji kujaa kutokana na mvua kubwa inayonyesha jijini Dar
Hali ilivo jijini Dar baada ya barabara ya Jangwani kufungwa
Hapa ni daraja la Kitunda kuelekea Banana Stand, jijini Dar es salaam.
Foleni Barabara ya Bagamoyo kuelekea maeneo ya Kinondoni & katikati ya Jiji asubuhi hii. Tatizo la msongamano wa magari katika bararaba kuu za jiji la Dar Es Salaam huongezeka wakati wa mvua, sababu moja ikitajwa kuwa ni ubovu wa barabara ndogo ambazo hazifai kutumika wakati huo.
Hali ya foleni ya magari katika kipande cha barabara kati ya Morocco na Victoria Jijini Dar es Salaam. Mvua zinazoendelea kunyesha katika jiji hilo zimesababisha baadhi ya shughuli za kiuchumi na kijamii kusimama kwa muda.
Mvua inayoendelea kunyesha Dar es salaam hali halisi baadhi ya maeneo ulivyo hapa Ni sinza darajani
Video ya kwanza ni eneo la Bamaga barabara ya Shekilango jijini Dar es Salaam ambao maji yamejaa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Video ya 2 hali ilivyo kwa sasa barabara ya TAZARA daraja la Mfugale na Video ya 3 ni barabara ya kuelekea Mikocheni kutokea Morocco.
Njia zote zimejaa maji na hasa pale Jangwani na maeneo mengi, hii sikuisikia jana TMA wakiitangaza nadhani hawakuiona kwenye rada zao.
Pia mvua hii imeungana na radi kubwa kiasi cha wale ambao hawakuzoea kuwatisha kiasi na miale ya radi.
Vipi mtaani kwako kuko salama? Hakuna maafa?
DART inatoa taarifa kwa umma kuwa sehemu ya Jangwani katika barabara ya Morogoro haipitiki kwa sababu ya mafuriko yanayotokana na mvua iliyonyesha usiku wa kuamukia leo, Alhamis, Januari 16, 2020.
Tunawashauri wasafiri wa mabasi ya Mwendokasi wanaotokea Kimara kuelekea mjini-kati kuwa watumie mabasi hayo mpaka Morocco halafu wachukue usafiri mbadala ikiwemo daladala mpaka mjini-kati, Kariakoo na sehemu nyingine za jiji.
Hivyo hivyo, wale wanaotokea mjini-kati kwenda Kimara wachukue usafiri mbadala mpaka Morocco ambapo wanaweza kuendelea na usafiri wa mabasi ya Mwendokasi kuelekea Kimara na nyingine za jiji.
Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani jijini Dar imefungwa baada ya maji kujaa kutokana na mvua kubwa inayonyesha jijini Dar
Hali ilivo jijini Dar baada ya barabara ya Jangwani kufungwa
Hapa ni daraja la Kitunda kuelekea Banana Stand, jijini Dar es salaam.
Foleni Barabara ya Bagamoyo kuelekea maeneo ya Kinondoni & katikati ya Jiji asubuhi hii. Tatizo la msongamano wa magari katika bararaba kuu za jiji la Dar Es Salaam huongezeka wakati wa mvua, sababu moja ikitajwa kuwa ni ubovu wa barabara ndogo ambazo hazifai kutumika wakati huo.
Hali ya foleni ya magari katika kipande cha barabara kati ya Morocco na Victoria Jijini Dar es Salaam. Mvua zinazoendelea kunyesha katika jiji hilo zimesababisha baadhi ya shughuli za kiuchumi na kijamii kusimama kwa muda.
Mvua inayoendelea kunyesha Dar es salaam hali halisi baadhi ya maeneo ulivyo hapa Ni sinza darajani
Video ya kwanza ni eneo la Bamaga barabara ya Shekilango jijini Dar es Salaam ambao maji yamejaa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Video ya 2 hali ilivyo kwa sasa barabara ya TAZARA daraja la Mfugale na Video ya 3 ni barabara ya kuelekea Mikocheni kutokea Morocco.