Mafukara milioni 30, Mabilionea 30

kuna watu humu wanaleta mambo ya vyama, lakini mkae mkijua mwisho wa siku sisi sote ni watanzania, maskini na matajiri wote ni watanzania. ndugu Zitto usikatishwe tamaa na baadhi ya maneno ya kejeli ya baadhi yetu, binafsi sina jinsi tu, lakini nina imani kubwa sana na wewe!
nafikiri tungeanzia kuangalia thamani ya UTU nchini kwetu ikoje?
 
Wivu unaowasumbua viongozi wa chadema kati ya zitto na jk ni nini????
Mbowe mbona hasemi vikao vyake vya siri na othuman ngongoseke na vikao vyake vya siri na jk pale ada estate?
 
Mbowe na dr.slaa na nyie wapiga kelele acheni kulialia,jengeni hoja kama zito kuhusu future ya nchi
 
ZITTO si ulikimbia JF na kuanzisha vi blog vyako umerudi na vi-thread vyako kila kukicha, ili tusijadili vifo vinavyotokana na POLICCM ambavyo hujapost hata comment vijana wanauwawa... mfano hii thread ni current issue? kama kiongozi wa Chadema vipi ulishawahi kuja na thread? mpinzani gani hutaki kumkosoa JK hadharani? Viongozi CDM wanatishiwa kuuwawa na TISS upo kimia... ama tusadiki ndio walewale na daima ufisadi hatuuwezi kuutoa kwa watu dizani yako wanaturudisha nyuma...

Hao wanaolialia kutishiwa kuuawa hawana hoja,Waulize wanalipi jipya walilolizungumza juu ya mstakabari wa Taifa hili???Visa vya kutungatunga kuwa wanatishiwa kuuwawa ni mchezo wa maigizo kuwaziba watanzania wasihoji Uwezo wao ulivyomdogo wa kujenga hoja.
 
JK is a past brother. I look future. Will JK contest in 2015? Dont lose focus. Be strategic. JK will not be on ballot and he has passed expiery date.

I am JF and JF is me. I am a founder and i remain so. Transformed it from Jambo to Jamii. Transformed myself from using a hidden identity to my real name. You seem to be a PAST.

Kuwa na blog sio dhambi. Makala zangu nyingi zimeletwa humu kutoka kwenye blog yangu. Lile ni jukwaa langu binafsi na hili ni jukwaa la umma. Kule nashiriki kama mimi na huku nashirikiana na wenzangu kuangalia mustakabali wa Taifa langu. Siku zote mijadala ya JF kwangu ni changamoto na ninaifuatilia.

Tatizo ukikosa hoja unaleta vioja........ rudi kwenye mada, Jadili mada. Achana na mtoa mada au anzisha thread ya kumjadili mtoa mada kama unapenda sana kumjadili mtoa mada.

I like it.."JK is a past brother .... he has passed expiery date" Ok, who is your current One? I trust on you "Mr Strategic" sitaki kuwanyima wengine utamu, mbona "umerukaruka" issue ya POLICCM kuuwa mafukara? ama ndio vioja!! mafukara million30, matriionea30. Mkuu, Binafsi sichukizwi daima na mtoa hoja nachukizwa na vitendo vya mtoa hoja hasa kijipendekeza CCM, kuudhofisha upinzani na vijana pia harakati za CDM , na nitajadili vitendo vya mtoa hoja na mjadala unaendelea...
 
mimi mwanahalisi walishanifunguaga kuhusu zitto.

hivi uelewa wako upo sawa ww?mbona mwanahalisi halihoji mbowe na umiliki wa nyumba ya kifahari kule dubai ambayo kainunua mwezi desemba mwaka 2011 kutokana na fedha za kukiuzia chama magari mitumba mabovu?
 
i like it.."jk is a past brother .... He has passed expiery date" ok, who is your current one? I trust on you "mr strategic" sitaki kuwanyima wengine utamu, mbona "umerukaruka" issue ya policcm kuuwa mafukara? Ama ndio vioja!! Mafukara million30, matriionea30. Mkuu, binafsi sichukizwi daima na mtoa hoja nachukizwa na vitendo vya mtoa hoja hasa kijipendekeza ccm, kuudhofisha upinzani na vijana pia harakati za cdm , na nitajadili vitendo vya mtoa hoja na mjadala unaendelea...

current one kwa sasa ni othuman na ngongoseke wale anaokaaga nao mafichoni mbowe pale ada estate
 
Mimi Mwanahalisi walishanifunguaga kuhusu Zitto.
HAO MWANAHALISI KWANINI HAWAJAKUFUNGUA KUHUSU Dr.slaa deni analodaiwa nachama,na kupelekea chama kuishiwa na kusimamisha ruzuku nchi nzima?
Hivi kwa nini Mwanahalisi halikukufungua kuhusu Kashfa ya Mbowe na vikao vyake na akina OTHUMANI NA NGONGOSEKE?
 
MUHTASARI WA MAHOJIANO YA MHE. ZITTO KABWE KATIKA KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA SAA 6:30

Mtangazaj
i; kuna malalamiko mengi kuhusu mikataba, inadiwa kuwa mikataba hainufaishi wananchi unalizungumziaje hili?.....
MHE Zitto Kabwe; Ni kweli kuwa nchi nyingi za kiafrika licha ya kuwa na rasilimali nyingi sana kama ardhi,madini, mafuta n.k zimekuwa hazifaidiki zaidi na rasilima hizo na kujikuta makampuni ambayo yanayochimba rasilimali hizo kufaidika zaid kuliko wananchi wa nchi hizo, na moja ya jambo ambalo limekuwa likielezwa ni mikataba ambayo nchi za Afrika zinaingia na makampuni haya ni mikataba ambayo inafaidisha zaid makampuni kuliko inavyofaidisha nchi zenyewe na sisi kwa upande wa Tanzania tuna uzoefu wa mapitio ya mikataba mwaka 2007 nilikuwa mbunge wa kamati ya jaji bomani ambayo ilipitia mikataba yote ya madini ambayo ilipelekea mapendekezo ya taarifa ile kwenda kutengeneza sera ya madini ya mwaka 2009 na baadae sheria mpya ya madini ya mwaka 2010.

Mtangazaji; Swala la mikataba limekuwa likizungumzwa sana na limekuwa kilio kwa wananchi wengi na si Tanzania tu hata baadhi ya maeneo mengina ya Afrika,kwamba watu wameshaingia mikataba lakini mikataba hainufaishi ninyi mnasema kwamba mlipitia nini mliweza kubadirisha kitu katika ile mikataba?
MHE Zitto Kabwe; yeah ndo maana tuna sheria mpya kwa mfano, katika sekta ya madini mikataba mikubwa tulionayo ni mikataba sita kwa sababu tuna migodi sita tu ya dhahabu tulionayo hapa nchini,na ilikuwa inachimba sehemu ndogo sana ya kiwango cha adhahabu ambacho tunacho hapa nchini, tukasema kwamba kwenye sheria mpya tuweke mazingira mapya ambayo makampuni mapya yatakayoingia nchini kwetu kufanya uchimbaj wa madini kusiwe na mikataba ile ambayo tulikuwa nayo zamani ambayo iliyokuwa inatulalia kwa mfano sasa hivi serikai yaTanzania kwa mujibu wa sheria ya madini ya 2010 itakuwa ma hisa kwenye migodi, kwa mfano pili uchimbaji wa madini ya vito kwa mfano Tanzanite na madin mengine ya vito sasa hivi kwa mujibu wa sheria ni kwa ajili ya wa Tanzania tu na pale ambapo wa tanzania hawana mtaji kuweza kuyachimba wanaruhusiwa kuwa na mgeni lakini yule mgeni asizidi asilimia 50%

Mtangazaji; Wengi wanasubiri kwamba labda swala la mrahaba au swala la baadhi ya kodi zitarekebishwa ziweze kuwanufaisha wananchi lakini katika mikataba ambayo tayari imekwishaingia ni kwamba nini kilichokuwa kigumu ni kwa sababu tayar mkataba umeshaingia kwa hiyo kuvunja ile mikataba imeshindikana ama ni kitu gani ama kuirekebiswe basi katika maeneo ambayo yanaonekana kwamba bado yanaendelea kuwanyonya zaid upande haswa ule ambao haunufaiki?
MHE Zitto Kabwe; Si tulifanya kazi yetu tulipitia tukatoa mapendekezo tukapeleka sera mpya ikatengenezwa na serikali, sheria mpya ikatungwa na bunge so jukumu la utendaji na namna gani ya kuboresha mambo hayo ni jukumu ambalo linapaswa kutoa maelekezo na maoni na tulifanya hivo na bahati nzuri sheria ya madini ipo bahati mbaya mpaka sasa kwenye hii sheria mpya hapajatoea migodi mikubwa ambao umetaka mikataba so hakuna kataba hata mmoja ambao umerekebishwa kwa sababu mikataba ile imebakia kama jinsi ilivyo isipokuwa kuna baadhi ya maeneo mbayo makampuni yalikubali kufanya marekebisho kidogo kwa mfano tumekosa sana kodi ya mapato kwa muda mrefu kwa sababu mwaka1997 tulipitisha sheria ambayo inasema kwamba makampuni ya madini yatarejesha asilimia...........

Mtangazaji; Kuna taarifa kuwa tume hii ilitembea nchi mbalimbali kuchunguza na kupata uzoefu labda,ebu tupe uzoefu wa nchi nyingine wa sababu mlitembelea nchi nyingine mikataba pamoja na mapato ya nchi zinazopata hizo ambazo zinatembelea kwa ajili ya kupata uzoefu zinafanana na mikataba ambayo Tanzania ama nchi za afrika zinapata?
MHE Zitto Kabwe; haziwezekani kufanana kama kwasababu kila nchi ina mazingira yake lakini pia ningependa kuliongezea kama ambavyo proffesor Muhongo ni jambo la kuelewa ili wanaloita mfumo wa kodi katika sekta ya madini kwa maana ya ...... regime na kwa mfano watu wengi wamekuwa wakitolea mfano kule Botswana, taifa la Botswana linapata asilimia 50 ya mapato yanayotoana na dhahabu. Watu wengi wanatoa mfano wanasema Botswana ni asilima 50 lakin wanasahu kwamba botswana, kampuni hii .....ya ambayo ni ushirikino kati ya serikali ya Botswana na kampuni ya Dibias hawalipi income tax,kwa sababu ni makubaliaono yao kwamba ni kampun ya serikali 50 50 hamna kodi fulani fulani,hamna mrahaba kwahiyo kitakacho kupatikana wanagawana ina maana kwamba serikali yenyewe inapaswa kuwekeza kwa hiyo ni modo ambayo inatumika, afrika kusini ina mrahaba ni sifuri(0) juzi ndo wamebadirisha sheria kwa ajili na wao waanze kuwa na mkataba lakini tatizo tulilonayo Tanzania ni kwamba mikataba ambayo tuliingia miaka ile ya tisin ni mikataba ambayo tuliingia tukiwa hatuna uzoefu katika maeneo ya madini na hasa so upande wa wataalamu wa jeologia au wataalam wamiamba au wataaam wamaswala kama hayo tatizo letu kubwa watanzania ni wataalam wakiuchumi iambao wanaweza wakasoma mfumo wa kodi nakuweza kuona hapa kampuni inapata nini na serikali inapata nini.

Mtangazaji;
unona kwamba haya ambayo yanapatikanna katika mapato katika mkataba ambao tayari makampuni ya Tanzania yameingia ni mapato mazuri ama niyale ambayo mlikuwa mkitarajia
MHE Zitto Kabwe; Hapana, tunapaswa kupata zaidi kwa mfano bado tuna misamaha mingi sana ya kodi kwenye makampuni haya ambayo ni kama tunawapa ruzuku ili waweze kazalisha bado hatufanyi uongezekaji wa thamani ya kutosha ndani ya nchi yetu kwa sababu tatizo kubwa ambalo linaitaguliza afrika ni mwamba bado sisi expoters kwa hiyo tunapeleka kazi nje badala ya hapa ndani leo hii kwa mfano tunatoa msamaha wa kodi kwa makampuni ya madin kuagiza mafuta kwa ajli ya uzalishaji wa umeme kwenye mifodi kwanini tusihaikishe ya kwamba shirika la umeme linasambaza umeme kwenye migodi na kuweza kutengenza hiyo linkage katika sekta ya umeme na sekta ya madini.

Mtangazaji;
unadhani sasa nini kifanyika sasa haya matatizoyaliojitokeza kwa sababu tumeona uzoefu wa Tanzania labda na baadhi ya nchi nyingine, umemskia waziri anasema nchi nyingine katika mikataba bila kuwa na uzoefu bila kuwa na wataalam kwamba imeingia tu na inabidi kukubali kuendelea na mikataba hiyo kwa sasa japo kuna sheria zimefanyiwa marekebisholakin kwa ajili ya makampuni yatakayo kuja hapo baadae,
MHE Zitto Kabwe
; jibu ni moja tu uwazi kwa mikataba na mimi wala nisingependa kuchukua nafasi kama hii kusema nani wa na kumlaamu kwamba ni wanasiasa au n.k kama professa anavyozungumza mi ninachokisema ni kwamba ukitaka kupambana na rushwa kwenye mikataba weka mikataba wazi, uzoefu wangu unanionesha kwamba Tanzania tumefanya mapitio ya mikataba muda mrefu sana,hiyo sekta ya madini tunayosema sasa hivi kila mtu sasa hivi kila mtu anazungumzia ripoti ya bomani kwa sababu baadhi yetu tulivyoinga kwenye kamati ya bomani tulilazimisha serikali kwamba tutashiriki kwenye kamati iwapo tu taarifa itawekwa wazi ndo maana leo kila mtu anazungumza kuhusu kamati ya bomani lakini kabla ya kamati ya bomani kulikuwa na kamati nyingi sana lakini hakuna kitu kilichowekwa wazi kwa mfano wazir ameagiza TPDC ipitia mikataba iliongia ya gesi, TPDC ndo iliingiia mkataba, wazir ndo ameingia mkataba huwezi kuwa mtu ambae unaingia mkataba we ndo umesaini, mkataba we ndo upitie mkataba, tulichokisema nikwamba tunataka mikataba iwe wazi ikishakuwa wazi wananchi wataona mkataba gani mzuri na mkataba gani mbaya maana yake kwa uzoefu wangu unaonesha mapitio hayaleti suluhushi mapitio yanafanywa wanasiasa wale wale wakae wajue lakini hatupati jibu la moja kwa moja
 
Mh. Zitto, kwanza pole sana na majukumu. Pia asante sana kwa kutukumbuka wana jukwaa (nilidhani umekimbia missile)!!

Mh. Zitto, ninayo mengi ningehitaji kuyafahamu kutoka kwako maadamu umekuja lakini naomba nianze na hili ili twende sawa:-

Mh, umezungumza vizuri sana na kwa uyakinifu, ila naomba kabla hujaendelea utufafanulie juu ya tuhuma zinazo kukabili kuhusu "HATA WEWE PIA UMETOROSHA PESA KWENDA USWIS KIASI CHA $3.5mln." Je nikweli(unalizungumziaje)? Je huoni kwamba nawewe "UNAFUKARISHA" watz(kama ni kweli)!?
hahahahahahah...."HATA WEWE PIA UMETOROSHA PESA KWENDA USWIS KIASI CHA $3.5mln." Je nikweli(unalizungumziaje)? Je huoni kwamba nawewe "UNAFUKARISHA"
Hili jambo ni zuri sana..sema umekosea mtu wa kumuuliza..Swali linamfaa sana Mbowe na Lema waliolamba hela ya M4C iliyofanyika jijini Dar es Salaam..Kwenye kikao cha kamati kuu walipohojiwa hawana jibu wanamba samahani tu.
Hili swala Linamhusu sana Dr.slaa na Josephine waliokopa pesa za chama,kujengea nyumba Bunju.Ona sasa chama kimefirisika kabisa,Ruzuku nchi nzima imesitishwa kwa muda wa miezi 6.
 
labda tukuulize zile pesa za m4c ambazo watanzania maskini wamechangia lema na mbowe wamezipeleka wapi?

Wee umeamua kusema kwasabubu husikii au huelewi ....subiri helkopta na magari yaje endelea kuchangia hoja ya zito acha umbea

 
Ni kweli. Lazima tuanzie hapa. Kwamba mtu anayetaka kuwa mtumishi wa umma lakini anafanya biashara aache biashara. Aweke kwenye 'blind trust' biashara zake katika kipindi chote cha utumishi wa uuma. Mataifa makubwa tena ya kibepari duniani yanafanya hivi. Sisi Taifa lililotoka kwenye ujamaa tunashindwa kuchukua hatua hii. Mara 3 nimepeleka muswada Bungeni kutaka kutungwa kwa sheria ambayo itadhibiti mgongano wa maslahi kati ya wafanyabiashara ambao ni wanasiasa na mra zote imekataliwa hata kuchapishwa kwenye gazeti la serikali (GN).

Nakubaliana na wewe kabisa kwamba hapa ndio mahala pa kuanzia. Kisha uwazi wa mali za viongozi. Hivi sasa tunatangaza mali lakini wananchi hawana access. Matokeo yake ni wananchi kuwa na mawazo tofauti kuhusu viongozi wao. Daftari la mali na madeni ya viongozi liwe wazi. Mfano kwa wabunge liwekwe pale ofisi za Bunge Dar na Dodoma. Daftari liwe wazi kwenye website ya Bunge. Ili kama kiongozi amedanganya iwe rahisi kwa wananchi kumsema na kuona kuona kama anamiliki mali zaidi ya kipato chake.

Uwazi ni msingi mkubwa sana wa kupambana na ufisadi. Uwazi utaondoa majungu na kuzushiana. Uwazi utawapa
nguvu wananchi juu ya viongozi wao.

Kama kweli wewe binafsi unakiri tumetoka kwenye UJAMAA na tuko kwenye UBEPARI unashangaa nini kuwa na Mafukara Milioni 30 na Mabilionea 30? Maana moja ya sifa kuu ya mfumo wa UBEPARI (Ambao wewe unadai tumo) ni kuwepo kwa matabaka tena kati ya walionacho na wasio nacho, mashindano bubu ya watu kuchuma fedha nk. nk.

Kitu ambacho kiko wazi ni kuwa, kwa sasa Siasa imewekwa kuwa njia kuu ya watu kuchuma fedha na kuupata utajiri wa haraka. No matter what, Siasa na Wanasiasa wako kwenye fursa kubwa ya kuchuma fedha watakavyo, kujilipa posho nono, kupokea rushwa kubwa kutoka kwa makampuni ya kibepari ili kulinda maslahi yao, kukwepa urasimu katika mahitaji mbalimbali ya kihuduma wanayoyahitaji na kupitisha biashara na maslahi yao binafsi.

Makala yako hii inataja uwepo wa mabilionea 30,hawa ni akina nani? Kuna Bilionea asiye mwanasiasa kwa sasa? Ni wachache. Jiulize kwa nini Ufisadi umekaa meza moja na Siasa yetu? Jibu ni rahisi sana, kuna ndoa ya Ufisadi baina ya Wanasiasa na Wafanyabiashara ambayo msingi wake ni huohuo kutengeneza mabilionea huku wakulima, wavuvi, wafugaji wakipigwa kumbo na kubaki kwenye lindi la ufukara.

Unasema tumeingia kwenye mfumo wa UPEBARI (Sijui ni lini?) hivyo, kubali tu uwepo wa Mabilionea hao 30 kati ya Mafukara Milioni 30, ndiyo sifa kuu ya UBEPARI, haiepukiki.Hata wewe kwa fursa uliyonayo una kila sababu ya kuchagua kundi la Mabilionea as far as UBEPARI unaruhusu Mashindano ya kuvuna utajiri baina ya watu, unaweza maana wenzako wameweza, pengine utakuwa umeanza, sijui.

Waumini wa dhati wa Mfumo wa Ujamaa kama (Karl Marx na Prof. Shivji ambaye unakiri ni mwalimu wako) muda wote wanalia na UBEPARI na sifa yake kuu ya matabaka katika jamii. Wamekuwa wakitoa wito wa kuyamaliza kama si kupunguza gape lililopo sasa.Prof. Shivji kila wakati amekuwa akipigania marejeo ya Sera ya Ujamaa na Kujitegemea.Hata Nyerere (RIP) alikufa akisisitiza kuwa haoni tatizo kwenye sera hii.

Ukweli ni kuwa, hata kama kutakuwa na utetezi wa namna gani dhidi ya Ufukara unaomtesa mwananchi wa kawaida huko kijijini bado Wanasiasa watabaki kuwa wa kwanza kulalamikiwa na Mafukara wanaotoka nchi ya KIJIJINI (Si nchi ya MJINI). Sheria zinapitishwa na wanasiasa, Bajeti za maendeleo zinapitishwa na Wanasiasa lakini Wanasiasa hawahawa (Hasa Wabunge(?)) ndiyo wenye fursa ya kuiwajibisha Serikali pale inaposhindwa kuwajibika ipasavyo.
 
bilioni huanza na milioni. Ukitaka kujua naye yumo kwenye list ya watu wanaomiliki bilioni, ni kuangalia maisha yake. Sijawahi kuliona gari lake analotumia hilo hammer, lakini naambiwa ni kati ya magari wanayotumia wenye nazo. Kama hana angelipata wapi?
napata shida kugundua jinsia yako kama ni ke au me...kwa sababu unatumia akili ya wenzio,ya kwako umepeleka wapi?
Utaishije kwa kusikiasikia mambo?
 
Eti ZITTO anazohofisha upinzani.how? sahihi ziliangusha mawaziri 8.huko ni kudhoofisha upinzani?lakini umemsikia kiongozi gani wa chadema anayeongelea mafanikio hayo makubwa.huyu mfumo wa kidini na kichaga ndani ya chadema mwakani lazima uondoke maana tumechoka na mbinu hizi.
 
Mleta mada hajui maana ya ufukara na umaskini ki undani. Umaskini na ufukara ni vitu tofauti kwa maana tofauti.

Masikini ni yule wa kuonewa huruma, yamemkuta tu na si kwa kupenda au kujitakia. Mfano kudhulumiwa, kuumwa, kuwa na maradhi au ulema unaokufanya ushindwe kujituma. Unaweza ukawa tajiri lakini ukajikuta kwenye shida inayokufanya uitwe maskini (wa kuonewa huruma).

Mfano mtu ajulikanae ni tajiri kama Mengi au Bakhresa leo aumwe hoi kitandani, hawezi kujisaidia mpaka kwa msaada wa mwengine basi huyo ni maskini ingawa ana utajiri.

Mfano leo wewe unapita na vogue lako, likapata pancha njiani, hujui hata namna ya kufunguwa tairi ukaomba msaada (hata kwa kulipia) basi u maskini wako ndio huo na umehitaji msaada kwa wakati huo.

Ufukara ni wa kujitakia au ni sifa ya watu wa aina fulani wasiojuwa thamani ya fedha au mali. Kujilimbikizia mali na vitu vya anasa za kidunia kwao haipo kabisa, wanapopata mali au fursa ya kuwa na mali, wao haina maana kwao wala haiwabadili maisha yao na hauwakuti kuomba wala kutafuta msaada, ukiwapa hawakatai, hufurahi lakini hukitoa unachowapa kwa wengine wanaoona kuwa kitawafaa zaidi. Ukimuona fukara anatafuta mali au fedha basi ujuwe hizo si kwa ajili yake, ameshaona kuna mahali akiipeleka hiyo mali kitawanufaisha zaidi.

Mfano mzuri wa Fakiri ni Rais Ahmedinajad wa Iran.

Mfano mzuri wa maskini ni kama ilivyokuwa kwa Gaddafi (alipokosa msaada na utajiri wake) na Hosni Mubarak (alipokuwa hawezi hata kujisaidia na utajiri wake) au Nyerere (alipoumwa na akawa wa kusaidiwa). Hao wote kwa wakati fulani walikuwa maskini wa kuonewa huruma.

Ufukara (verb), Fakiri (noun).

Kuwa Fakiri ni sifa njema kabisa.

Sioni tatizo la Utajiri, umaskini na ufukara kuwa ni la kuumiza kichwa, ni vitu tu vilivyojengwa na mifumo ya kidunia ili kuwatia watu hofu na chuki.

Tajiri ana umaskini wake wa aina fulani.
Fukara ana utajiri wake wa aina fulani.
Maskini haina maana hana utajiri.

Tanzania, kama nchi yoyote nyingine duniani kuna Utajiri, Umaskini na Ufukara.

Nitajie ni nchi ipi haina hivyo.

Wewe!!!!! Mwambie Zitto arudishe mshahara anaolipwa na zile kampuni za madini..... hapo ndo atakuwa na haki ya kusema.
 
wee umeamua kusema kwasabubu husikii au huelewi ....subiri helkopta na magari yaje endelea kuchangia hoja ya zito acha umbea

magari 10 yameshafika yameandikwa m4c msaada toka uingereza,baada ya hapo kuna ambulance 3 zinakuja,helcopta sio ya chama niya mbowe alimtuma mdogo wake(binamu yake) godbless lema akaulizie bei tayari kwa kuwania urais mwaka 2015
kwa hiyo usipotoshe tunauliza lema kapelaka wapi hela za m4c pesa za watanzania????
 
Ila Zitto na wewe si sehemu ya kundi la mabilionea? au unakuja hapa kutusanifu? huna credibility ya kuwanyooshea vidole wengine, wewe ni Paulo na una mikono michafu usije kucheza na sisi.
 
Wewe!!!!! Mwambie Zitto arudishe mshahara anaolipwa na zile kampuni za madini..... hapo ndo atakuwa na haki ya kusema.

UJUMBE HUU UNGEKUWA SAHIHI KAMA UNGEMWENDEA LEMA NA MBOWE WARUDISHE PESA ZA M4C KWENYE CHAMA,DR.SLAA ALIPE DENI ANALODAIWA NA CHAMA
Mbowe na Wabunge wengine ukimtoa Zitto warudishe Posho Bungeni wanazo chukua...Mbona mbowe alizuga anarudisha VX YA BUNGE,,,NYuma ya pazia ameshakwenda kulichukua nalitumia?
 
Back
Top Bottom