Kamende
JF-Expert Member
- Mar 1, 2008
- 416
- 45
Habari zisizo rasmi ambazo zimepatikana kwa hisani ya wajanja wanusao habari za ndani za serikali, usalama wa Taifa na zile za Chama Cha Mapinduzi zimeanika kuwa mkakati kamambe umeandaliwa wa kupandikiza migogoro ndani ya kambi zinazopambana na MAFISADI.
Kundi moja la wabunge wa CCM na wafuasi wao ambao wamebainika kushadadia vita dhidi ya MAFISADI wamewekewa mkakati wa kushambuliwa kwa kuharibiwa haiba zao mbele ya jamii na pia kuwaondolea nguvu za kisiasa katika mikoa yao. Ni lazima wawekewe mazingira ya kutochagulika na pia watanyang'anywa nafasi zozote za ushawishi walizonazo.
Katika mkakati huo CHADEMA imepangiwa mkakati maalum wa kuiweka busy na hata kuisambaratisha. Hii ni kwa lengo la kuiondolea uwezo wa kujipanga dhidi ya MAFISADI katika uchaguzi ujao. Hapa waheshimiwa hawa wanajiaminisha kuwa watapandikiza migogoro ndani ya CHADEMA kila siku. Media itajaa habari za migogoro ya CHADEMA kila siku. Hatimaye UFISADI pekee utakaokuwa ukijadiliwa ni wa CHADEMA. Viongozi wa CHADEMA watalazimishwa kuwa wakijibu shutuma dhidi yao na dhidi ya chama na hivyo hawatakuwa na muda wa kurusha makombora kwa MAFISADI.
Mkakati mwingine ambao utaunganisha sana mikakati mingine yote ya kundi hili ni ule wa kutumia vyombo vya habari. Magazeti yatajaa habari enezi za propaganda hizi. Kila siku kutafumuliwa mgogoro mmoja baina ya viongozi wa juu wa CCM, Mawaziri, Vyama vingine vya siasa hasa CUF na CHADEMA na pia biashara za mahasimu wa kundi la MAFISADI zitatengenezewa propaganda ya kuzichafua.
Wakuu hawa watu wana hela nyingi na wako tayari kuzitumia kuimaliza demokrasia ya nchi yetu. Wanazitumia sasa kwa wingi ili waweke mazingira mazuri ya kuzirudisha baada uchaguzi ujao.
Tuwe macho sana na yanayotokea na yatakayokuwa yakitokea!!!
Kundi moja la wabunge wa CCM na wafuasi wao ambao wamebainika kushadadia vita dhidi ya MAFISADI wamewekewa mkakati wa kushambuliwa kwa kuharibiwa haiba zao mbele ya jamii na pia kuwaondolea nguvu za kisiasa katika mikoa yao. Ni lazima wawekewe mazingira ya kutochagulika na pia watanyang'anywa nafasi zozote za ushawishi walizonazo.
Katika mkakati huo CHADEMA imepangiwa mkakati maalum wa kuiweka busy na hata kuisambaratisha. Hii ni kwa lengo la kuiondolea uwezo wa kujipanga dhidi ya MAFISADI katika uchaguzi ujao. Hapa waheshimiwa hawa wanajiaminisha kuwa watapandikiza migogoro ndani ya CHADEMA kila siku. Media itajaa habari za migogoro ya CHADEMA kila siku. Hatimaye UFISADI pekee utakaokuwa ukijadiliwa ni wa CHADEMA. Viongozi wa CHADEMA watalazimishwa kuwa wakijibu shutuma dhidi yao na dhidi ya chama na hivyo hawatakuwa na muda wa kurusha makombora kwa MAFISADI.
Mkakati mwingine ambao utaunganisha sana mikakati mingine yote ya kundi hili ni ule wa kutumia vyombo vya habari. Magazeti yatajaa habari enezi za propaganda hizi. Kila siku kutafumuliwa mgogoro mmoja baina ya viongozi wa juu wa CCM, Mawaziri, Vyama vingine vya siasa hasa CUF na CHADEMA na pia biashara za mahasimu wa kundi la MAFISADI zitatengenezewa propaganda ya kuzichafua.
Wakuu hawa watu wana hela nyingi na wako tayari kuzitumia kuimaliza demokrasia ya nchi yetu. Wanazitumia sasa kwa wingi ili waweke mazingira mazuri ya kuzirudisha baada uchaguzi ujao.
Tuwe macho sana na yanayotokea na yatakayokuwa yakitokea!!!