Maendeleo yaingia Kigoma kwa kishindo, Hongera Serikali

Maendeleo yaingia Kigoma kwa kishindo, Hongera Serikali

Huu mkoa ulitengwa sana
jamaa wameujenga kivyao vyao
yaani kishida shida tu
 
Vipa de ni virefu kutoka kigwa ukiwa unaelekea itigi vumbi ni lisaa 1 na nusu, halafu lami baada ya hapo vumbi tena kwa lisaa limoja na nusu...
Unapo itaja Itigi
umesha toka Tabora
kutokea kigoma njia ya Uvinza
 
Kama unatokea Kigoma kweli huna shukrani.Kigoma ya enzi zile ungepita Malagarasi kipindi cha masika?.Kaeneo kalikobaki nako kana mkandarasi!.Bisha kama mikungu ya ndizi haisombwi kwa milori kwenda Tabora.Pengine wewe ni mtoto huijui Kigoma ya zamani.
mie nimepinga andiko lako kigoma, uvinza tabora lami sio kweli urambo kaliua no lami then mbele ya kaliua hakuna lami unaikuta mbele kidogo then vumbi mpaka uvinza ndo lami
 
Kigoma niliyokuwa naisikia Mimi ni tofauti na niliyoiona.Vijiji karibu vyote vimeunganishwa na barabara za kudumu,vina masoko ya kisasa,umeme wa REA unasambaa kila kona,masoko mengine yamewekewa umeme wa sola.Baadhi ya vijiji ukifika utadhani unaingia mjini kutokana na umeme.Jamaa wanajenga nyumba za matofali ya kuchoma na bati kila sehemu.Yaani karibu wanafuta nyumba za nyasi.Barabara ya Kigoma - Uvinza- Tabora sasa ni ya lami(daraja la Kikwete kwenye mto Malagarasi ni muujiza).Waha wanasafirisha ndizi kwenda Tabora kama kazi.Kigoma sasa imo kwenye big 6 katika kuzalisha zao la mahindi.Shule za sekondari za kata kila kona.Kigoma hawajawahi kuomba chakula cha msaada miaka mingi iliyopita kama siyo hapana kabisa.Aidha nimeshuhudia vipaji vikuu vya kuimba sijawahi kutegemea.Vijamaa vina maumbo madogo lakini vinaimba balaa.Tatizo la hawa Jamaa ni ubishi,japokuwa ukiwasikiliza kwa makini wana hoja.Ukibishana na Muha Hata kama ni darasa la 4 jipange sawa sawa.Kama huamini hudhuria kwenye vikao vyao vya Baraza la .madiwani.Kimsingi Kigoma nimeshuhudia maendeleo makubwa ambayo sikuyatarajia.Hongera serikali.Jitahidini kumalizia barabara ya Kigoma Nyakanazi.KIGOMA YA SASA YASONGA MBELE.
Tupia kapicha basi
 
Lindi na Kigoma bora Lindi

Miaka mingi Kule hakuna umeme wa mgao, taa za barabarani tangia 2010.

Mji una route kama 12 za daladala pale mjini, maji ya mgao yenye ratiba ya kueleweka.

Vyakula vya kila aina yaani mfuko wako tu.

Hotel za nyota 5,4,3 pia zipo.

Mwisho acha ujinga wa kizamani wa kuifananisha Kigoma na Lindi
 
Jamani kigoma ni wachawi nyie

Kule kigoma ukimuangalia mzee machoni, kesho utaamka mdomo umehamia sikioni
 
Uzi Bila viambatanisho vya tupicha kwa tusioijua kigoma tutaisifia lindi mkoa wenye bahari nzuri kuliko mikoa yote yenye bahari Tanzania maana Tanga nimefika bahari yao haifikii ya Lindi,Dar mmmmhhh walau kidogo pale mikindani mtwara.So watu WA kigoma wekeni tupicha
 
Nakubaliana na mtoa mada, kwa sasa hali nzuri aisee ila nadhani umeme wa national grid ukifika mambo yatakua mujarabu plus tabora kigoma na kigoma mwanza roads zikikamilika hakika watu watafanya biashara kigoma otherwise kwa level ya sasa imeendelea ila nimewapenda waha nimekula uyoga kwa jero tu
 
Kigoma hii hii niijuayo mm au nyingine..?? Embu weka picha hapo.. maana LINDI NA KIGOMA KUNAWIANA KABISAAA...
 
Kigoma niliyokuwa naisikia Mimi ni tofauti na niliyoiona.Vijiji karibu vyote vimeunganishwa na barabara za kudumu,vina masoko ya kisasa,umeme wa REA unasambaa kila kona,masoko mengine yamewekewa umeme wa sola.Baadhi ya vijiji ukifika utadhani unaingia mjini kutokana na umeme.Jamaa wanajenga nyumba za matofali ya kuchoma na bati kila sehemu.Yaani karibu wanafuta nyumba za nyasi.Barabara ya Kigoma - Uvinza- Tabora sasa ni ya lami(daraja la Kikwete kwenye mto Malagarasi ni muujiza).Waha wanasafirisha ndizi kwenda Tabora kama kazi.Kigoma sasa imo kwenye big 6 katika kuzalisha zao la mahindi.Shule za sekondari za kata kila kona.Kigoma hawajawahi kuomba chakula cha msaada miaka mingi iliyopita kama siyo hapana kabisa.Aidha nimeshuhudia vipaji vikuu vya kuimba sijawahi kutegemea.Vijamaa vina maumbo madogo lakini vinaimba balaa.Tatizo la hawa Jamaa ni ubishi,japokuwa ukiwasikiliza kwa makini wana hoja.Ukibishana na Muha Hata kama ni darasa la 4 jipange sawa sawa.Kama huamini hudhuria kwenye vikao vyao vya Baraza la .madiwani.Kimsingi Kigoma nimeshuhudia maendeleo makubwa ambayo sikuyatarajia.Hongera serikali.Jitahidini kumalizia barabara ya Kigoma Nyakanazi.KIGOMA YA SASA YASONGA MBELE.
Umesahau na vile vi baby vya kule ni vizuri kupita wote duniani. Na ile migebuka haipatikani sehemu yo yote nyingine duniani na ni tamu kuliko vitu vyote kwenye sayari hii. Plus na hao sokwe mtu kwenye hiyo hifadhi. Baada ya miundo mbinu kufunguka yaki ya nani Kigoma si ya mchezo. Tutegemee mafuriko ya watalii Kigoma. Arusha si cho chote kwa Kigoma. Bravo Ndalichako, mbunge mtarajiwa wa Kigoma mjini 2020. Wabunge kama Zitto ndiyo wanatuharibia sifa za mkoa wetu na kuonekana sisi ni wabishi wakati sisi wanachigoma ni poa kinoma. Sisi ni futuhi tu 24/7/52.
 
L
Miaka mingi Kule hakuna umeme wa mgao, taa za barabarani tangia 2010.

Mji una route kama 12 za daladala pale mjini, maji ya mgao yenye ratiba ya kueleweka.

Vyakula vya kila aina yaani mfuko wako tu.

Hotel za nyota 5,4,3 pia zipo.

Mwisho acha ujinga wa kizamani wa kuifananisha Kigoma na Lindi
Lindi!.Mbona kile kimji kinaonekana cha zamani sana na majengo yake kama magofu.Lindi iliizaa Mtwara lakini Mtwara sasa iko juu mno kuliko Lindi.Nenda vijijini Lindi uone nyumba za makuti.Tatizo la Lindi harakati za wananchi kujiletea maendeleo bado ziko chini.Serikali wanatakiwa wafanye Kampeni kubwa ya kuhamasisha maendeleo
 
Kigoma ulitelekezwa na Nyerere, kiongozi aliyewaletea sana maendeleo ni Kikwete, juhudi za Raisi kikwete kuiendeleza Kigoma ilikuwa kubwa sana, na urafiki wake na Zitto pia ulilisaidia sana hilo jimbo.
 
Nilichopenda kigoma vijiji vyao vingi nivizuri wamejenga nyumba bora hasa ulemwambao waziwa kusini dah safi kabisa vijiji vya rukoma igalula mgambo buhingu kalya pazuri kabisa wamejifungia zao solar karibu kila nyumba
 
Unapo itaja Itigi
umesha toka Tabora
kutokea kigoma njia ya Uvinza
Elewa point ni kwamba unapotoka kigwa ambayo ni uyui vipande virefu sana hakuna lami, unapotoka kigwa unaelekea itigi usichoelewa ni kipi hapo
 
Kama unatokea Kigoma kweli huna shukrani.Kigoma ya enzi zile ungepita Malagarasi kipindi cha masika?.Kaeneo kalikobaki nako kana mkandarasi!.Bisha kama mikungu ya ndizi haisombwi kwa milori kwenda Tabora.Pengine wewe ni mtoto huijui Kigoma ya zamani.
Unapamba na ambavyo havipambiki. Serikali kujenga miundo mbinu ni wajibu wake. Ndizi miaka yote inasafirishwa kwenda Tabora kwa njia ya reli, sema wewe hukuwahi kulijua hilo. Tabora bila Kigoma haina maisha ndiyo maana reli ikipata tatizo ni shida sana. Hii habari ya kusema Kigoma ni mkoa wa mwisho kimaendeleo si kweli. Mkoa wa Rukwa, Lindi na hata Dodoma bado ni mikoa maskini zaidi. Dodoma inabebwa na manispaa tuu lakini mawilaya yako hoi tuu. Ni vile watu wengi Kigoma wanaijua kwa maneno na si kwa kufika
 
Back
Top Bottom