Maendeleo yaingia Kigoma kwa kishindo, Hongera Serikali

Maendeleo yaingia Kigoma kwa kishindo, Hongera Serikali

urio f

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2017
Posts
302
Reaction score
271
19074892618_e2d55e54fd.jpg


Picha Na 1.jpg

Picha Na 2.jpg

Kigoma niliyokuwa naisikia Mimi ni tofauti na niliyoiona.Vijiji karibu vyote vimeunganishwa na barabara za kudumu,vina masoko ya kisasa,umeme wa REA unasambaa kila kona,masoko mengine yamewekewa umeme wa sola.

Baadhi ya vijiji ukifika utadhani unaingia mjini kutokana na umeme.Jamaa wanajenga nyumba za matofali ya kuchoma na bati kila sehemu.Yaani karibu wanafuta nyumba za nyasi.Barabara ya Kigoma - Uvinza- Tabora sasa ni ya lami(daraja la Kikwete kwenye mto Malagarasi ni muujiza).

Waha wanasafirisha ndizi kwenda Tabora kama kazi.Kigoma sasa imo kwenye big 6 katika kuzalisha zao la mahindi.Shule za sekondari za kata kila kona.Kigoma hawajawahi kuomba chakula cha msaada miaka mingi iliyopita kama siyo hapana kabisa.Aidha nimeshuhudia vipaji vikuu vya kuimba sijawahi kutegemea.

Vijamaa vina maumbo madogo lakini vinaimba balaa.Tatizo la hawa Jamaa ni ubishi,japokuwa ukiwasikiliza kwa makini wana hoja.Ukibishana na Muha Hata kama ni darasa la 4 jipange sawa sawa.Kama huamini hudhuria kwenye vikao vyao vya Baraza la .madiwani.

Kimsingi Kigoma nimeshuhudia maendeleo makubwa ambayo sikuyatarajia.Hongera serikali.Jitahidini kumalizia barabara ya Kigoma Nyakanazi.KIGOMA YA SASA YASONGA MBELE.
 
Mkoa huu ulisahaulika katika swala zima la huduma mhimu za jamii, kwa kipindi kirefu hongereni viongozi kwa kuliona hilo
 
Muache sasa zile "taaluma zenu za asili" zinazowafanya waalimu na wataalamu mbalimbali wageni wanaokuja kufanya kazi huko kujikuta wamelala nje pamoja na vibwenga kibao.
 
Picha tafadhari kusupport uzi huu.... naamini KIGOMA ndio mkoa wa mwisho kimaendeleo Tanzania
 
Picha tafadhari kusupport uzi huu.... naamini KIGOMA ndio mkoa wa mwisho kimaendeleo Tanzania
Mkuu ukisema kigoma mkoa wa mwisho kimaendeleo kuna mikoa kama Lindi yaani hali ni mbaya japo wana natural resources za kutosha
 
Kigoma niliyokuwa naisikia Mimi ni tofauti na niliyoiona.Vijiji karibu vyote vimeunganishwa na barabara za kudumu,vina masoko ya kisasa,umeme wa REA unasambaa kila kona,masoko mengine yamewekewa umeme wa sola.Baadhi ya vijiji ukifika utadhani unaingia mjini kutokana na umeme.Jamaa wanajenga nyumba za matofali ya kuchoma na bati kila sehemu.Yaani karibu wanafuta nyumba za nyasi.Barabara ya Kigoma - Uvinza- Tabora sasa ni ya lami(daraja la Kikwete kwenye mto Malagarasi ni muujiza).Waha wanasafirisha ndizi kwenda Tabora kama kazi.Kigoma sasa imo kwenye big 6 katika kuzalisha zao la mahindi.Shule za sekondari za kata kila kona.Kigoma hawajawahi kuomba chakula cha msaada miaka mingi iliyopita kama siyo hapana kabisa.Aidha nimeshuhudia vipaji vikuu vya kuimba sijawahi kutegemea.Vijamaa vina maumbo madogo lakini vinaimba balaa.Tatizo la hawa Jamaa ni ubishi,japokuwa ukiwasikiliza kwa makini wana hoja.Ukibishana na Muha Hata kama ni darasa la 4 jipange sawa sawa.Kama huamini hudhuria kwenye vikao vyao vya Baraza la .madiwani.Kimsingi Kigoma nimeshuhudia maendeleo makubwa ambayo sikuyatarajia.Hongera serikali.Jitahidini kumalizia barabara ya Kigoma Nyakanazi.KIGOMA YA SASA YASONGA MBELE.
Kikwete
 
acha uongo barabara ya tabora kigoma sio yote lami kuna kilometa kama 200 bado vumbi
 
Muache sasa zile "taaluma zenu za asili" zinazowafanya waalimu na wataalamu mbalimbali wageni wanaokuja kufanya kazi huko kujikuta wamelala nje pamoja na vibwenga kibao.
 
acha uongo barabara ya tabora kigoma sio yote lami kuna kilometa kama 200 bado vumbi
Kama unatokea Kigoma kweli huna shukrani.Kigoma ya enzi zile ungepita Malagarasi kipindi cha masika?.Kaeneo kalikobaki nako kana mkandarasi!.Bisha kama mikungu ya ndizi haisombwi kwa milori kwenda Tabora.Pengine wewe ni mtoto huijui Kigoma ya zamani.
 
acha uongo barabara ya tabora kigoma sio yote lami kuna kilometa kama 200 bado vumbi
Umemuelewa kasema uvinza kigoma
kwanza hizo 200km unazitoa wapi!!
Nivipande 3 pekee vyenye vumbi
tena kipande kirefu ni Uvinza Nguruka
Hivi viwili vya Nguruka Usinge,Kaliua-Urambo vidogo mno
 
umepita njia ya tabora-uvinza-kigoma, sasa hivi pita njia ya kigoma-kasulu-kibondo-kakonko-nyakanazi halafu tuone hizo ngojera zako zitasimama, unakula vumbi masaa 6 unakuja kuiona nyakanazi...umeme wa rea kwa kweli upo na wamejitahidi ingawa umewashwa kuanzia kasulu mjini mpaka mgombe, ila lami ilianza kurekebishwa kuanzi 2012 lakino wapi hakuna lami ni vumbi tuuu
 
Kama unatokea Kigoma kweli huna shukrani.Kigoma ya enzi zile ungepita Malagarasi kipindi cha masika?.Kaeneo kalikobaki nako kana mkandarasi!.Bisha kama mikungu ya ndizi haisombwi kwa milori kwenda Tabora.Pengine wewe ni mtoto huijui Kigoma ya zamani.
Eneo moja pekee litabaki
sehemu zingine unenzi unaendelea
 
Umemuelewa kasema uvinza kigoma
kwanza hizo 200km unazitoa wapi!!
Nivipande 3 pekee vyenye vumbi
tena kipande kirefu ni Uvinza Nguruka
Hivi viwili vya Nguruka Usinge,Kaliua-Urambo vidogo mno
Vipa de ni virefu kutoka kigwa ukiwa unaelekea itigi vumbi ni lisaa 1 na nusu, halafu lami baada ya hapo vumbi tena kwa lisaa limoja na nusu...
 
Back
Top Bottom