zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,938
Ukishindwa kusoma tazama picha,au ndo macho yako kilakitu yanaona ni kijani na njano.GAMBA CHAKAVU WE!
Hujajibu swali, ndio nini hiki?
Ukishindwa kusoma tazama picha,au ndo macho yako kilakitu yanaona ni kijani na njano.GAMBA CHAKAVU WE!
Nini hicho?
Ndiyo mpango.
Nimefuatilia kwa makini sana mwenendo wa siasa za vyama vingi hapa nchini, kiasi cha kuweza kusema kwa hakika kuwa vyama vyote vina
malengo yanayofanana ya kuhakikisha vinalinda maslahi ya vijikundi vidogo vya matajiri ambao wamejipatia utajiri huo kwa njia halali au la, na wala si kusimamia maslahi ya masikini walio wengi.
Matajiri hawa wachache kwa kutumia tamaa za mafanikio au umasikini walionao vijana wengi wamewatumia vijana hao kwenye matukio mbalimbali ya kihalifu ili kufikia malengo yao ya kisiasa kwa gharama yoyote ile. Lakini kama ilivyo kwa mbwa na mwenye mbwa siku zote mbwa ndiye anayepatwa na misukosuko mikubwa ndivyo hivyo ilivyo kwa vijana hawa wanaotumika na hawa mafisadi wachache huishia aidha kupigwa, kuteswa vibaya na wakati mwingine kupoteza maisha kabisa.
Kwa kuwa tumepoteza muelekeo sisi kama nchi, napenda kuwaasa wananchi wenzangu hasa vijana kwamba kwa sasa tuna machaguo mawili tu ya au kukubaliana na hali iende kama ilivyo na sisi tujikite kwenye shughuli zetu za kujiletea maendeleo bila kujali yanayowakuta majirani zetu au kuamuwa kwa dhati kuachana na ushabiki wa vyama na kuamuwa kuchagua viongozi kwa kuzingatia sifa bora alizonazo mtu katika kusimamia na kutetea ustawi wa wananchi, mtu asiyependa kujilimbikizia mali, anayekerwa na umasikini wa wananchi, anayeheshimu haki za binadamu na kuamini kuwa binadamu wote ni sawa nk.
Kwa ujumla kama tungekuwa tunaijuwa vizuri siasa ya vyama vingi tungenufaika sana lakini kwa kuwa ama hutuijuwi au kwa makusudi ya walioshika hatamu badala ya kufanya siasa ya upinzani wa hoja na mitazamo sasa imekuwa ni uadui, ambao kama hatutaamka mapema tutaingia kwenye matatizo makubwa kuliko haya tunayoyaona sasa.
Nimalizie kwa kusema vyama vyote vinaendeshwa na watu walewale (kimtazamo),wenye malengo yanayofanana (kulinda maslahi ya waongoza vikundi ambao ni matajiri/mafisadi wachache), kama tukichagua watu kwa uzingatia uadilifu wao bila kuangalia vyama vyao tunaweza kufua dafu mbele ya wamiliki wa hivi vyama.
Vijana tumesha tumikishwa vya kutosha na mafisadi wa vyama vyote kupitia the so called green, red or blue whatever sasa tujitambue, nchi iko chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu, Please wake up.
Mkuu usiwalaghai wana Jf vyama vya siasa vinaumuhumumkubwa sana kwa kuktakabali wa maendeleo yetu wananchi wanapo kosea ktk uchaguzi wa vyama uwagharimu daima Ktk swala zima la maendeleo so usipotoshe kabisha..!Ndugu wananchi maendeleo hayaletwi na vyama vya siasa, maendeleo yanaletwa na watu walioamua kuendelea.
Nchi ikiwa na wananchi walioamua kuendelea itaendelea tu.
Vijana changamkeni tumieni nguvu zenu. Nchi yetu ipo wanasiasa hawataweza hata siku moja kutuletea
maendeleo.