Maendeleo hayaletwi na vyama vya siasa

Maendeleo hayaletwi na vyama vya siasa

Mzee Mwanakijiji amekuwa mpiga zomari wa Magufuli. Naye anatamani awe mteule kama mwenzie Slow slow.

Ukabila unamsubua huyu Mzee!
Other wise hakuwa na chuki na Ufisadi au CCM, zaidi alikuwa anchuki na Lowassa,
Kwanini ?
Mimi sijuhi:-
Labda tujiulize ni kwanini alikimbia Tanzania?
au alitumbuliwaga JIPU na LOWASSA ?
sina hakika!
Tusubiri maaana naamini MUDA UTATUPA UKWELI!
 
Ndiyo maana binafsi siamini kabisa kuwa mabadiliko nchini yataletwa na wasomi hasa wale wenye kufurahia utawala wa CCM! Ni sawasawa na hapa Marekani ambapo historia inatuonesha tofauti ya “watumwa wa nyumbani”na “watumwa wa kondeni”.

Watumwa wa nyumbani walikuwa karibu sana na bosi na walipewa mahali pa kula na kulala na walitendewa vizuri zaidi kuliko watumwa wa kondeni. Matokeo yake ni wale watumwa wa kondeni ndio hatimaye waliweza kuwa chachu ya mabadiliko kuliko watumwa wa nyumbani. Maana hawa wa nyumbani kuambiwa kuwa kuna uhuru wanajikuta hawaamini kwamba watoke katika ‘maisha mazuri’ na kwenda kwenye ‘uhuru’haiingii akilini.

Lakini wenginewalipoweza kufunguliwa kiakili waligeuka wapelelezi wazuri sana; lakini wengine walikufa wakiwa wanafurahia kuitwa “mtumwa mzuri kwa bwana wake!”....

Haya ni maneno ya Makala ya M.M wanakijiji 2012

Mweh; mna kazi kweli sasa ni kipi hapa ambacho si cha kweli?
 
Laiti nguvu zinazotumika kupambana na wapinzani kila kukicha zingeelekezwa katika kuweka vipaumbele katika mambo ya maendeleo sambamba bin selele na mipango mkakati ya namna ya kutekeleza na kufikia maendeleo hayo kwa hakika tungekuwa mbali sana.

Ama kweli sikio la kufa halisikii dawa!
 
Mbona CCM in kuwa chama pekee cha siasa toka 1977 mpaka 1995 Maendeleo gani ya kutisha yalipatikana?
 
Wadau tushirikiani kuwaomba wabunge wa CCM wawaonee huruma wananchi kwani wamekuwa masikini hawana maendeleo yoyote licha ya Nchi yao kuwa Na Rasilimali nyingi.Inashangaza kuona Wabunge wa CCM wao wana maendeleo makubwa .Hebu wabunge wa CCM kuweni Na huruma Kwa Wananchi.
 
Wadau tushirikiani kuwaomba wabunge wa CCM wawaonee huruma wananchi kwani wamekuwa masikini hawana maendeleo yoyote licha ya Nchi yao kuwa Na Rasilimali nyingi.Inashangaza kuona Wabunge wa CCM wao wana maendeleo makubwa .Hebu wabunge wa CCM kuweni Na huruma Kwa Wananchi.

Tatizo siyo WABUNGE WA CCM tatizo sisi wananchi tunawachagua wa nini??Wakishatupa kipande cha keki na kahawa tunasahahu kama BUNGE ndilo kila kitu kwetu.

Unamkabidhi Ngedere shamba halafu unalalamika huvuni mahindi
 
Ndugu wananchi maendeleo hayaletwi na vyama vya siasa, maendeleo yanaletwa na watu walioamua kuendelea.

Nchi ikiwa na wananchi walioamua kuendelea itaendelea tu.

Vijana changamkeni tumieni nguvu zenu. Nchi yetu ipo wanasiasa hawataweza hata siku moja kutuletea maendeleo.
Wewe ni wakusamehe tu...
 
Vp Jaman hivi kwa sasa chama Kipi kipo kwa ajili ya wananchi na Sio kwa ajili yao binafsi????
Karibuni kwa mchango Nataka kuamia
 
Back
Top Bottom