Madilu ni mwanamuziki wa congo aliyeheshimika sana africa sio na watu wa kawaida kama sisi tu bali hata baadhi ya viongozi wakuu wa nchi barani africa,mfano hapa kwenye video hii chini utamuona madilu akimburudisha ikulu rais wa Gabon Mzee Omari Bongo na mkewe first lady wa Gabon mama Editha Bongo a.k.a.Editha mwana ya Sassou,huyu mama ni mtoto wa rais Dennis Sassou Nguesso wa CONGO Brazzaa..ambao nae alikuwepo kwenye hafla hii iliyoandaliwa na mkwewe pamoja na binti yake kwenye ikulu ya Gabon.
Mzee Bongo(mfupi na suti nyeusi hapo kwenye video) na mkewe Editha(mwenye gauni refu la kijani) kwa sasa wote ni marehemu,lakini Madilu pia nae hatunae tena duniani,itabaki kuwa historia hii video murua.