Mwamba wa Tanga
Member
- Apr 4, 2024
- 77
- 277
Habari wadau wa jukwaa hili
Bila shaka mko salama
Miaka 20 iliopita pale Tanga wilaya ya mkinga zamani
Muheza
Kata ya Maramba kijiji Cha Maramba kitongoji Cha msumbiji
Ilikua muda wa saa Saba usiku nikiwa natoka kuangalia mkanda wa video enzi hizo
Tulikua wengi lkn kadri tunavyokwenda ndo tunazidi kupungua mpk nafika njia panda ya kwenda nyumbani nilibaki mwenyewe
Picha lilianzia njia panda nikakutana na mtu mrefu sana akakimbiza akanipiga ngwala nikaanguka nikaburuzika Tumbo lilichubuka sana
Nilivyoamka sikuangalia nyuma nikaendelea na mbio
Lkn nafika mbele kidogo nikaona kiatu kikubwa kama buti la JEJE likiwa halina mguu lipo nyuma yangu linanikimbiza
Nilipokaribia nyumbani kiatu kikapotea.
Nafika nyumbani mzee anagoma kufungua mlango ananiambia Leo lala nje
Nikiwa mlangoni nimejibanza
Nikaona kundi kubwa la mapaka likiwa linaelekea mwisho wa mji ambako Kuna mashamba
Nilitulia tuliii
Nikalala pale pale mpk asbh
Mzee alipoamka akanikanya sana mambo ya kutembea usiku
Nikaomba msamaha yakaisha
Lkn muda wa saa moja asbh likaonekana lile buti na jembe kubwa vikiwa njia panda kilicho washangaza watu ni ukubwa wa lile buti likiwa na matope na lile jembe ni kubwa sana binadamu wa kawaida hawezi kutumia.
Na Yale matope ilikua wakati wa kiangazi.
Ikabidi mwenyekiti na wajumbe wakaita watu wao wanaowajua vikabebwa wakapeleka wanakojua wao
Sasa najiuliza lile buti kwann limenikimbiza? Na je lingenikamata ingekuaje?
Mpk Leo naogopa sana lile eneo
Bila shaka mko salama
Miaka 20 iliopita pale Tanga wilaya ya mkinga zamani
Muheza
Kata ya Maramba kijiji Cha Maramba kitongoji Cha msumbiji
Ilikua muda wa saa Saba usiku nikiwa natoka kuangalia mkanda wa video enzi hizo
Tulikua wengi lkn kadri tunavyokwenda ndo tunazidi kupungua mpk nafika njia panda ya kwenda nyumbani nilibaki mwenyewe
Picha lilianzia njia panda nikakutana na mtu mrefu sana akakimbiza akanipiga ngwala nikaanguka nikaburuzika Tumbo lilichubuka sana
Nilivyoamka sikuangalia nyuma nikaendelea na mbio
Lkn nafika mbele kidogo nikaona kiatu kikubwa kama buti la JEJE likiwa halina mguu lipo nyuma yangu linanikimbiza
Nilipokaribia nyumbani kiatu kikapotea.
Nafika nyumbani mzee anagoma kufungua mlango ananiambia Leo lala nje
Nikiwa mlangoni nimejibanza
Nikaona kundi kubwa la mapaka likiwa linaelekea mwisho wa mji ambako Kuna mashamba
Nilitulia tuliii
Nikalala pale pale mpk asbh
Mzee alipoamka akanikanya sana mambo ya kutembea usiku
Nikaomba msamaha yakaisha
Lkn muda wa saa moja asbh likaonekana lile buti na jembe kubwa vikiwa njia panda kilicho washangaza watu ni ukubwa wa lile buti likiwa na matope na lile jembe ni kubwa sana binadamu wa kawaida hawezi kutumia.
Na Yale matope ilikua wakati wa kiangazi.
Ikabidi mwenyekiti na wajumbe wakaita watu wao wanaowajua vikabebwa wakapeleka wanakojua wao
Sasa najiuliza lile buti kwann limenikimbiza? Na je lingenikamata ingekuaje?
Mpk Leo naogopa sana lile eneo