A
Anonymous
Guest
Kumekuwa na dharau nyingi zinazofanywa na madereva wanaotumia barabara ya kutoka Mbalizi kuelekea Tunduma.
Madereva hao wamekuwa waki-overtake bila kuchukua tahadhari, na mara nyingi wanafanya hivi kama chombo cha moto kinachokuja mbele yao ni pikipiki.
Unakuta dereva anataka ku-overtake na ukamuashia taa kumzuia au ukapiga honi, yeye hajali hilo anaendelea kukuletea gari, sasa mimi dereva wa pikipiki nipite wapi?
Madereva wanaoongoza ku-overtake bila tahadhari ni wale wa coastal za kutoka Mbeya kwenda Tunduma, madereva wa shuttle za Airport ya Songwe, madereva wa mabasi makubwa ya kampuni ya ABC, Shabiby, New Force, Golden Deer, na Abood, na madereva wa malori ya mafuta.
Madereva hawa wamekuwa chanzo cha ajali nyingi zinazotokea barabarani, vyombo vya usalama barabarani watimize wajibu wao ipasavyo kuwachukulia sheria stahiki madereva wa namna hii.
Pia madereva husika waache kutudharau sisi madereva pikipiki kwa sababu na sisi pia tuna haki kikatiba ya kutumia miundombinu ya barabara bila kusumbuliwa na madereva wengine.
Madereva hao wamekuwa waki-overtake bila kuchukua tahadhari, na mara nyingi wanafanya hivi kama chombo cha moto kinachokuja mbele yao ni pikipiki.
Unakuta dereva anataka ku-overtake na ukamuashia taa kumzuia au ukapiga honi, yeye hajali hilo anaendelea kukuletea gari, sasa mimi dereva wa pikipiki nipite wapi?
Madereva wanaoongoza ku-overtake bila tahadhari ni wale wa coastal za kutoka Mbeya kwenda Tunduma, madereva wa shuttle za Airport ya Songwe, madereva wa mabasi makubwa ya kampuni ya ABC, Shabiby, New Force, Golden Deer, na Abood, na madereva wa malori ya mafuta.
Madereva hawa wamekuwa chanzo cha ajali nyingi zinazotokea barabarani, vyombo vya usalama barabarani watimize wajibu wao ipasavyo kuwachukulia sheria stahiki madereva wa namna hii.
Pia madereva husika waache kutudharau sisi madereva pikipiki kwa sababu na sisi pia tuna haki kikatiba ya kutumia miundombinu ya barabara bila kusumbuliwa na madereva wengine.