Nini maana ya Kampuni ya kukusanya Madeni(debt collection agency)?
Zinafanyaje kazi?
Wanafaika wa hizi Kampuni ni akina nani?
Je,zinasajiriwa na mamlaka gani?
Taratibu zipi zinatakiwa kufuatwa katika ukusanyaji wa madeni?
Tukianza na maana ya kampuni ya kukusanya madeni, ni wakala binafsi wa kukusanya,kufuatilia deni au mkopo kwa niaba ya mdai halisi mpaka pale deni litakapokuwa limelipwa.
Kampuni zinaomba zabuni au zinatafutwa na mtu au watu ambao wana madeni lakini kwa sababu mbalimbali hawana uwezo au muda wa kufuatilia madeni hayo.Sababu zinaweza kuwa Muda wa kufuatilia kuwa adimu,kuepuka vulugu katika kufuatilia deni kwa hiyo kwa maana nyingine wanahamisha risk kwenda kwa kampuni kwa makubaliano ya malipo.
Ufanyaji kazi wa kampuni unatofautiana kutika kampuni moja kwenda nyingine lakini kuna mambo muhimu kabla ya kuanza kufanya kazi ya kudai wanatakiwa wawe nayo;
* Barua ya utambulisho toka kwa mdai halisi kwenda kwa mdaiwa,hii ni kwa ajiri ya utambulisho wa Kampuni iliyopewa zabuni ya kudai deni
* Pamoja na barua mdai anaweza kwenda kukabidhi kampuni ya kukusanya madeni kwa mdaiwa
* Kama deni lilikuwa na dhamana dhamana pia zinatakiwa kuonyeshwa kwa mdai mpya (kampuni)
* Kampuni inatakiwa kuandaa notice kwenda kwa mdaiwa ikiwa na mambo muhimu kama
Kiasi cha deni anachodaiwa
Muda wa kulipa deni tajwa
Madhara au yanayoweza kutokea kama atashindwa kutekeleza notice hiyo ndani ya muda wa notice
Namna ya kufanya malipo.
Pia ikumbukwe barua za notice nakala lazima zibaki kwa uongozi wa mtaa/kata ambayo mdaiwa anapatikana.
Akina nani hasa wanufaika wa Kampuni za kukusanya madeni;
Taasisi za fedha(bank,microfinance,wafanya biashara na watu binafsi).
Kampuni za kukusanya madeni lazima ziwe zimesajiriwa kisheria na mamlaka ya usajiri wa Kampuni kwa Tanzania ni Brela na kupewa cheti cha usajiri, Pia lazima wawe na namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN) inanayotolewa na TRA, Leseni ya biashara nayo ni kitu cha lazima kutoka halmashauri,jiji husika.
Kampuni za kukusanya zina njia nyingi ya kuhakikisha deni la mteja wake linalipwa, kama mkopo au deni vina dhamana wana mamlaka ya kukamata na kuuza kwa mnada ili kulipa deni na gharama za usumbufu pale tu utakapokuwa umepokea notice ya kulipa na kushindwa kufanya hivyo.
Wanaweza kukupeleka mahakamani kama hakuna dhamana iliyowekwa ili kuomba kibali cha mahakama kukamata mali zako.
Kampuni za kukusanya madeni ni rafiki wa wafanyabiashara na wadaiwa.
Karibu Nyakisasa Empire tukuhudumie katika kukusanya madeni na mikopo yako.
Unaweza kuwasiliana nasi kwa;
info@nyakisasaempire.co.tz
+255 (0) 782 39 66 66