Madaktari wamjibu Antony Lusekelo...

Madaktari wamjibu Antony Lusekelo...

mnaotulaumu kwa kugoma ebu tuambieni njia mbadala ambayo tungetumia ili hii serikali ya jk itusikilize.tumeanza mgomo lini na imewachukua siku ngapi kurespond?kama kweli swrikali yenu inawajali kwanini hawakutusikiliza hili mgomo uishe kabla maafa hayajatokea?mwanajeshi akienda vitani na akaua utamlaumu yeye au aliyeanzisha vita...
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Mkuu umeelezea kisomo zaidi,ila swala la kujiuliza,je kwanin madktari waligoma? Na jiulize kwanin pinda alivyoongea nao tar9 mambo yamekuwa swafi? Mbona kama week nyuma hiv j2 pinda alitoa onyo na mgomo ndo ulizidi zaidi,uoni kama pinda(serikali) ndio ilichochea mgomo? Tafadhalia add column ya kauli za serikali,iwe inasomeka hv madatkari wasipogoma na serikali isipogomo+kauli mbovu za viongozi=maafa
Mkuu, Pinda (serikali) alipoongea about a week ago, hakuonyesha kama serikali ipo tayari kuongeza mafao, ndio maana akaongelea impact za nyongeza hiyo kwenye bajeti ya serikali na kusema haiwezekani, madaktari hawakurudi kazini. Tarehe 9 juzi aliongea wazi kuongeza mafao ya madaktari, nao wakakubali kurudi kazini. Kwa hiyo hapo si kauli tu za serikali, ishu ni mafao, so naweza kusema madaktari walizingatia zaidi kusikia nyongeza ya mafao kuliko kauli nyingine hata zingekuwa za upole namna gani. Kwa hiyo kauli mbovu/nzuri za viongozi sio moja ya INPUT katika logic circuit yangu, ila nimeimerge ndani ya WAJIBU WA SERIKALI. So ninabaki na 2 inputs and 2[SUP]2[/SUP] outputs. INPUT zangu ni wajibu wa serikali na wajibu wa madaktari, na output zangu ni either kuwepo maafa au kutokuwepo maafa, kutegemeana na combinations za the two inputs.
 
Ijumaa waliporudi nina uhakika vitendea kazi vilikuwa havijafika Muhimbili. Ni sawa mgomo wao utaleta mabadiriko, lakini not at the expense ya wagonjwa kufa. Other means could have been used. Think if it were your child dying would you applause the striking doctors?

una uhakika gani?gauze zilianza kuingia siku chache kabla ya pinda kwenda kuongea na madaktari.hiyo other means ni ipi?iseme basi!
haya mambo ya kuoneana aibu ndio yaliyotufikisha hapa.mimi nashauri migomo mingine iambatane na bakora kwa viongozi ili waelewe uzembe hautakiwi.
 
Waingereza wanamsemo wao unasema "The end justifies the means."

Wakati wa vita ya pili ya dunia, England hawakuwa na uhakika kama USA yupo upande wao au German. Ili wahakikishe, ilibidi wafuate maneno ya Shakespear yasemayo TO BE OR NOT TO BE (si mtaalamu kwa hilo).
Walichofanya ni kuchukua marubani 7 wa ndege za jeshi za UK na kuwapeleka USA huku ndege zao zikiwa zimepakwa rangi ya jeshi la German. Wakaambiwa kuwa wasiongee chochote watakapoulizwa kwenye radio.

Vijana wakiwa wanajua kuwa ndiyo yalikuwa makubaliano, waliondoka wakiwa na imani wanaenda fanya kazi rahisi sana. USA walipoona ndege za jeshi za German na jamaa hawajibu, wakajua kazi imeanza, wakazishughulikia sawasawa na vijana wote 7 wakafa.
UK ikawa na UHAKIKA sasa kuwa USA wapo upande mmoja nao na ni adui na German.

Kuhusu hii sentesi ya pili, nakukumbusha tu kuwa MKONO MTUPU HAULAMBWI. Kuna watu wamekufa, yes wamekufa au kuteseka sana ila vifo vyao vimeleta mabadiliko sana Tanzania. Kwa mara ya kwanza, imeonekana kuwa Tanzania unaweza kugoma na kushinda ila inatakiwa tu kuwa na UMOJA.

Viongozi wameanza kuweka akili kichwani taratibu na kuacha kuchezea watu wengine kama hawana akili. Uchaguzi ujao, sidhani kama watu watalilia kugombea ubunge kama ilivyokuwa zamani maana wengi sasa wanalia kwani wana madeni hadi yanatisha.

Daktari atimize wajibu wake, ndiyo. Ila inauma sana kama unaona mtu anakufa kwa figo wakati mashine ya kusafisha damu, kuna kifaa kidogo tu kinakosekana na akina Nyoni hawataki kununua maana wao wana mtambo wao Msasani. This is like a JOKE.
Halafu kibaya zaidi, mtu anakuja hapa na kuanza kutulisha maneno kuwa HAKUNA MAAFA.

Museven alisema "barafu/Mvuke ni maji (H20). Ila huwezi kuniambia nikiwa na kiu, ninywe Mvuke au barafu kwa sabau tu ni Maji."
2. Serikali isitimize wajibu wake ila madaktari wakatimiza wajibu wao - hakuna maafa
 
mnaotulaumu kwa kugoma ebu tuambieni njia mbadala ambayo tungetumia ili hii serikali ya jk itusikilize.tumeanza mgomo lini na imewachukua siku ngapi kurespond?kama kweli swrikali yenu inawajali kwanini hawakutusikiliza hili mgomo uishe kabla maafa hayajatokea?mwanajeshi akienda vitani na akaua utamlaumu yeye au aliyeanzisha vita...

Ulinhanifu wako siyo sahihi. Nyie madaktari hamkuwa kwenye blink ya kuuawa at gun point. Daktari usifanye hivyo. kama Mungu kweli yupo utamwambia kuwa niligoma kwa vile nilikuwa nakaribia kufa ? Siyo kweli.
 
Tuheshimiane ndugu,unajua makato tunayokatwa na siye au unafikiri siye atulipi kodi?
huwa nawashangaa sana wanaosema 'mmesomeshwa kwa kodi zetu'kama vile madaktari wapo kwenye tax holiday au utadhani madaktari hawana wazazi au ndugu na marafiki wanaolipa kodi.napenda kuwashauri serikali kama haina fedha za kuwalipa vizuri madaktar
i wake basi iwaondolee kodi mbalimbali kama vile PAYE.
 
Mkuu,

ndiyo maana nina hamu sana kwenye KATIBA MPYA, nguvu za viongozi wa dini na Rais Zipunguzwe sana tu.

Ningelikuwa na uwezo, Tanzania ningeli i-China kwa kupiga marufuku dini zote kwa miaka kama 10 hivi. Hapo ndiyo tungeliongea sasa kisawasawa na hawa akina Lusekelo. Ona viongozi wa dini wote wanavyoikumbatia CCM kama Mlevi na Pombe yake.

Ukichunguza, Marehemu Sheick Yahya, Moses Kulola, Kakobe, Rwakatare na wengine wengi, ni Pro-CCM sana. Walikuwa wanajifungia majumbani kama vile wanasali kumbe wanafanya kampeni zao ili CCM ishinde. Walokole wanaiangamiza sana Tanzania. Kibaya zaidi ni kuwa CCM WANALIJUA HILO NA WANALITUMIA KWELI.

Flora Mbasha, Mjukuu wa Moses Kulola.......

IMG_0376.JPG


Rwakatare anajulikana mambo yake na hamna haja ya kusema zaidi. Sheick Yahya pia aliandikwa sana.

Mengine hebu soma hapa: http://amazingforums.com/forum/MUNISHI/8.html
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/124272-askofu-moses-kulola-kada-wa-ccm.html
huwa nawashangaa sana wanaosema 'mmesomeshwa kwa kodi zetu'kama vile madaktari wapo kwenye tax holiday au utadhani madaktari hawana wazazi au ndugu na marafiki wanaolipa kodi.napenda kuwashauri serikali kama haina fedha za kuwalipa vizuri madaktar
i wake basi iwaondolee kodi mbalimbali kama vile PAYE.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Kitabu cha yoshua bin sira kinapatikana kwenye biblia ya kikatoliki pekee, si rahisi kwa lusekelo kuijua hiyo kwani madhehebu na makanisa yenye mwelekeo wa kiprotestant hutumia biblia ambayo haina vitabu kama, yoshua bin sira, makabayo na vingine vitano. Biblia yakikatoliki ina vitabu saba zaidi kwenye agano la kale.
 
mkuu,

ndiyo maana nina hamu sana kwenye katiba mpya, nguvu za viongozi wa dini na rais zipunguzwe sana tu.

Ningelikuwa na uwezo, tanzania ningeli i-china kwa kupiga marufuku dini zote kwa miaka kama 10 hivi. Hapo ndiyo tungeliongea sasa kisawasawa na hawa akina lusekelo. Ona viongozi wa dini wote wanavyoikumbatia ccm kama mlevi na pombe yake.

Ukichunguza, marehemu sheick yahya, moses kulola, kakobe, rwakatare na wengine wengi, ni pro-ccm sana. Walikuwa wanajifungia majumbani kama vile wanasali kumbe wanafanya kampeni zao ili ccm ishinde. Walokole wanaiangamiza sana tanzania. Kibaya zaidi ni kuwa ccm wanalijua hilo na wanalitumia kweli.

Flora mbasha, mjukuu wa moses kulola.......

img_0376.jpg


rwakatare anajulikana mambo yake na hamna haja ya kusema zaidi. Sheick yahya pia aliandikwa sana.

Mengine hebu soma hapa: http://amazingforums.com/forum/munishi/8.html
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/124272-askofu-moses-kulola-kada-wa-ccm.html

hayo mavazi na ulokole.mh!
 
Kutokana na maneno machafu yalitolewa na mchungaji huyo madaktari wamjibu na kumfundisha anthony lusekelo kuisoma biblia vizuri, kifungu cha maandiko matakatifu kinachompa daktari mamlaka ya juu.
hiki hapa

Kitabu: Biblia takatifu: Yoshua Bin Sira 38:1-15
Baadhi ya mistari inasomeka hivi:
38:1 [FONT=comic sans ms,sans-serif]Umheshimu daktari(tabibu), kwa kadiri ulivyo na haja nae, [FONT=comic sans ms,sans-serif]na kwa heshima iliyo haki yake[/FONT][/FONT]
38:2 Kwa maana ni kutoka kwake aliye juu, daktari(tabibu) alivyoupata ufundi wake, [FONT=comic sans ms,sans-serif]hata na kwa mfalme atapokea ada (consultation fee)[/FONT]
38:3 Maarifa yake daktari(tabibu) yatamwinua kichwa chake,[FONT=comic sans ms,sans-serif]naye atasimama ni mkuu katika wakuu[/FONT]
38:6 Nae(Mungu) amewapa wanadamu maarifa, ili atukuzwe mwenyewe kwa ajili ya miujiza yake

Pia Kile Kiapo cha udaktari kinasomeka hivi:

[FONT=comic sans ms,sans-serif]"Wakati nikikishika kiapo hiki, na ijaliwe kwangu kuyafurahia maisha na kazi yangu. Jamii (serikali) iniheshimu na kunikumbuka(kunitukuza) , nikiwa hai au nimekufa" Mwisho wa kunukuu[/FONT]

Hivyo tuangalie fani hii imelindwa katika nyanja zote. Asije mtu akatudhulumu kwa namna yoyote ile hasa kwa kutumia kiapo chetu kama wafanyavyo sasa.
cleardot.gif




Kibogoyo, sitaki kuzungumzia hoja ya kumjibu Lusekelo bali maelezo yako binafsi.

Yoshua Bin Sira ni kitabu kilichoko katika Biblia ipi? Yangu inaonyesha kitabu kinachitwa Yoshua na sura zake zinaishia 24 na siyo 38 kama ulivyoitaja wewe.

Naomba kueleweshwa. Ningependa kuijua Yoshua Bin Sira inapatikana wapi au labda ni Biblia ya madaktari wengine hatujaisoma maana haituhusu.
 
Hivi huyu si ndo ule mchungaji anayehubiri huku akiwa anatunzwa madhabahuni kama mwanamuziki? Anapiga neno kidogo, ananyoosha mkono anapokea fedha,ujumbe unapotea kidogo anazuga anarudi kwenye mstari.
 
Kibogoyo, sitaki kuzungumzia hoja ya kumjibu Lusekelo bali maelezo yako binafsi.

Yoshua Bin Sira ni kitabu kilichoko katika Biblia ipi? Yangu inaonyesha kitabu kinachitwa Yoshua na sura zake zinaishia 24 na siyo 38 kama ulivyoitaja wewe.

Naomba kueleweshwa. Ningependa kuijua Yoshua Bin Sira inapatikana wapi au labda ni Biblia ya madaktari wengine hatujaisoma maana haituhusu.

matolea ya biblia yako mengi,mfano kuna wagideon,kuna kings james version, kuna toleo moja origin yake ufaransa,halafu kuna hii ya waroman,.ni biblia toleo gani unatumia wewe?
 
Mbona hatuwalaumu hawa madaktari? Tusiwe fuata upepo, tuangalie nani alikuwa na nafasi nzuri ya kuokoa maafa kati ya serikali na madaktari. Ukitaka kujua kosa la madaktari, tafakari hili:

1. Serikali isitimize wajibu wake na madaktari wasitimize wajibu wao - kuna maafa
2. Serikali isitimize wajibu wake ila madaktari wakatimiza wajibu wao - hakuna maafa
3. Serikali itimize wajibu wake ila madaktari wasitimize wajibu wao - kuna maafa
4. Serikali itimize wajibu wake na madaktari wakatimiza wajibu wao - hakuna maafa

Nilitamani kama kila mtu angekuwa na knowledge ya truth tables za logic circuit humu, ningeyachorea table maelezo yangu. Utaona kwamba maafa yatatokea pale ambapo madaktari hawajatimiza wajibu wao regardless uwajibikaji wa serikali. Kwa hiyo madaktari ndio waliokuwa na uwezo wa kuepusha vifo visivyo vya lazima, na si serikali. Mimi nitaendelea kuwalaumu madaktari
Kabla hujatuchorea hizo meza ...e..table zako hebu tufafanuliwe uwajibikaji wa serikari na madakatari halafu urudi tena na hizo meza ..er table zako !
 
wapendwa,

hebu tufikiri. mume wangu anaacha hela ya dagaa kila siku nyumbani, mie kama mama nagoma kupika hao dagaa eti nimechoka kulishwa dagaa kila siku tena huku nikijua kabisa kuwa kuwashindisha na kuwalaza njaa watoto wasio na hatia ni MAUTI kwao! nashinikiza ninunuliwe samaki, mume anasema sina hela ya samaki kwa wakati huu, mimi nasema ngoja tuone. baada ya siku kadhaa bila kuwasha moto jikoni wala kupika chochote, watoto wetu wanakufa kwa njaa huku dagaa wakiwa wamejaa tele hapo nyumbani na unga haujapungua! sasa hapo muuaji ni nani?

mimi si mwanasheria, ila kadiri nijuavyo, sheria za kazi haziwaruhusu madaktari, askari, zimamoto, idara za maji na nishati (kama umeme na gesi) nk. kugoma. hizi zote zinaitwa "essential services' kisheria. ikitokea dispute of right (mgogoro wa haki) wanaweza ku-opt mediation/arbitration ila ikitokea dispute of interest (mgogoro wa maslahi), wanapaswa kuitisha compulsory arbitration (mwenye kuelewa zaidi haya mambo ya kisheria naomba anisaidie katika kuweka sawa hapa)

madaktari walikuwa na mgogoro wa maslahi na mwajiri wake (serikali) japo pia walikuwa na madai yanayoonekana kama ni ya haki yakiwa yamechanganywa humo kwenye madai ya maslahi zaidi ili kupata sympathy ya jamii. cha kusikitisha sikusikia chochote kuhusu hatua za kisheria kama zilivyoainishwa kwenye sheria za kazi, badala yake nilisikia tu "tools down"! na hata hayo ya kutaka watu fulani wafukuzwe kazi nayo twaweza kusema ni maslahi/haki za madaktari?? au madai haya niyaweke kundi gani?? nikisema ni ya kisiasa tutakuwa nimekosea?

hapo mtaona kuwa TUGHE na TUCTA walikuwa sahihi kabisa waliposema kuwa mgomo huo si halali KISHERIA kwa sababu haukufuata taratibu za kisheria. ninaamini kama taratibu zingefuatwa kisheria na documemntation yote ikawekwa sawa, basi hata siku tatu za mgomo zisingefika kabla ya maridhiano kufikiwa kati serikali na madaktari. walichofanya ni MOB JUSTICE! ni kujichukulia sheria mkononi! na wameua wapendwa wetu!

kuhusu mashairi yaliyonukuliwa toka kwenye apocryphal souce ya Yoshua bin Sira 38:1-15, haiwapi madaktari utukufu wa aina yoyote zaidi ya watumishi wengine. kila mtumishi anastahili heshima, kuthaminiwa na kuenziwa huduma yake. hakuna mwanya hata kidogo kwenye biblia wa kutukuza baadhi ya fani. wao ni watumishi na wamepewa vipawa hivyo kutoka juu (kwa Baba yetu aliye mbinguni) ambaye ndiye mwenye kutawala katika ufalme wa wanadamu. hivyo wanapaswa kuwa wanyenyekevu siku zote wakitarajia malipo yao kutoka kwa Baba yetu sote aketiye katika kiti halisi cha enzi. hiyo taaluma yao ndiyo talanta yao!

kuhusu Anthony Lusekelo, sikumsikia alisema nini, kwa hiyo sina la kusema juu yake.

kwa kumalizia, (na bila kujipa haki ya kutoa hukumu) naaminini kwamba, serikali ilikosea kama ambavyo inakosea kila siku katika kusimamia sekta mbalimbali (kama si zote). madaktari nao walikosea katika kuwasilisha madai na malalamiko yao kwa mujibu wa sheria, lakini WALIOUA WAPENDWA WETU NI MADAKTARI!

Mungu awabariki sana wapendwa

Glory to God!
 
Wananchi tumechangia kuua coz nihatua gan 2liyoichukua kuwaacha wale walioandamana kuishnikza serikal?hivi mnafikir serikali haiui?inaongoza kuua serkal kwa kuptisha dawa feki,kuchakachua elimu,kuptia mauaj ya polisi,rushwa,epa nk.mbona huko hamulaumu?tunaangalia short term effects zinazooneka kirahisi ndo serkal inaamua kujtokeza,je umeshajiulza kwa nin wanafunz wanafeli sna,tatzo ni Walimu walio ktk mgomo baridi lakin hapo serkal inajua mwanafunz asiyefundshwa math. drs la 5 effects zake ztaonekana badae sna,wanaouwawa na walmu ni weng kulko na madaktar leo.ASIKUDANGANYE MTU BILA MASLAHI HAKUNA UZALENDO POPOTE,WAFISADI NCHI ALAFU WEWE UUMIE ETI UZALENDO SHENZ KABSA,sherehe miaka 50 ya uhuru wametumia mabilion kutuonesha vifaru...non sense!haki kwanza ndipo wajibu.Nchi zilzo na wananch wazalendo ni kwasabab serkal inawajal waliowake,mf. Tz ktk vita ya Kagera,nchi ilikuwa maskn lakn uzalendo ulikuwepo sabab serkal ni kwel ilikuwa maskin lakn si kwa kuwa corrupt!kufa kwa watu ni sio hoja(fallacy)tatzo ni nin na kwa nn?tafakar ajal ya meli Zenj,je abiria hawakuona kuwa wamejaa melini?,sumatra je? SERIKALI HII IPO SIKU TU...wengne nafikiri hatuelew vema au wivu tu unatusumbua dhidi ya madr. Nasisi tudai kivyetu yanayotuhusu.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Inawezekana Mzee wa upako asiwe na kifungu kilichonukuliwa katika Biblia yake, kwani nijuavyo mimi YUSHUA BIN SIRA iko katika Biblia ya Kiroma pekee. Hata hivyo cha msingi hapa ni kwamba inawezekana Mzee wa upako ameanza kuwa mwanasiasa. Maana wanasiasa wengi ni wavivu kufanya utafiti matatizo ya aina hii yakijitokeza. Mara nyingi hutegemea maelekezo ya makada na watu walio karibu nao. Ndo maana tulishuhudia Waziri mkuu akijaribu kuwalazimisha Madaktari kurejea kazini la sivyo wajihesabu kazi imekwisha bila kujua msingi wa madai yao! Sisemi Mzee wa upako apuuzwe, lakini nadhani kauli zake zisiginwe!
 
Madaktari wengi wa Tanzania wako kimaslahi zaidi wala si huruma kwa mgonjwa; ukiwaacha wachache sana ambao wanahangaika na mgonjwa na kufanya diagnosis vizuri na hata kuwa watafiti na wenye kujiendeleza wengi wao wanafanya mazao tuuuuuuuuuu.. unaweza kwenda kwa daktari akakupa the same diagnosis na dawa hata ugonjwa haujapona wakati umeenda kwake mara nyingi..

Naomba madaktari wawe na tabia nzuri, wajisomee, wafanye uchunguzi wa maradhi vema, riziki yao itakuwa juu kupita maelezo..

Lakini sasa hivi wengi wao ni malaya, walevi na hufanya kazi kwa mazoea tu hakuna uchunguzi wa kina na maelezo ya maana roho mbaya kama huna pesa etc...

Bado sijawa support mdrs
 
Ijumaa waliporudi nina uhakika vitendea kazi vilikuwa havijafika Muhimbili. Ni sawa mgomo wao utaleta mabadiriko, lakini not at the expense ya wagonjwa kufa. Other means could have been used. Think if it were your child dying would you applause the striking doctors?

Nafikiri wewe hufahamu hili lazima wachache wafe kwa ajili ya wengi hata bwana Yesu alikufa na wengi tuliokolewa. Yaani hilo haliepukiki
 
wapendwa,

hebu tufikiri. mume wangu anaacha hela ya dagaa kila siku nyumbani, mie kama mama nagoma kupika hao dagaa eti nimechoka kulishwa dagaa kila siku tena huku nikijua kabisa kuwa kuwashindisha na kuwalaza njaa watoto wasio na hatia ni MAUTI kwao! nashinikiza ninunuliwe samaki, mume anasema sina hela ya samaki kwa wakati huu, mimi nasema ngoja tuone. baada ya siku kadhaa bila kuwasha moto jikoni wala kupika chochote, watoto wetu wanakufa kwa njaa huku dagaa wakiwa wamejaa tele hapo nyumbani na unga haujapungua! sasa hapo muuaji ni nani?

mimi si mwanasheria, ila kadiri nijuavyo, sheria za kazi haziwaruhusu madaktari, askari, zimamoto, idara za maji na nishati (kama umeme na gesi) nk. kugoma. hizi zote zinaitwa "essential services' kisheria. ikitokea dispute of right (mgogoro wa haki) wanaweza ku-opt mediation/arbitration ila ikitokea dispute of interest (mgogoro wa maslahi), wanapaswa kuitisha compulsory arbitration (mwenye kuelewa zaidi haya mambo ya kisheria naomba anisaidie katika kuweka sawa hapa)

madaktari walikuwa na mgogoro wa maslahi na mwajiri wake (serikali) japo pia walikuwa na madai yanayoonekana kama ni ya haki yakiwa yamechanganywa humo kwenye madai ya maslahi zaidi ili kupata sympathy ya jamii. cha kusikitisha sikusikia chochote kuhusu hatua za kisheria kama zilivyoainishwa kwenye sheria za kazi, badala yake nilisikia tu "tools down"! na hata hayo ya kutaka watu fulani wafukuzwe kazi nayo twaweza kusema ni maslahi/haki za madaktari?? au madai haya niyaweke kundi gani?? nikisema ni ya kisiasa tutakuwa nimekosea?

hapo mtaona kuwa TUGHE na TUCTA walikuwa sahihi kabisa waliposema kuwa mgomo huo si halali KISHERIA kwa sababu haukufuata taratibu za kisheria. ninaamini kama taratibu zingefuatwa kisheria na documemntation yote ikawekwa sawa, basi hata siku tatu za mgomo zisingefika kabla ya maridhiano kufikiwa kati serikali na madaktari. walichofanya ni MOB JUSTICE! ni kujichukulia sheria mkononi! na wameua wapendwa wetu!

kuhusu mashairi yaliyonukuliwa toka kwenye apocryphal souce ya Yoshua bin Sira 38:1-15, haiwapi madaktari utukufu wa aina yoyote zaidi ya watumishi wengine. kila mtumishi anastahili heshima, kuthaminiwa na kuenziwa huduma yake. hakuna mwanya hata kidogo kwenye biblia wa kutukuza baadhi ya fani. wao ni watumishi na wamepewa vipawa hivyo kutoka juu (kwa Baba yetu aliye mbinguni) ambaye ndiye mwenye kutawala katika ufalme wa wanadamu. hivyo wanapaswa kuwa wanyenyekevu siku zote wakitarajia malipo yao kutoka kwa Baba yetu sote aketiye katika kiti halisi cha enzi. hiyo taaluma yao ndiyo talanta yao!

kuhusu Anthony Lusekelo, sikumsikia alisema nini, kwa hiyo sina la kusema juu yake.

kwa kumalizia, (na bila kujipa haki ya kutoa hukumu) naaminini kwamba, serikali ilikosea kama ambavyo inakosea kila siku katika kusimamia sekta mbalimbali (kama si zote). madaktari nao walikosea katika kuwasilisha madai na malalamiko yao kwa mujibu wa sheria, lakini WALIOUA WAPENDWA WETU NI MADAKTARI!

Mungu awabariki sana wapendwa

Glory to God!

Kinachoturudisha nyuma watu wengi ni kufananisha mifano ambayo haiendani kiutendaji wala utekelezaji. Ninamaana wewe unayewanyima watoto msosi huoni kama unaweza ukaungana na wanao ukawa unawapikia ila wanaact hawajala na linawezekana au hata mkajifanya mnautapiamlo na mnavyeti vya daktari? Sio kila tatizo linatatuliwa kwa kutesa wengine. Sina uhakika na huo usomi wako lazima utakuwa wa kukremisha au kuvuliwa ch*** ndio maana una cheti au ujuzi lakini ktk maisha ya kawaida ni zero.

Kuhusu sheria ya wapi wanapaswa kugoma nafikiri hiyo itabaki kuwa sheria na inahitaji mabadiliko sababu inaonekana iko biased na lazima kuna vifungu vinavyosema wanatakiwa wafanye kazi ktk mazingira timilifu (vifaa, ujira sahihi nk) ndio maana tunaona wanajeshi wakichukua nchi na kumpindua amirijeshi mkuu wao je ukandamizaji usikemewe ili kuepusha athari kubwa zaidi???? Tafakari
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Back
Top Bottom