Kinachoturudisha nyuma watu wengi ni kufananisha mifano ambayo haiendani kiutendaji wala utekelezaji. Ninamaana wewe unayewanyima watoto msosi huoni kama unaweza ukaungana na wanao ukawa unawapikia ila wanaact hawajala na linawezekana au hata mkajifanya mnautapiamlo na mnavyeti vya daktari? Sio kila tatizo linatatuliwa kwa kutesa wengine. Sina uhakika na huo usomi wako lazima utakuwa wa kukremisha au kuvuliwa ch*** ndio maana una cheti au ujuzi lakini ktk maisha ya kawaida ni zero.
Kuhusu sheria ya wapi wanapaswa kugoma nafikiri hiyo itabaki kuwa sheria na inahitaji mabadiliko sababu inaonekana iko biased na lazima kuna vifungu vinavyosema wanatakiwa wafanye kazi ktk mazingira timilifu (vifaa, ujira sahihi nk) ndio maana tunaona wanajeshi wakichukua nchi na kumpindua amirijeshi mkuu wao je ukandamizaji usikemewe ili kuepusha athari kubwa zaidi???? Tafakari
kwenye blue: kwa nini hujaona kuwa madaktari nao walipaswa kuungana na wagonjwa? tafakari
kwenye red: sijajua kwa nini umeacha hoja na kukimbilia unecessary personal attacks?? hata hivyo nimekusamehe. tuendelee kujadili. ubarikiwe sana mpendwa
kwenye green: je, unaweza kutuambia ni sekta gani katika nchi yetu serikali imeweza kupeleka vifaa timilifu, ajira sahihi nk? je, hujaona askari akiwa amevaa viatu vilivyotoboka, waalimu je, hujaona wakilala nyumba za nyasi? kwenye ofisi mbalimbali za serikali kama halmashauri zeyu nk, hujaona jinsi watumishi walivyopauka na kuchakaa? unajua hali za mabwana shamba zilivyo?
si afadhali hata huyo dr. anayepata posho ya 10,000/- kwa siku. polisi anapata 100,000 kwa mwezi (sawa na siku 10 tu za daktari) na hata hivyo wanakatwa 50,000 na wanapewa 50,000/ tu! nafikiri sualal hili wote tuliosikia likihojiwa hata bungeni. sasa unashauri nao wagome? je, askari magereza unajua wanafanya kazi katika mazingira gani? wanapata posho ya sh. ngapi kwa siku? wakigoma hao majambazi yakarudi mitaani yataua watu wangapi?? hebu tafakari kwa mapana ndugu yangu.
daktari huanza kazi kama afisa wa daraja la kati na sio la chini. kada nyingine huanza chini kabisa, hii limeishafafanuliwa vizuri. daktari mwenye shahada uya kwanza anaanza na mshahara karibu sawa na mtu mwenye master degree kwenye sekta nyingine. hilo unaliona ni dogo?
hatusemi kuwa wasidai haki zao, ila wajue hali halisi ya nchi yetu na wafuate sheria tulizojiwekea wenyewe kama taifa na ambazo ndio msingi wa ustaarabu wetu (civilization) kama jamii ya watu walio sawa na huru
So cheap. Extremely cheap. Si wewe ambaye kila siku unatetea CCM? unataka kusema hao (most) CCM hawako kimaslahi ndiyo maana unawatetea? Unafiquun.
mpendwa, usimjadili mtoa hoja, bali jadili hoja yake!
pia sioni kwa nini uamini kuwa kama CCM wako kimaslahi zaidi basi hilo linahalalisha madaktari wajichukulie sheria mkononi dhidi ya wagoinjwa wakioapa kuwaangalia afya zao kwa huruma na uaminifu. kumbuka mob justice waliyofanya haikuwa juu ya CCM wala serikali, bali ilikuwa juu ya wagonjwa! wana tofauti gani na 'watu wenye hasira" wanaochoma moto vibaka hadi kufa kwa kuwa tu hao vibaka wakipelekwa polisi huachiwa kwa dhamana na kuonekana tena mitaani??
kama CCM na serikali yake havifai, basi kila inapotokea fursa ya uchaguzi, tutumie haki zetu za kidemokrasia kuleta mabadiliko tunayotaka na sio kuwashukia wagonjwa wasio na hatia yoyote na kuwaua kama madaktari walivyofanya
Acha unafiki. Wengi wenu huwa mnakimbilia kujinasibisha na kauli ya Bwana Yesu kuwa "usihukumu usije ukahukumiwa" ili kujipa moyo kuwa hamfanani na mfarisayo aliyemsimanga mtoza ushuru katika ibada. Kumbe ninyi ni makaburi yaliyopakwa chokaa kwa nje na ndani mkiwa mifupa mitupu, mnawazuia watu kuingia ilhali ninyi hamuingii wenyewe, mnawakusanya watu na kuwafanya wabaya maradufu.
Mnakimbilia "usihukumu usije ukahukumiwa" pale mnapoishiwa hoja ama mnapotaka kuwatetea wazembe wenzenu. Judy katika conclusions zako nilizopata kuziona this is the worst. Unaigiza kuongea busara (ama kujishusha) kumbe unafanya unafiki. Tutawatambua ninyi manabii wa uongo kwa matunda yenu.
ooh my God!!
mbona hujadili hoja yangu, na umeamua kunijadili mimi?
mlitaka madaktari waibembeleze serikali?
binafsi nataka wafuate sheria tulizojiwekea wenyewe kama taifa la watu wastaarabu walio sawa na huru. unapofuata sheria haina maana unaibembeleza serikali. sheria ni msumeno, inaweza hata kuikata na serikali yenyewe bila kuleta maafa kwa wagonjwa wasio na hatia!
sioni vyema karne hii kuishi kwa kufuata kanuni ya survival of the fittest! kumbuka wanyonge ndio waliokufa. wenye pesa zao na nafasi za maana hata malaria wanapelekwa india, na hili madaktari wanalijua vizuri, na wengine huwasindikiza!
Lete huo unaouita "mubadala." Kitendo cha kuwaambia watu wengine "tafuteni" ni ushahidi kwako wewe mwenyewe kuwa ni mvivu wa kufikiri. Tuambie huo mbadala ni upi.
Watu wanaongea hisia (feelings) badala ya mantiki. Hawana majibu wanaishia kutisha watu na vifungu vya vitabu vitakatifu. Ndiyo maana Spika Makinda aliwaambia akina Mhe. T. Lissu (nnaowaheshimu) leteni hoja badala ya kutisha wabunge kwa kumtaja Rais.
mpendwa,
ni kweli ninaweza kuwa nimeandika kwa hisia. lakini pia nimegusia suala la kisheria na nimesema kuwa licha ya sheria ku-categirise huduma za afya kama essentiasl services, madaktari wameipuuza sheria na kujichukulia sheria mikononi mwao wakafanya walivyoona wao kuwa sawa na hatimaye wamewaua watanzania wenzao wasio na hatia kwa sababu zilizo ndani ya wigo wa kushughulikiwa kisheria!
kwa kweli ushabiki si mzuri, kaulize wagonjwa na wafiwa wakwambie kama wanakubali walistahili hayo yaliyowakuta huko mahospitalini wakati wa mgomo!
mbarikiwe sana wapendwa
Glory to God!