Madaktari wamjibu Antony Lusekelo...

Madaktari wamjibu Antony Lusekelo...

Hapo kwenye umalaya na ulevi si kwa madaktari tu bali hili linamhusu kila mmoja wakiwemo wanasiasa mwananchi wa kawaida na hata baadhi ya vigozi wa dini so in general binadamu wote are concern

Naomba nikusahihishe kidogo umalaya na ulevi si kwa madaktari tu na pia baadhi ya wanasiasa mwananchi wa kawaida na hata vigozi wa dini manake naona kwenye viongozi wa dini tuu ndio umeweka baadhi kana kwamba wanasiasa na wananchi wote ni malaya na viongozi wa dini ndio baadhi.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Mkuu, hebu jaribu kuendana na thread. Kwa hiyo una maana effect za MSD kudispose tons and tons of medicine last year zimekuja kujitokeza immediately mara baada ya madaktari kugoma? Na una maana hizo effects za MSD zimeisha ghafla baada ya madaktari kurudi kazini?
We inaelekea uko karibu na serkali uwashauri kuwa waangalie na makundi mengine nayo yanakuja na dizaini hiyo ebu imagine zero zinakuwa zaidi ya mia mbili shule moja. Usije ukaanza oooh na walimu nao wamefelisha wanafunzi.
 
ukisoma sheria za kazi utajua kwamba mgomo hutokea wakati waajiriwa wanadai maslahi ambayo hayapo kisheria.mgomo ni shinikizo lisilofuata sheria na utaratibu,sasa siwaelewi nyie mnaotaka urembo wa kufuata sheria n.k mnajidanganya tu na kupiga porojo tu.mnaleta theories zisizo na kichwa wala miguu.halafu naona mnajichanganya sana kwa sababu ikija kwenye maslahi mnasema ooh daktari ni sawa na kazi nyingine kama muhasibu,mwalimu,dereva n.k lakini ikija kwenye kugoma eti daktari ni mtu muhimu hafai kugoma,stupid politics!!unafiki huu na wanafiki kama miss jud ndio chanzo cha kukosa uwajibikaji serikalini,kitu kinachotuletea maafa.hivi wewe miss jud ulitoa maoni gani kuhusu maafa ya gongo la mboto,mbagala,meli ya zanzibar,watu kupigwa risasi arusha,mbeya,mara?unaongelea nn kuhusu mama mjamzito kufariki kisa amekosa oxygen baada ya umeme kukatika na generator kukosa mafuta huku ?tuache unafiki!madaktari wamevumilia wakitegemea serikali au mwananchi atafanya kitu lakini wapi sasa wakati umefika na watu wameamka.

mpendwa,

hapo kwenye red: nimeishasema wazi kuwa yoyote anayejua vizuri sheria zinasemaje inapotokea dispute of interest kwenye essential services, atusaidie kutuweka sawa. sasa kama we mwenzetu umesoma vizuri sheria za kazi, hebu tufafanulie zinasemaje kuhusu vitu kinachoitwa hiuzo ESSENTIAL SERVICES, DISPUTES OF RIGHTS, DISPUTES OF INTERESTS na COMPULSORY ARBITRATION

nijuavyo mimi, migogoro ya kikazi inayohusisha madai yasiyo ya kisheria ndiyo ijulikanayo kama dispute of interest na migogoro ya kikazi ihusuyo madai yaliyo ya kisheria hujulikana kama dispute of rights na madai ya aina zote hizo yameainishwa utaratibu wake wa kuyadai kisheria na hata suala la mgomo (strike) limetamkwa na kuanishwa taratibu zake kisheria. kwa hiyo siyo kweli usemapo kuwa mgomo ni shinikizo lisilofuata sheria na utaratibu!

kwenye blue: naona bado ni personal attacks zinzendelea. ni vizuri kama daktari wangu mwenye madai sahihi, ukajikita katika kujadili mada na sio kunishambulia mimi binafsi.

asante kwa kunielewa na ubarikiwe na Bwana.

Na nyie madaktari mmefanya makosa hamna cha kusema mpo deep kwenye bible wala nini maana bible hiyo hiyo imeandikwa " mtii mamlaka (serikali) kwa maana mamlaka(serikali ) zote zinatoka kwa MUNGU"

nashukuru mpendwa Kimbweka kwa kudokeza hilo.

wengi wanatafuta biblia pale tu wanapotaka ku-justify mambo fulanifulani tu lakini kamwe biblia hawaitumii kama taa ya kuongoza miguu na maisha yao kila siku! utaona hawa madaktari imewabidi hadi kufukua apokriphal account ya YBS ili mradi tu waonekane wako sawa na wajikweze juu ya fani nyingine, kitu ambacho Bwana Mungu hajawahi kukiamuru na wala hakijawahi kuingia kwenye moyo yake!

tatizo wabongo tumezoea kushabikia ili tuonekane tunaweza, but hakuja jambo la msingi hapo. kama mtu unaakili timamu na unauwezo mkubwa wa kufikiri, nadhani utakubaliana na ukweli pamoja na kuwa madaktari walikuwa wanadai haki yao lakini hawakustahiri kugoma kabisa, na damu zote za waliokufa kwa ajili ya mgomo zi juu ya mikono yao wala sio serikali.

kwa nini wabongo hatubadiliki tuweke maslay ya taifa mbele kuliko maslai binafsi, ivi wewe leo kama kaka/dada/mama/baba/shangazi/mjomba/au ndugu yako yeyote angekuwa anakata roho mbele yako pale muhimbili ili hali daktari amesimama anamwangalia ungemlilia nani, ungeenda ikulu kwa pinda kumuomba amuokoe au ungemlilia daktari pale muhimbili.

fikiri kabla ya kuandika bana. wengine yanatuuma koz tumeexperience shuruba za mgomo na tumeshuhudia madaktari wakipitapita katika varanda za hospitali ile hali wagonjwa wanateseka kwa maumivu wodini yaani hata kuwapiga sindano za kutuliza maumivu walikataa, kweli ilikuwa inaumiza sana roho kwa sie tuliekuwa pale

achilia mbali mafisadi wachache walioko madarakani wanaoiba fedha lakini lamsing lilikuwa kuokoa maisha ya watanzania.

mpendwa Gango2,

hapo kwenye red, nakuunga mkono kabisa. walilolifanya madaktari ni kujichukul;ia sheria mikononi na kwa mgomo wao wamesababisha vifo vingi vya watui wasio na hatia wala nafasi ya kuwatimizia madai yao. kwa kweli wamemuonea sana MTANZANIA MNYONGE NA KUUTWAA UHAI WAKE ILI WAPATE MASLAHI BINAFSI! huu ni ukatili wa kutisha sana kuwahi kushuhudiwa katika nchi yetu!

kwenye blue: kama kweli mtu aliyetoka nyumbani kwake kufuata huduma yako hapo hospitali, wewe unayelipwa mshahara utokanao na kodi yake, anakufa mbele ya macho yako, ukiwa na vifaa na madawa husika tena vya serikali na unajua kabisa ungeweza kufanya chochote kusaidia kuokoa maisha yake na usifanye, kwa kweli wewe ndiye muuaji na dhalimu, na hapo UPENDO wako ni sifuri kabisa, huo hauna tofauti na UJAMBAZI WA KUTUMIA TAALUMA!

inauma sana wapendwa. nitaendelea kuwaombea madaktari wote kwa Mungu.

mbarikiwe sana

Glory to God!
 
Pamoja na uzuri wa quotations hizo zinazowapa utukufu na kweli mnastahiri kuheshimiwa kwa kazi yenu, hakuna kifungu ambacho kinasema unaponyimwa ujira wako ufanye nini. Sidhani utatuonyesha kuwa ukinyimwa ujira UGOME na UUE kwa kutowatibu wagonjwa. Hapo kuna tatizo, kweli mnastahili kulipwa ujira mzuri, kazi yenu ni ngumu na inahitaji umakini mkubwa. Nadhani wapendwa kuanzia sasa mpange kama msipopewa ujira mfanye nini, but at the same time your major concern should be to preserve life. Then you will win muder case siku ya hukumu

I hate pathetic people. "Their major concern should be preserving life", Well! What is your major concern then?

Kulilia haki bila kuchukua wajibu ni tabia mbaya kabisa. Wapi kwenye Biblia kumeeleza kuwa mgonjwa anahesabiwa haki kwa ugonjwa wake na hawajibiki kuchagua serikali inayomjali daktari wake?
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Na nyie madaktari mmefanya makosa hamna cha kusema mpo deep kwenye bible wala nini maana bible hiyo hiyo imeandikwa " mtii mamlaka (serikali) kwa maana mamlaka(serikali ) zote zinatoka kwa MUNGU"

Na wapi kwenye Bible kumeandikwa kuwa hayo majipu yako ni shida yao?
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
madaktar wanahak kwa wanacho kidai. yeye mchungaj mbona anaweka account no. bank, tigo na m-pesa akiomba pesa. na hajawah kuongoza ibada bila ya muda wa sadaka. jaman tuthamin nafas ya kila mtu na haki zake na sio kulaaaaaaaniiiiiiiiiii watu vibaya hata MUNGU HAPENDIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII
 
mpendwa, usimjadili mtoa hoja, bali jadili hoja yake!

pia sioni kwa nini uamini kuwa kama CCM wako kimaslahi zaidi basi hilo linahalalisha madaktari wajichukulie sheria mkononi dhidi ya .............................................................................

kama CCM na serikali yake havifai, basi kila inapotokea fursa ya uchaguzi, tutumie haki zetu za kidemokrasia kuleta mabadiliko tunayotaka na sio kuwashukia wagonjwa wasio na hatia yoyote na kuwaua kama madaktari walivyofanya

..................................................................................

ooh my God!!

mbona hujadili hoja yangu, na umeamua kunijadili mimi?

......................................

Judy, unafiki si sura ya mtu wala maumbile yake. Ni tabia. Napozungumzia unafiki nazungumzia michezo ya kuuma na kupuliza, kusema huku hili na kule lile. Kama hoja zako zingekuwa na mashiko nisingekuwa na haja ya kukuita mnafiki. Kuhukumu madaktari kuwa wameua huku ukijilinda kuwa "hujipi haki ya kuhukumu" ndiyo unafiki wenyewe. Hii si personal attack bali ni ukinzani dhidi ya kile ulichosema na mbinu chafu za kutisha watu kwa misingi ya dini. Utetezi wako juu ya Topical bado ni dhaifu kwa kuwa mbali na ukengeufu wa hoja aliyotoa anabakia kuwa mfano wa watu wasiotabirika. Majibu mepesi na ya jumlajumla (eg wengi wa madaktari wanaangalia maslahi binafsi) huku mtu huyu huyu anapigana awezavyo kutetea CCM ahata katika mambo yaliyo wazi ndiyo msingi wangu wa kumuita mnafiki.

Upande wako (na wenzako) michezo ya kuzuga kuwa mnajinyenyekeza huku mkibebesha watu hukumu ndiyo unafiki wenyewe. Bado nasimamia palepale, acha unafiki.
 
3D unaonekana unatoa hoja kwa kutukana/kuwaona wenzako hawana ubongo etc. Arrogance ya hali ya juu!!!! Nimesoma posting zako, unakuwa na hasira na kutukana. jaribu kurekebisha tabia hiyo. yakatae mawazo ya wenzako bila kutukana- maneno ya cheap, extremely cheap unafiquun (ingawa sijui maana yake) yanaweza yakawa replaced na maneno kama sikubaliani na mtazamo wako, umekosea, etc etc

Bado nasimamia pale pale ukiishia kuambia watu wameua (sijui unajua uzito wa kauli yako hii!!!) halafu ukasema watafute mbadala huku ukiwa huna majibu ya mbadala huo ndicho nachoita uviu wa kufikiri. Unatamka kauli "zinazoappear" kuwa nzuri ilhali ni impractical.

Mbadala mtafuteni nyie, mnaogoma. Sisis tunaona mlivyofanya si vizuri KUUA. Nyie madaktari mna sauti ya kusikika, waulize watanzania watawapa mbadala, kama mmeshindwa kupata mbadala.

Ndiyo maana nikakwambia unaona uvivu kufikiri (unatoa kauli cheap) halafu unakuja kulalamika umetukanwa. Madaktari wamefuata hatua zipi hadi kufikia kugoma? Au waligoma ghafla. Ulitaka walie? Ukija kuambiwa ukweli usilalamike umetukanwa.

NB. Unafiquun ni unafiki.
 
Juduth asante sana. 3D anachofanya ni personal attack, ad hominen argument. Nimemwambia humu kuwa ajifunze kujibu wenzake bila kuwatukana. Kila mmoja ana matusi, lakini wastaarabu hatufanyi hivyo.

Sioni nilipotukana. Niliyemwambia mnafiki nimemweleza sababu za kusema hivyo. Kitendo cha wewe kujisikia vibaya kuitwa mnafiki halafu ukawa na amani kumuita mtu mwingine muuaji tukiitaje? Mi najua ni unafiki na ndiyo sababu hata sasa nakwambia uache unafiki.

Kitendo chako cha kuwaambia madaktari wasigome hata pale wanapotoa rai zao na wakapuuzwa ila watafute mbadala ambao hata wewe huujui ndiyo hoja nyepesi hizo (labda tusi limekuja kwa kuweka neno cheap). Mjomba, usikimbilie kutafuta sympathy kwa kujitaja mstaarabu (Miss Judith anajipigia chapuo kuwa "hahukumu"), wastaarabu huleta mbadala na si kutaja neno mbadala. Haya bana "Tafuta mbadala."
 
ukisoma sheria za kazi utajua kwamba mgomo hutokea wakati waajiriwa wanadai maslahi ambayo hayapo kisheria.mgomo ni shinikizo lisilofuata sheria na utaratibu,sasa siwaelewi nyie mnaotaka urembo wa kufuata sheria n.k mnajidanganya tu na kupiga porojo tu.mnaleta theories zisizo na kichwa wala miguu.halafu naona mnajichanganya sana kwa sababu ikija kwenye maslahi mnasema ooh daktari ni sawa na kazi nyingine kama muhasibu,mwalimu,dereva n.k lakini ikija kwenye kugoma eti daktari ni mtu muhimu hafai kugoma,stupid politics!!unafiki huu na wanafiki kama miss jud ndio chanzo cha kukosa uwajibikaji serikalini,kitu kinachotuletea maafa.hivi wewe miss jud ulitoa maoni gani kuhusu maafa ya gongo la mboto,mbagala,meli ya zanzibar,watu kupigwa risasi arusha,mbeya,mara?unaongelea nn kuhusu mama mjamzito kufariki kisa amekosa oxygen baada ya umeme kukatika na generator kukosa mafuta huku ?tuache unafiki!madaktari wamevumilia wakitegemea serikali au mwananchi atafanya kitu lakini wapi sasa wakati umefika na watu wameamka.

Akina Judy hawajui haya. Wako bize wanafanya maigizo ambayo mimi bila kumung'unya maneno nayaita UNAFIKI.
 
poleni sana madaktar, nyie, waalimu na wanajeshi ni watu mnaohitaji kipaumbele kuliko mtu yeyote. poleni sana...
 
Judy, unafiki si sura ya mtu wala maumbile yake. Ni tabia. Napozungumzia unafiki nazungumzia michezo ya kuuma na kupuliza, kusema huku hili na kule lile. Kama hoja zako zingekuwa na mashiko nisingekuwa na haja ya kukuita mnafiki. Kuhukumu madaktari kuwa wameua huku ukijilinda kuwa "hujipi haki ya kuhukumu" ndiyo unafiki wenyewe. Hii si personal attack bali ni ukinzani dhidi ya kile ulichosema na mbinu chafu za kutisha watu kwa misingi ya dini. Utetezi wako juu ya Topical bado ni dhaifu kwa kuwa mbali na ukengeufu wa hoja aliyotoa anabakia kuwa mfano wa watu wasiotabirika. Majibu mepesi na ya jumlajumla (eg wengi wa madaktari wanaangalia maslahi binafsi) huku mtu huyu huyu anapigana awezavyo kutetea CCM ahata katika mambo yaliyo wazi ndiyo msingi wangu wa kumuita mnafiki.

Upande wako (na wenzako) michezo ya kuzuga kuwa mnajinyenyekeza huku mkibebesha watu hukumu ndiyo unafiki wenyewe. Bado nasimamia palepale, acha unafiki.

mpendwa,

asante sana kwa ufafanuzi wako mzuri. ubarikiwe sana.

ila tuwekane sawa kuwa ninaposema MADAKTARI WAMEWAUA WAPENDWA WETU ninatoa maoni tu na sitoi hukumu! hukumu ni zake Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi na hakika hatimaye atamhukumu kila mtu sawasawa na matendo yake siku aliyoiweka yeye ambayo kila mtu bila kujali elimu na fani yake atajongea kwake na yeye atahukumu kwa HAKI.

suala la Topical kuitetea CCM na serikali yake ni mapenzi yake na bado inabaki kuwa ni maoni yake tu na hilo halimzuii kwa namna yoyote (kama raia mwenye mtazamo huru) kutoa maoni yake juu ya mgomo uliomalizika wa madaktari nchini mwetu na madhara yake.

naamini tuko pamoja sasa

ila nisamehe kama maoni yangu yamekosa kibali machoni mwako. kama wewe ni daktari, usiwakasirikie wagonjwa kwa sababu ya maoni yangu haya, endelea kutimiza wajibu wako na wito ulioitiwa kwa bidii na upendo mwingi huku ukimtukuza Baba yetu aliye mbinguni kwa elimu yako na kipaji chako. pia utakapopata wasaa wa kutubu (kama vile ambavyo sisi sote tunatubu kila siku), usifanye moyo wako kuwa mgumu na Mungu wa rehema atakusamehe hakika.

ubarikiwe sana mpendwa,

Glory to God!
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
mpendwa,

..................................

ila tuwekane sawa kuwa ninaposema ...........................

Glory to God!

Ah! haya bana. Ukiweza fanyia kazi niliyoyasema. Sitapenda kuendelea na mjadala huu kwa kuwa nimekwisha-eleza msimamo wangu.

NB. Mimi si daktari.
 
Madaktari, kumbukeni ya kuwa kila kiungo kina umuhimu wake katika mwili,
wala mwili wote hauwezi kuwa kichwa peke yake, au jicho peke yake.
Hata kile kiungo kidhaniwacho kuwa ni dhaifu kina umuhimu wake.
kwa hiyo hamwezi kusema kuwa sisi ni bora zaidi ya mkulima au mwalimu n.k.
Timizeni wajibu wenu huku mkiendelea kudai haki yenu kwa hekima.
 
Haki haiombwi ila inadaiwa na kupiganiwa...........madaktari wana haki zao na serikali ina wajibu wa kutimiza km wanavyowatimizia marais,wabunge,mawaziri kila wakohoapo
 
Madaktari, kumbukeni ya kuwa kila kiungo kina umuhimu wake katika mwili,
wala mwili wote hauwezi kuwa kichwa peke yake, au jicho peke yake.
Hata kile kiungo kidhaniwacho kuwa ni dhaifu kina umuhimu wake.
kwa hiyo hamwezi kusema kuwa sisi ni bora zaidi ya mkulima au mwalimu n.k.
Timizeni wajibu wenu huku mkiendelea kudai haki zenu kwa hekima.
 
Asiyejua maana haambiwi maana, na hata akiambiwa inaweza isimsaidie kutokana na uelewa wake wa kuchaganua mambo. Iwe ni Madaktari wana makosa au la, LIWALO NA LIWE.
 
Simpendi Antony Lusekelo, ni freemason. Kabla ya mahubiri yake anakuwa kesha piga whisky yakutosha, ulevi anaita upako.
 
Back
Top Bottom