Madaktari wa Muhimbili: This is unprofessional....!

Madaktari wa Muhimbili: This is unprofessional....!

Pole sana mtambuzi,lakini tatizo letu wabongo tunapenda kudanganywa mgonjwa akiambiwa ukweli hatupendi.Pili muhimbili ni hospitali ya kufundishia,kwahiyo huwezi kwepa mgonjwa wako kutumika kama kitabu.
Watu Kama wewe inatakiwa uundwe Mkoa mpya(Lalaland)kwa ajili yenu.
Suala la Work Ethics halina wabongo kupenda kudanganywa wala nini,kuna mambo ambayo unaweza kushabikia Kama mechi za mpira lakini sio suala la Afya na matibabu ya binadamu.

Hata Kama Muhimbili ni hospitali ya kufundishia,bado haiwapi uhuru wa kisheria au wa lazima kutoa hayo mafunzo mbele ya Mgonjwa bila ridhaa (Consent) yake. Ni rahisi Kwako kuona ni sawa kwa hayo ulioyoandika hapo juu kwa kuwa huyo Mgonjwa sio Mama yako wala hana uhusiano na wewe. Wewe inaelekea ni wale mnaoenda kutibiwa Apollo ukipata mafua,ndio maana shida na karaha za Mtanzania wa kawaida hazikugusi.
 
Kama ndio hivyo basi yamefanyika makosa makubwa haya:

1. Kutokumpa mgonjwa opportunity ya kuopt out kutumika katika kufundisha wanafunzi. Hii ni haki ya mgonjwa kuamua kama yuko tayari kutumiwa kimasomo au la.

2. Mgonjwa kutojulishwa taarifa ya hali yake mapema. Majibu ya mgonjwa yakipatikana tu ni wajibu wa daktari kumjulihsa mgonjwa juu ya majibu hayo mapema iwezekanavyo.

3. Kupita round na wanafunzi mbele ya ndugu za mgonjwa. Kunaweza kuwa na mambo ambayo mgonjwa hataki ndugu zake wajue. Kuzungumza kuhusu afya ya mgonjwa mbele ya watu ambao si wahudumu wa afya wanaomhudumia ni kosa la kimaadili unless mgonjwa mwenyewe atoe ruhusu.

4.Kutoa taarifa mpya kwa watu wengine (wanafunzi) mbele ya mgonjwa bila kumshirikisha mgonjwa.

Watanzania huwa tunapenda sana kukesha tukiwalaumu wanasiasa, lakini inatakiwa ifike mahali tujiangalie kila mmoja katika kazi yake, je anaifanya kwa ufanisi???
mkuu umejibu vyema sana ila naomba nikwambie matatizo yanayozaa haya yote hapo juu.kwa kufuata maswali ambayo nimeyaibua kwenye hoja zako.
1) swala hili kwa sisi wagonjwa ama ndugu tunaouguza hapo muhimbili ni tatizo sana. mwaka huu mwezi wa kwanza nilimuuguza ndugu yangu hapo muhimbili wodi ya watoto..............huwezi kuamini mm nilikuwa wa kwanza kukataa mwanangu asiwe modo and nilisema with support ya proffesinoal code of conduct kwamba sitak awe modo. na nikawaambia sababua gani sitaki, kwanza nilisema haitomsaidia mwanangu chochote kile zaid ya kumdhalilisha tu mbele ya madaktari. pia kwa uzoefu wangu mgonjwa anayetumika kama modo anatakiwa apewe chumba ambacho kitakuwa na privacy ya kutosha sasa kwenye public wodi namna hii mtoto aanze kupekuliwa na kutamkiwa maneno siafiki kabisa ni kimyume kabisa na sheria za uuguzi. tatu mgonjwa anapokuwa modo haimaanish kwamba ndio anapate huduma bora kuliko wengine so to me ni bora akawa mgonjwa anaangaliwa na daktari wake za zamu tu.

2) mawasiliano kati ya mgonjwa na tabibu wake sio mazuri kabisa hasa hosp zetu hizi na zaid hapo muhimbili. thankas God hawa watu nimekuwa nikifanya nao kazi ka karibu kwa kaisi cha kuwa wawazi kwangu ila nimeona mapungufu hayo kwa wagonjwa wengine. Dr hawi muwazi kwa mgonjwa juu ya ugnjwa wake, na yuko tayari kumweleza mwanafunzi wa intern kabla hata ya mgonjwa mwenyewe.huu ni ukiukwaji wa maadili na haki za mgonjwa. mtu pekee anayepaswa kujua mgojwa anaumwa nini ni dr na mgonjwa kabla hata ya ndugu zake.
inapendeza zaid mgojwa akashirikishwa kwenye maamuzi juu ya ugojwa wake na hii itamfanya dr amuuguze mgonjwa kwa raha na uhuru zaid.

3) nashangaa sana kwann hawa mdaktari walipita round mbele ya ndugu wa mgonjwa???????? kwakweli kama mgonjwa ni mtu mzima sio mtoto hatakiwi relative kuwepo kabisa wakati wa round nashangaa kwann hawa ndugu wa Mtambuzi walikuwepo sijui waliwezaje kwanza. na hili kosa litakuja kuwagharimu sana madaktari na wauguzi wasipokuwa makini nalo. suppose unasema yupo katika terminal stage kisha ndugu wakaskia mmoja akadodoka kwa panic ama akaanza kulia wodini hapo utafanyaje?? huu ni uzembe sana sana.

4) hili ni kosa la kufunguliwa mashtaka kabisa. ila madaktari wetu huwa wanadharau wagonjwa wao na kuona kana kwamba haajui ama hawaelewi kumbe wegine hata kama sio madaktari lkn ni wauguzi ama ni watu wanaofaya kazi nao kwa karibu pasi kujua.

ushaui wangu madaktari na wauguzi wawe makini katika kufuata maadili ya kazi zao, wasione kana kwamba wapo juu ya wagonjwa wao, pia wajue kwamba wanalipwa mshahara kwa kazi hiyo. kama umeona clinical dr inakuzeveza basi njoo kwenye community medicine uwe mtafiti.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana Mkuu kwa kweli inauma sana wanamfanya mgonjwa ni darasa halafu huenda hata tiba yenyewe hapati wanamfanya aumie zaidi. Kama Madaktari Muhimbili huwa wanasoma hapa JF wafanye marekebisho kuhusu hili, muhimu sana!!!
 
pole mkuu ila huyu ungekuwa ume mrekodi tungeenda mahakamani tumfungulie kesi haraka iwezekanavyo
 
Mtambuzi pole sana, wanaacha kumkomoa Kikwete na CCM yake, wanatukomoa sisi ambao hatuna uwezo hata wa kulipia hospitali kama ya Aga Khan.
Waganga wa kienyeji nao feki ile mbaya,
waombeaji nao wamekuwa magumashi ile mbaya.
Sijui tukimbilie wapi ili tupone.
Na wakati huohuo kila tunachokula na tunywacho tunaambiwa eti ni sumu.
Duhh

Bujibuji unajua wewe ni chizi? Umeongea point sana ila jinsi ulivyoiandika nimejikuta nikicheka bila kutarajia. Hapa watu wananishangaa
 
Last edited by a moderator:
Pole sana mtambuzi,lakini tatizo letu wabongo tunapenda kudanganywa mgonjwa akiambiwa ukweli hatupendi.Pili muhimbili ni hospitali ya kufundishia,kwahiyo huwezi kwepa mgonjwa wako kutumika kama kitabu.

walimueleza mgonjwa? Unadhani ni sahihi mgonjwa kujua hali yake kwa staili hiyo?

Pia utamtumiaje mhinjwa kama darasa bila idhini yake? Na watu kama nyie mnajaribu kahalalisha hilo?
 
Pole kwa kuuguliwa. Hapo Daktari alikosea kabisa kwanza kupita round mkiwa wodini ni kosa kubwa sana na hilo la kusema hali ya mgonjwa ni pacha ya kosa la kwanza.
 
Tatizo sio kuwashtaki mkuu. Tatizo ni unawashtakia kwa nani???? Kuna sekta nyingi sana Tanzania zinatakiwa kuvunjwa na kuundwa upya ikiwepo hii ya Afya. Hao Madaktari kutokuwa weledi ni tatizo kubwa sana. Nilishawahi kumpeleka Wife kwa Daktari mmoja wa wanawake(Gyno) kwa check up ya kawaida kwa akina mama. Baada ya kuingia kwa Dr. Akaanza kueleza matatizo ya mgonjwa aliyetoka kumuona,yaani aliyekuwa mbele kwenye foleni kabla ya Wife. Alikuwa anaeleza vitu personal sana mpaka Wife aliponielezea nilichanganyikiwa. Halafu cha kushangaza Huyo Dr. Alikuwa ni mwanamke. Kwa hiyo Ina maana hata Issue za Mke wangu alimuelezea huyo anayefuata. Ethics Zero kabisa.

Pole sana Mtambuzi na familia kwa kuuguliwa na Mama.

Duuh, madaktari wengine bwana, where is the so called privacy ya mgonjwa? Ikifika jioni si watu wote tunajua matatizo ya wagonjwa walioenda kumuona huyo daktari?

Niliwahi kupeleka mtoto hospitali moja DSM, of course mtoto alikuwa na matatizo ambayo hata mie mama mzazi nilikuwa nalia kila siku. Huyo daktari aliitaje madaktari wote wa watoto hapo hospitalini? Chumba kilijaaje hao madaktari na mishangao ya oooh, we are very sorry...aah poor kid...and the blaah blaah... Sijui nilitoa ujasiri wapi wa kutulia na kuendelea kuwasikiliza, manake kilichokua kichwani ni kunyakua mtoto wangu na kutoka nje.....
 
vyuo vya kina kigwangwala. Unaweza kuropoka chochote hata kwa mgonjwa wako, 'nilikutibu kichaa wewe'
 
Pole sana mkuu.

Ni kweli kabisa kitendo kilichofanywa na hao madaktari siyo cha kiungwana lakini na wewe haukupaswa kususa.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Mkuu Sumu hata ingekuwa mie ningesusa na kumtoa mgonjwa wangu wodini. Kuna faida gani kuchukua vipimo vya mgonjwa na wasirudishe majibu? Sasa mgonjwa anatibiwa vipi? Atapona kwa kulala tu kitandani? Kama ni kitanda hata nyumbani kipo na chaweza kuwa comfortable zaidi!
 
Last edited by a moderator:
Kama ndio hivyo basi yamefanyika makosa makubwa haya:

1. Kutokumpa mgonjwa opportunity ya kuopt out kutumika katika kufundisha wanafunzi. Hii ni haki ya mgonjwa kuamua kama yuko tayari kutumiwa kimasomo au la.

2. Mgonjwa kutojulishwa taarifa ya hali yake mapema. Majibu ya mgonjwa yakipatikana tu ni wajibu wa daktari kumjulihsa mgonjwa juu ya majibu hayo mapema iwezekanavyo.

3. Kupita round na wanafunzi mbele ya ndugu za mgonjwa. Kunaweza kuwa na mambo ambayo mgonjwa hataki ndugu zake wajue. Kuzungumza kuhusu afya ya mgonjwa mbele ya watu ambao si wahudumu wa afya wanaomhudumia ni kosa la kimaadili unless mgonjwa mwenyewe atoe ruhusu.

4.Kutoa taarifa mpya kwa watu wengine (wanafunzi) mbele ya mgonjwa bila kumshirikisha mgonjwa.

Watanzania huwa tunapenda sana kukesha tukiwalaumu wanasiasa, lakini inatakiwa ifike mahali tujiangalie kila mmoja katika kazi yake, je anaifanya kwa ufanisi???
ZeMarcopolo hii ndio thread unayopashwa kuchangia sio kulamba matapishi ya wanasiasa unadharirisha ilimu yako. Nimekupa like ukiendelea kulamba matapishi ya wanasiasa na kukubali malipo ya nape kukaa online 24hrs kuandika ujinga na hii like nitaitoa
 
Last edited by a moderator:
Me naomba kwanza nikupe pole kwa kuuguza na pia kwa yaliyotokea,labda niseme kwamba MNH imekuwa teaching hospital tangu enzi hizo,utaratibu unaotumika katika kuomba ridhaa ya mgonjwa ili aweze kutumika kufundishia wanafunzi ni VERBAL CONSENT na sio WRITTEN CONSENT ,Jambo lingine kipindi cha ward round relatives huwa wanatolewa nje na baada ya round kama kuna maelekezo yoyote hapo ndipo ndugu huitwa na kupewa hivyo naomba niwe mgumu kuamini kama ward round ilifanyika huku ndugu wakiwemo na pia haiwezekani Daktari akatoka tu from nowhere na kuanza kumtumia mgonjwa bila kuestablish rappot
 
Mtambuzi (Baba Ngina) pole sana.
Itabidi utafute daktari mmoja akupe ushauri kuhusu mgonjwa,
(Miaka 70 siyo ya mtu kufa Mtambuzi) jitahidi apate matibabu.
 
Last edited by a moderator:
Mmmmh..Pole mkuu.Nasikiaga ikifikia stage iyo wanaweza kukudunga sindano ya kukurestisha kabisa.
 
Mtambuzi pole sana, wanaacha kumkomoa Kikwete na CCM yake, wanatukomoa sisi ambao hatuna uwezo hata wa kulipia hospitali kama ya Aga Khan.
Waganga wa kienyeji nao feki ile mbaya,
waombeaji nao wamekuwa magumashi ile mbaya.
Sijui tukimbilie wapi ili tupone.
Na wakati huohuo kila tunachokula na tunywacho tunaambiwa eti ni sumu.
Duhh

Ndio tujue kwamba tatizo la Tanzania sio CCM wala Bw.Kikwete, bali ni sisi wenyewe kwa ujumla wetu, Watz wote tuko hivyo kuanzia majumbani mwetu mpaka maofisini na kuendelea, na utashangaa hao madaktari wamo humu kutwa nzima wanamporomoshea matusi Bw.Kikwete na CCM, wakati wao wenyewe wanaua wagonjwa kila siku mahospitalini!

 
Mtambuzi.... Ilianza na walimu sasa ni madaktari, KITAELEWEKA TU

NDIO MATUNDA YA NCHI AMBAYO HATA RAGE, MWIGULU NA LUSINDE WANA THAMANI KULIKO MEDICAL SPECIALIST

POLE
 
Sikatai mgonjwa kutumika kufundishia wanafunzi, hawa ni ndio madaktari wetu wa kesho wakajifunzie wapi. Lakini pale dakatari anapowaambia wanafunzi wake kwamba huyu mgonjwa aliyeko mbele yao yuko katika TERMINAL STAGE huku wanaomuuguza wakiwa karibu na hata mgonjwa mwenyewe akisikia, huu ni uuaji. Daktari huyo aliendelea kuwaonyesha wanafunzi wake dalili zinazothibitisha kuwa mgonjwa wetu yuko kwenye terminal stage.

Pole sana kaka Mtambuzi, kwa kweli kilichofanyika hapo si kitendo cha kiungwana hata kidogo. Kwa kweli naona wame-disturb kwa kiasi kikubwa sana saikolojia ya mgonjwa na ndg zake wa karibu ...
Hili si jambo la kiungwana. Kwa sasa hata kama mnajadiliana namna ya kumsaidia mgonjwa, kwa maelezo ya hao madakatrai mgonjwa anaweza kufikiria vinginevyo kuwa labda mnampangia mipango ya mazishi yake. Mbaya sana.
 
Duuh, madaktari wengine bwana, where is the so called privacy ya mgonjwa? Ikifika jioni si watu wote tunajua matatizo ya wagonjwa walioenda kumuona huyo daktari?

Niliwahi kupeleka mtoto hospitali moja DSM, of course mtoto alikuwa na matatizo ambayo hata mie mama mzazi nilikuwa nalia kila siku. Huyo daktari aliitaje madaktari wote wa watoto hapo hospitalini? Chumba kilijaaje hao madaktari na mishangao ya oooh, we are very sorry...aah poor kid...and the blaah blaah... Sijui nilitoa ujasiri wapi wa kutulia na kuendelea kuwasikiliza, manake kilichokua kichwani ni kunyakua mtoto wangu na kutoka nje.....

Duuuh!! Pole sana Dina.
Wanamfanya mtoto au mgonjwa Kama "freak show". Halafu unakuta na Daktari mwingine casually anasema kwa pembeni "Huyu sidhani Kama atapona warudi nyumbani tu hawa" huku mgonjwa na ndugu zake wakisikia.
Kwa kweli kuwa Mtanzania kunahitaji uvumilivu wa hali ya juu.


BTW nimeikubali hiyo signature yako. Inaweza kuwa na maana nyingi katika maisha ya Mtanzania..that only it you think outside the box...tehe.
 
Back
Top Bottom