Madai au hoja ya janga/baa la njaa nchini iliishia wapi?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Hii nchi ina vichekesho vya kushangaza na sio kufurahisha!

Kuna kipindi kila mwanasiasa na hasa wa upinzani alikuwa akipanda kwenye jukwaa analalamika kuhusu baa la njaa ambalo walikuwa wanadai liko mbioni kulikumba taifa wengine wakaenda mbali zaidi na kumtaka Rais atangaze hali ya hatari.

Thread nyingi hapa Jamiiforums za kuanzia mwezi wa Desemba-Januari 2017 zilijaa hoja kuhusu baa la njaa nchini na athari zake.

Rais Magufuli aliposema, hakuna baa la njaa na akasisitiza yeye ni kiongozi pekee nchini mwenye uwezo wa kujua kama kuna baa la njaa au la. Kauli yake ilikoleza moto kutoka kwa wanasiasa.

Wanasiasa walipanda majukwaani na kudai Rais Magufuli ni kiongozi ambaye ana kiburi na hana huruma na pia hajui anachokisema kwa sababu wao wanawasiliana moja kwa moja na wananchi.

Wengine wakaanza kuja na takwimu za upungufu wa akiba ya taifa ya chakula wakidai haitoshi kutokana na baa la njaa linalokabili taifa.

Kuna baadhi ya wanasiasa wakaenda mbali zaidi na kudai kilichotokea mwaka 1983-85 nchini Ethiopia kuhusu baa la njaa kinainyemelea Tanzania.

Baadhi ya viongozi wa dini ''walinasa'' kwenye mtego wa wanasiasa na kuanza kuimba wimbo ya wanasiasa wakiomba serikali itambue kuwa kuna baa la njaa nchini.

Leo hii hakuna tena hoja ya baa la njaa wala wananchi kufa na njaa lakini kikubwa zaidi, wanasiasa waliotaka kutuaminisha kuna baa la njaa hatuwasikii wakileta mrejesho wa hoja zao.

Siwezi kushangaa kama nikiwasikia tena wanasiasa wakisema, wananchi wamekosa soko la kuuzia mazao yao baada ya uwepo wa mazao mengi nchini!

Madai ya wanasiasa kuhusu uwepo wa baa la njaa yanatoa picha/angalizo gani kama taifa?

Hii inatuambia kuwa tuna wanasiasa nchini ambao ni wanafiki, wapotoshaji, waongo au hawana uhakika wa kile wanachokisema.

Hii pia inatoa angalizo kwa serikali kuwa makini kwa kila hoja au madai yanayotolewa na wanansiasa.

Kikubwa zaidi, Madai ya wanasiasa hasa wa upinzani yanampa Rais Magufuli ''ruhusa'' ya kutosikiliza kinachodaiwa na wanasiasa.

Baadhi ya Thread/Mada kuhusu baa la njaa nchini zilizoanzishwa mwezi Dec-Jan 2017;

LINK>>>Ukame umetamalaki sasa, nchi inaelekea kwenye baa la njaa

LINK>>>Taarifa za serikali juu ya baa la njaa nchini zinajikanganya

LINK>>>Baa la njaa na ukame: KKKT waonya upungufu wa chakula nchini

LINK>>>Baa la njaa na ukame: Kanisa Katoliki lawataka waumini kufunga na kuomba mvua

LINK>>>Baa la njaa: Bei za vyakula hazikamatiki, watu washindia maembe
 
Kati ya vilivyonishangaza katika awamu ya mzee wa chato ni hili la njaa.

Kwa nini ameleta mahindi ya msaada( japokuwa anatuuzia kilo kwa 1000/=).

Ilihalu alikataa kuwa hakuna njaa, lakini baada ya kuanza kuvuna ndo kayaleta!
 
Nadhani tumeishashiba saivi tunapiga miayo tu. Mavuno bwerere.
Mkuu;

Tuliambiwa na baadhi ya wanasiasa kuna ukame na baa la njaa!

Mimi nilidhani hamtofika hata kwenye msimu wa mavuno achilia mbali kupata chakula mpaka mkashiba na kupiga miayo ya shibe!
 
CCM ITATAWALA MILELE..NAANZA HATA KUONA UMUHIMU WA KURUDI KWA CHAMA KIMOJA ..Kama wananchi walivyotaka kipindi wanahojiwa juu ya hili.
 
Hahaha....hakukuwepo na njaa.

Kilichokuwepo ni kikundi tu cha watu wachache ambao ni kama wafa maji.

Mfa maji hata akiona kijikaratasi ataking'ang'ania kwa matumaini ya kwamba labda kitamwokoa asife maji.

Hata huko Marekani tunaona wafa maji wanavyohaha kubuni na kuzua 'fake news' dhidi ya Rais Trump.

Jana tu wamezua jingine eti mke wa rais wa Poland alikataa kumsalimia kwa kumshika mkono Trump, jambo ambalo ni uongo mtupu.

Video za tukio zimewaumbua vile ambavyo hao watangaza njaa walivyoumbuka.

Hawa wafamaji wetu ni watu wa kudandia matukio wakiwa na matumaini ya kunufaika nayo kisiasa.

Umeona wapi wanaotangaza njaa wana vitambi?

Ukiwauliza mara yao ya mwisho kula ilikuwa lini, wanabaki kucheua tu kama nguruwe!

Ilikuwa ni kutapatapa kwa wafa maji tu.
 
Hahaha....hakukuwepo na njaa.

Kilichokuwepo ni kikundi tu cha watu wachache ambao ni kama wafa maji.

Mfa maji hata akiona kijikaratasi ataking'ang'ania kwa matumaini ya kwamba labda kitamwokoa asife maji.

Hata huko Marekani tunaona wafa maji wanavyohaha kubuni na kuzua 'fake news' dhidi ya Rais Trump.

Jana tu wamezua jingine eti mke wa rais wa Poland alikataa kumsalimia kwa kumshika mkono Trump, jambo ambalo ni uongo mtupu.

Video za tukio zimewaumbua vile ambavyo hao watangaza njaa walivyoumbuka.

Umeona wapi wanaotangaza njaa wana vitambi?

Ukiwauliza mara yao ya mwisho kula ilikuwa lini, wanabaki kucheua tu kama nguruwe!

Ilikuwa ni kutapatapa kwa wafa maji tu.

Ur not informed, tafuta habari, sehemu zenye nja mahindi yaloletwa na mpaka sasa bado yanaletwa cha ajabu ni kuwa sehemu nyingi washaanza kuvuna kwa sasa na hawahitaji tena mahindi ya msaada.

je wanao leta kwa sasa ni yanini na walikataa kuleta mwanzo?
 
Ur not informed, tafuta habari, sehemu zenye nja mahindi yaloletwa na mpaka sasa bado yanaletwa cha ajabu ni kuwa sehemu nyingi washaanza kuvuna kwa sasa na hawahitaji tena mahindi ya msaada.

je wanao leta kwa sasa ni yanini na walikataa kuleta mwanzo?

You're the one who is not informed.

A low information fanboy.

Might as well get some pompoms and bust a move.
 
Kati ya vilivyonishangaza katika awamu ya mzee wa chato ni hili la njaa.

Kwa nini ameleta mahindi ya msaada( japokuwa anatuuzia kilo kwa 1000/=).

Ilihalu alikataa kuwa hakuna njaa, lakini baada ya kuanza kuvuna ndo kayaleta!
Mkuu;

Unajukua maana ya baa la njaa?

Kuwa na njaa ni kawaida ya kibinadamu lakini pia uhaba wa chakula kwa baadhi ya maeneo nchini ni kitu cha kawaida kutokana na mazingira ya hali ya hewa na nyenzo za kilimo.

Kuwa na njaa haina maana kuwa kuna baa la njaa!
 
Mkuu;

Unajukua maana ya baa la njaa?

Kuwa na njaa ni kawaida ya kibinadamu lakini pia uhaba wa chakula kwa baadhi ya maeneo nchini ni kitu cha kawaida kutokana na mazingira ya hali ya hewa na nyenzo za kilimo.

Kuwa na njaa haina maana kuwa kuna baa la njaa!
Ivi umenielewa kweli?
 
Mkuu;

Unajukua maana ya baa la njaa?

Kuwa na njaa ni kawaida ya kibinadamu lakini pia uhaba wa chakula kwa baadhi ya maeneo nchini ni kitu cha kawaida kutokana na mazingira ya hali ya hewa na nyenzo za kilimo.

Kuwa na njaa haina maana kuwa kuna baa la njaa!
1.jana ulisema hakuna tatizo.
2.leo unakuja unasema nataka kutatua hilo.

Ebu unganisha hizo dot mbili kama mtu wa kuelewa utaelewa!
 
Back
Top Bottom