Hiyo mada siioni tena hapa, pengine imeunganishwa na ile kuu ihusuyo Kampeni za CCM.
Mimi nawaomba wahusika mada hii wasiiunganishe huko; kwa sababu ile mada ya mkuu Stuxnet ilihitaji mjadala makini sana kujuwa ni sababu zipi hasa zinawavuta waTanzania kwenye mikutano hiyo ya kampeni.
Ingawa nilikuwa bado sijaisoma ile mada ilizungumzia sababu zipi hasa zilizo wavuta watu; nimjuwavyo mkuu 'Stuxnet' nachelea kusema atakuwa anajigamba sana juu ya kupendwa kwa mgombea wa CCm; pamoja na sera anzo waeleza waTanzania.
Hii ni haki yake kusema; lakini nijuavyo hali ya kisiasa iliyopo nchini wakati huu; ni busara kufanya uchambuzi wa kina kuhusu hali ya mikutano hiyo inavyo onekana kwa picha.
Bila kutaka kuandika kwa kirefu zaidi, maoni yangu ni kwamba hizi nyomi za mikutano ya Samia zingekuwa na maana kama pangekuwepo na mlinganishio na mikutano ya vyama vingine; hususani CHADEMA.
Je wakati huu mikutano ya CHADEMA ingekuwa na hali gani ikilinganishwa na hii ya Samia Sluhu Hassan? Huu ungekuwa ni mlinganisho mzuri wa kutolea uchambuzi makini kuhusu kupendwa kwa Samia Suluhu Hassan na sera zazake; kuliko wapinzani wake wakuu.
Pili, je tunajuwa ni mbinu gani zinazotumika kuwapata waTanzania hawa kwenye mikutano hiyo? Hawa waTanzania wamekuja kwa hiari zao, au kuna njia za chini chini za kuwalazimisha kwenda kwenye mikutano hiyo; ni nini nafasi za viongozi wa mitaa na wengineo katika kuhimiza hata wanachama wasikose kuhudhuria kwenye mikutano hiyo!
Inajulikana hizo ni mbinu zilizo andaliwa hata siku ya uchaguzi kuhakikisha waTanzania wanasukumwa kwenda kupiga kura
Kwa hiyo, ile mada ya mkuu 'Stuxnet' ilitakiwa ijadiliwe kisayansi; tupate na ushahidi halisi ni kipi hasa kinacho tokea huko mitaani kuhusu maandalizi ya mikutano hii na kuhakikisha nyomi kubwa inakuwepo.
Sikuhariri. Naomba radhi kama kuna makosa ya kiuandishi.
Mimi nawaomba wahusika mada hii wasiiunganishe huko; kwa sababu ile mada ya mkuu Stuxnet ilihitaji mjadala makini sana kujuwa ni sababu zipi hasa zinawavuta waTanzania kwenye mikutano hiyo ya kampeni.
Ingawa nilikuwa bado sijaisoma ile mada ilizungumzia sababu zipi hasa zilizo wavuta watu; nimjuwavyo mkuu 'Stuxnet' nachelea kusema atakuwa anajigamba sana juu ya kupendwa kwa mgombea wa CCm; pamoja na sera anzo waeleza waTanzania.
Hii ni haki yake kusema; lakini nijuavyo hali ya kisiasa iliyopo nchini wakati huu; ni busara kufanya uchambuzi wa kina kuhusu hali ya mikutano hiyo inavyo onekana kwa picha.
Bila kutaka kuandika kwa kirefu zaidi, maoni yangu ni kwamba hizi nyomi za mikutano ya Samia zingekuwa na maana kama pangekuwepo na mlinganishio na mikutano ya vyama vingine; hususani CHADEMA.
Je wakati huu mikutano ya CHADEMA ingekuwa na hali gani ikilinganishwa na hii ya Samia Sluhu Hassan? Huu ungekuwa ni mlinganisho mzuri wa kutolea uchambuzi makini kuhusu kupendwa kwa Samia Suluhu Hassan na sera zazake; kuliko wapinzani wake wakuu.
Pili, je tunajuwa ni mbinu gani zinazotumika kuwapata waTanzania hawa kwenye mikutano hiyo? Hawa waTanzania wamekuja kwa hiari zao, au kuna njia za chini chini za kuwalazimisha kwenda kwenye mikutano hiyo; ni nini nafasi za viongozi wa mitaa na wengineo katika kuhimiza hata wanachama wasikose kuhudhuria kwenye mikutano hiyo!
Inajulikana hizo ni mbinu zilizo andaliwa hata siku ya uchaguzi kuhakikisha waTanzania wanasukumwa kwenda kupiga kura
Kwa hiyo, ile mada ya mkuu 'Stuxnet' ilitakiwa ijadiliwe kisayansi; tupate na ushahidi halisi ni kipi hasa kinacho tokea huko mitaani kuhusu maandalizi ya mikutano hii na kuhakikisha nyomi kubwa inakuwepo.
Sikuhariri. Naomba radhi kama kuna makosa ya kiuandishi.