Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Masikitiko makubwa na hisia za kusalitiwa vinatawala maisha ya sasa ya Nahodha "Captain" Patrick Waweru Mwangi, rubani mkongwe wa ndege za biashara nchini Kenya.

Katika simulizi yake ya kusikitisha, nahodha huyo anaeleza kwa masikitiko makubwa jinsi alivyopoteza kila kitu alichokifanyia kazi maisha yake yote.

Maumivu yake yanatokana na ukweli kwamba, licha ya kujitolea kikamilifu kwa miaka 34 kuitunza familia yake na hata kumnusuru mke wake kwa kumfadhili na kumkabidhi mamilioni ya pesa, leo hii ameachwa peke yake, hana makazi, na hana hata senti moja mfukoni.

Kisa hiki cha kusikitisha kilianza wakati rubani huyo alipokuwa akipokea mshahara mnene kutoka kwa mashirika makubwa ya ndege kama vile Kenya Airways.

Kwa sababu ya upendo na uaminifu usio na kifani, Captain Waweru alikuwa akihamisha mshahara wake wote moja kwa moja hadi kwenye akaunti ya benki iliyokuwa inasimamiwa na mke wake.

Kupitia fedha hizo na mikopo mikubwa aliyochukua yeye mwenyewe, walifanikiwa kujenga boma la kifahari na kuanzisha shule kubwa ya kibinafsi katika kaunti ya Kiambu.

Hata hivyo, nyufa katika ndoa yao zilianza kuonekana mnamo mwaka 2016 kufuatia misukosuko ya kikazi iliyomfanya asiruke angani kwa muda.

Mgogoro huo ulizidi zaidi pale alipogundua kuwa mali zote walizochuma pamoja, ikiwemo shule na nyumba yao, zilikuwa zimehamishwa na kusajiliwa chini ya jina la mke wake pekee tangu mwaka 2014 bila yeye kujua.

Baada ya ndoa kuvunjika kabisa, alifukuzwa kwenye jumba lake, akanyimwa haki ya mali hizo, na mke wake akafungua kesi ya talaka huku akidai mali zote ni zake binafsi.
1784474413306.jpg
 
Kujificha au kuzamia "stoway" kwenye chumba cha gurudumu za ndege "Landing Gear Bay" ni moja ya maamuzi hatari zaidi ambayo mtu anaweza kuchukua.
Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia kubwa ya wanaojaribu hupoteza maisha kabla ya kufika safari.

Mara ndege inapopaa, hatari ya kwanza ni kupondwa na matairi yanaporudi ndani. Sehemu hiyo imetengenezwa kubana bila kuacha nafasi, hivyo mwili wa mtu unaweza kubanwa na mfumo mzito wa mitambo "Hydraulics Cylinders".

Ndege inapoendelea kupanda kufika futi 30,000 hadi 40,000, shinikizo la hewa hushuka kwa kasi na kusababisha ukosefu mkubwa wa oksijeni.

Hali hiyo humfanya mtu apoteze fahamu haraka na kupata uharibifu wa ubongo (Hupoxia) au kufa kwa kukosa hewa

Kwa wakati huo huo joto hushuka hadi nyuzi joto hasi 60 (- 60°C).
Baridi hiyo kali inafanya mwili ugande na kupata madhara mabaya yasiyoweza kupona.
Kelele kali za injini pamoja na upepo mkali pia huongeza uharibifu wa kibaiolojia mwilini kwa muda wote wa safari.

Hatari ya mwisho hutokea wakati ndege inapoanza kushuka kwenda kutua.
Milango ya sehemu ya gurudumu hufunguka ghafla ili kutoa gurudumu nje.

Mtu aliyepoteza fahamu au kudhoofika kwa baridi kali na ukosefu wa hewa ya oksijeni hushindwa kujishikilia na huanguka kutoka angani.

Kwa mujibu wa rekodi za Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Marekani, tangu mwaka 1947 kumekuwa na zaidi ya matukio 113 hadi 129 duniani kote ya watu kujificha kwenye chumba cha gurudumu za ndege.

Kati yao zaidi ya watu 86 hadi 100 wamepoteza maisha. Hii inamaanisha kiwango cha vifo ni takriban asilimia 76 hadi 77.

Ni watu 29 tu ndio waliorekodiwa kunusurika, na wengi wao walikuwa kwenye safari fupi ambapo ndege haikupanda hadi umbali wa juu kwenye baridi kali.

Takwimu zinaonyesha kuwa wote waliojaribu walikuwa wanaume, wengi wakiwa vijana chini ya miaka 30.

Zaidi ya asilimia 77 ya matukio yametokea katika viwanja vya ndege vya nchi zinazoendelea au zenye migogoro, hasa barani Afrika na eneo la Caribbean, ambapo vijana hao walikuwa wakijaribu kukimbilia Ulaya au Amerika ya Kaskazini kutafuta maisha bora au usalama.
1784642094070.jpg
 
China inaandaa mradi wake wa kwanza wa kihistoria wa ulinzi wa sayari kwa lengo la kugongesha chombo kwenye gimba "asteroid" inayokaribia Dunia ili kujaribu kuhamisha kwenye njia yake kabla haijaleta hatari.

Mradi huu kabambe unaotarajiwa kuzinduliwa kabla ya mwaka 2030 utahusisha vyombo viwili, ambapo chombo cha kwanza kitachunguza asteroidi hiyo kwa ukaribu na chombo cha pili kitagonga asteroidi hiyo kwa kasi kubwa ya kilomita 9 kwa sekunde ambayo ni sawa na kilomita 32,000 kwa saa.

Tofauti na mradi wa DART wa NASA wa mwaka 2022 uliogongesha mwezi mdogo wa asteroidi, mradi wa China unalenga kubadili mwelekeo wa asteroidi yenyewe kwa uwiano wa sayari ya Dunia na kuchunguza jinsi athari za migongano ya kasi kubwa zinavyobadili muundo wa miamba hiyo.

Mgongano huo utafanyika mamilioni ya kilomita mbali na Dunia hivyo hautaleta hatari yoyote kwa sayari yetu, na matokeo yake yatasaidia kuboresha mikakati ya kimataifa ya ulinzi wa sayari.

Jaribio hili ni sehemu ya mpango mpana wa China wa kujenga mfumo wa ufuatiliaji na tahadhari ya mapema dhidi ya asteroidi hatari, jambo linalothibitisha kuwa ulinzi wa sayari ni sekta ya kipekee ambapo mafanikio ya nchi moja yanaleta faida na usalama kwa wanadamu wote duniani.
1784650311194.jpg
 
Sekta ya anga nchini Tanzania inaomboleza kifo cha Mhandisi Mkongwe wa Matengenezo ya Ndege 𝗘𝗿𝗶𝗰𝗸 𝗡𝘆𝗮𝗯𝘄𝗼𝗿𝗼 𝗠𝘂𝗵𝗮𝗻𝘂𝗸𝗮 aliyefariki tarehe 18 Julai 2026.

Erick alihudumu kwa zaidi ya miaka 45 katika sekta hiyo akianza na Air Tanzania, kisha Light Air Transport Libya, na mwaka 1999 alijiunga na Precision Air ambapo alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo Meneja wa Matengenezo.

Alikuwa na leseni za ndege tofauti zikiwemo ATR, Boeing 737, Cessna Caravan na Hawker, na pia alikuwa mshauri mzuri kwa wahandisi wengi vijana.

Mazishi yake yatafanyika Jumatano, 22 Julai 2026 katika Makaburi ya Kerege, Bagamoyo, baada ya Misa katika Parokia ya Christ the King, Kerege.

Rambirambi ziwafikie familia, ndugu, jamaa, marafiki na jamii yote katika sekta ya anga.

𝗣𝘂𝗺𝘇𝗶𝗸𝗮 𝗸𝘄𝗮 𝗮𝗺𝗮𝗻𝗶
1784704407103.jpg
 
Dhoruba kali ya radi imesababisha hitilafu kubwa katika viwanja vya ndege vya jiji la New York, na kusababisha mamia ya safari za ndege kuahirishwa na maelfu ya abiria kukwama.

Hali hiyo mbaya ya hewa iliyokumba eneo la Kaskazini-Mashariki mwa Marekani ilileta upepo mkali wenye kasi ya zaidi ya maili 75 kwa saa pamoja na mvua kubwa ya mawe.

Hali hiyo imeifanya Mamlaka ya Anga ya Shirikisho (FAA) kusitisha kwa muda shughuli zote za urushaji na utulizaji wa ndege katika viwanja vikuu vya eneo hilo ili kulinda usalama wa abiria na wafanyakazi.

Kutokana na hali hiyo, Uwanja wa Ndege wa LaGuardia umelazimika kufuta zaidi ya robo ya safari zake zote zilizopangwa, huku Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa John F. Kennedy ukikabiliwa na ucheleweshaji wa safari unaofikia wastani wa saa nne.

Uwanja wa Ndege wa Newark Liberty nao haukusalia salama, kwani umerekodi mamia ya safari zilizofutwa huku kukiwa na mrundikano mkubwa wa abiria wanaosubiri huduma.

Kufuatia dharura hii, mashirika makuu ya ndege kama Delta, American, United, na JetBlue yameamua kuwasaidia abiria kwa kuondoa ada za kawaida za kubadilisha tiketi ili kuwawezesha kupanga upya safari zao mtandaoni bila gharama ya ziada.
1784712460495.jpg
 
𝗧𝗘𝗟 𝗔𝗩𝗜𝗩 / 𝗟𝗢𝗡𝗗𝗢𝗡, 𝗝𝘂𝗹𝗮𝗶 2026 - Mamlaka ya usafiri wa anga ya Israel inachunguza uwezekano wa uhujumu wa makusudi baada ya ndege ya tatu ya shirika la Israir kuharibiwa katika Uwanja wa Ndege wa London Luton ndani ya chini ya mwaka mmoja.

Kwa mujibu wa taarifa, wiki iliyopita ndege ya Israir iliharibiwa na gari la kuburuta "aircraft tug" ilipokuwa ikivutwa kabla ya kuruka.

Wizara ya usafiri wa anga ya Israel imesema inashuku uharibifu huo ulifanywa kwa makusudi, kwa “wapinga taifa” na tayari ipo katika mawasiliano na mamlaka husika nchini Uingereza ili kubaini kama hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Israir imeeleza kuwa huu ni tukio la tatu la ndege zake kuharibiwa katika uwanja huo wa Luton ndani ya muda wa chini ya mwaka. Msisitizo huo umeongeza mashaka kuwa matukio hayo si ajali za kawaida.

Mamlaka za Uingereza bado hazijatoa taarifa rasmi kuhusu uchunguzi huo.
1784738971296.jpg
 
China inaandaa mradi wake wa kwanza wa kihistoria wa ulinzi wa sayari kwa lengo la kugongesha chombo kwenye gimba "asteroid" inayokaribia Dunia ili kujaribu kuhamisha kwenye njia yake kabla haijaleta hatari.

Mradi huu kabambe unaotarajiwa kuzinduliwa kabla ya mwaka 2030 utahusisha vyombo viwili, ambapo chombo cha kwanza kitachunguza asteroidi hiyo kwa ukaribu na chombo cha pili kitagonga asteroidi hiyo kwa kasi kubwa ya kilomita 9 kwa sekunde ambayo ni sawa na kilomita 32,000 kwa saa.

Tofauti na mradi wa DART wa NASA wa mwaka 2022 uliogongesha mwezi mdogo wa asteroidi, mradi wa China unalenga kubadili mwelekeo wa asteroidi yenyewe kwa uwiano wa sayari ya Dunia na kuchunguza jinsi athari za migongano ya kasi kubwa zinavyobadili muundo wa miamba hiyo.

Mgongano huo utafanyika mamilioni ya kilomita mbali na Dunia hivyo hautaleta hatari yoyote kwa sayari yetu, na matokeo yake yatasaidia kuboresha mikakati ya kimataifa ya ulinzi wa sayari.

Jaribio hili ni sehemu ya mpango mpana wa China wa kujenga mfumo wa ufuatiliaji na tahadhari ya mapema dhidi ya asteroidi hatari, jambo linalothibitisha kuwa ulinzi wa sayari ni sekta ya kipekee ambapo mafanikio ya nchi moja yanaleta faida na usalama kwa wanadamu wote duniani.View attachment 3634376
Kila nukuu ya takwimu zako hazina shida

Ila umewahi kujiuliza kwanini unapenda kuishi sana..!

Kwanini Nasema hivyo.!? Mtu anayependa kuishi sana Duniani ndio mwenye maono ya marekibisho
 
Kila nukuu ya takwimu zako hazina shida

Ila umewahi kujiuliza kwanini unapenda kuishi sana..!

Kwanini Nasema hivyo.!? Mtu anayependa kuishi sana Duniani ndio mwenye maono ya marekibisho
Umenifikirisha mno🥺 yaani ni kama umeingia nafsini mwangu na kuyaona yaliyomo ndani take🥺🙌🏿🙌🏿🏃🏿
 
𝗘𝗡𝗧𝗘𝗕𝗕𝗘, 𝗨𝗚𝗔𝗡𝗗𝗔, 22 𝗝𝘂𝗹𝗮𝗶 2026 - Shirika la Ndege la Uganda (Uganda Airlines) limeingia mkataba wa kihistoria na kampuni ya Boeing wa kununua ndege nane (08) mpya za kisasa zenye ufanisi mkubwa wa matumizi ya mafuta.

Mkataba huo uliosainiwa katika Maonesho ya Kimataifa ya Anga ya Farnborough 2026 nchini Uingereza, unajumuisha ndege 04 za masafa ya kati aina ya Boeing 737-8 MAX na ndege 04 kubwa za masafa marefu aina ya Boeing 787-9 Dreamliner.

Maonesho hayo ya anga yanafanyika katika kaunti ya Hampshire, Uingereza kuanzia tarehe 20 hadi 24 Julai 2026 ambayo ni moja ya matukio makubwa zaidi duniani ya biashara ya ndege na teknolojia ya ulinzi.

Akizungumzia mkataba huo, uongozi wa Uganda Airlines umesema lengo ni kutatua changamoto ya uhaba wa ndege, kupunguza gharama za uendeshaji kwa asilimia 20 hadi 25, na kupanua mtandao wa safari kutoka vituo 17 vya sasa hadi vituo 32 ndani ya miaka ijayo.

Ndege hizo mpya zinatarajiwa kutumika kuimarisha safari za ndani ya Afrika na kufungua njia mpya za kimataifa kuelekea Mashariki ya Kati, Asia na Ulaya.

Pia shirika hilo linalenga kutumia ndege hizo kuikuza *wanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe na kuufanya kuwa kitovu kikuu cha usafiri wa anga wa kikanda.
1784741094131.jpg
 
𝗙𝗔𝗥𝗡𝗕𝗢𝗥𝗢𝗨𝗚𝗛, 𝗨𝗶𝗻𝗴𝗲𝗿𝗲𝘇𝗮 - Rais wa shirika la ndege la Emirates, Sir Tim Clark, amesema shirika hilo halitapokea kundi la kwanza la ndege 10 za Boeing 777X, akieleza kuwa ucheleweshaji mrefu umefanya ndege hizo zisiwe na manufaa.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Anga ya Farnborough, Sir Tim alisema kundi hilo la kwanza litahitaji marekebisho mengi kiasi kwamba halitakuwa tena la kufaa kwa matumizi.

"Hatutapokea kundi hilo na hivyo ndivyo ilivyo," alisema.
"Kwa mtazamo wetu, wao wajue cha kufanya nazo."

Pia aliongeza kwa mzaha kuwa, ndege hizo "zitakuwa bora zikageuzwa kuwa makopo ya maharagwe ya kuokwa".

Emirates ina jumla ya oda ya ndege 270 za 777X kutoka Boeing, kila moja ikiwa na thamani ya takriban dola milioni 440 au pauni milioni 330, huku ndege ya kwanza ikiwa imetengenezwa mwaka 2019.

Hata hivyo, ucheleweshaji wa mara kwa mara kutokana na mabadiliko ya muundo umesababisha Emirates kusubiri ndege hizo kwa miaka saba bila kuzipokea.

Boeing bado haijatoa taarifa rasmi kuhusu uamuzi huo wa Emirates.
1784741757678.jpg
 
Kuna vitu vitatu,
Maji, Anga, Ukweli katika hamna

Watu wa visiwani tutaishia kupigiana vidiokolo😂
 
Antonov An-124 NDEGE YA PILI KUBWA ZAIDI DUNIANI ILITUA DAR ES SALAAM 🇹🇿🇹🇿 KUONGEZA MAFUTA 🔥🔥🔥🔥💯
1784956523345.jpg
 
Ndege mbili za kivita za Jeshi la Anga la Uingereza (RAF) aina ya Eurofighter Typhoon zilitumwa jana kuifuata na kuisindikiza ndege ya abiria ya Qatar Airways baada ya kupoteza mawasiliano na waongozaji wa ndege.

Ndege hiyo ya Qatar Airways aina ya Boeing 777, iliyokuwa ikitokea Doha kuelekea Manchester, ilipoteza mawasiliano ghafla wakati ikiingia kwenye anga ya Uingereza na kusababisha tahadhari ya usalama wa anga.

Ndege hizo za kivita ziliondoka kwa kasi kutoka kituo cha RAF Coningsby na kuipata ndege hiyo ya abiria karibu na eneo la Nottingham ili kuhakikisha usalama wa rubani na abiria.

Mawasiliano ya redio yaliporejea kawaida, ndege za kivita ziliondoka na kuacha ndege hiyo ya abiria iendelee na safari ambapo ilitua salama katika Uwanja wa Ndege wa Manchester majira ya saa mbili usiku, na abiria wote walishuka salama
1784967697903.jpg
 
Back
Top Bottom