Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Ndege binafsi ya Rais Donald Trump aina ya Boeing 757, inayojulikana kama "Trump Force One," imeweka historia kwa kuwa ndege ya kwanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Rais Donald J. Trump uliopo West Palm Beach, Florida, punde tu baada ya uwanja huo kubadilishwa jina rasmi mapema Alhamisi, tarehe 9 Julai 2026.

Safari hiyo fupi ya dakika 30 iliratibiwa maalum ili gurudumu za ndege hiyo ya Kampuni ya Trump yawe ya kwanza kugusa ardhi ya uwanja huo chini ya jina lake jipya, ikiwa imebeba wanafamilia wa Trump pamoja na viongozi wa serikali ya mitaa.

Uwanja huo, ambao zamani ulijulikana kama Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Palm Beach (PBI) na uliopo karibu na hoteli ya Mar-a-Lago, ulibadilishwa jina kupitia sheria iliyopitishwa na bunge la Florida na kuidhinishwa na Gavana Ron DeSantis.
1783683278928.jpg
 
MOSCOW - Chombo huru cha habari cha Astra kimeripoti kuwa ndege za kivita za Urusi zimedondosha kwa bahati mbaya angalau mabomu 334 ndani ya Urusi na katika maeneo ya Ukraine yanayokaliwa na Urusi tangu kuanza kwa uvamizi Februari 2022. Kati ya hayo, mabomu 26 yamedondoka mwaka huu pekee.

Mhariri mkuu wa Astra, Anastasia Chumakova, amesema idadi hiyo ni makadirio ya tahadhari na imejumuisha tu matukio yaliyothibitishwa na vyanzo vya huduma za dharura, mashahidi na ushahidi wa picha.

Uchunguzi unaonyesha kuwa silaha kubwa zinazosababisha matukio hayo ni mabomu ya kuruka kwa kuelekezwa "glide bombs". Mabomu haya huwekewa kifaa maalum kinachoitwa "UMP glide kit" chenye mabawa madogo yanayofunguka baada ya kurushwa, ili bomu liweze kuelea umbali mrefu na kushambulia malengo yakiwa ndani ya anga ya Urusi, mbali na mifumo ya ulinzi wa anga ya Ukraine.

Hata hivyo, wakati mwingine mabawa hayo hushindwa kufunguka.
Ruslan Loyev kutoka kikundi cha uchunguzi "Conflict Intelligence Team" anaamini tatizo linaweza kuwa ni hitilafu katika vilipuzi vidogo vinavyoanzisha mfumo wa chemchemi unaofungua mabawa. Anasema pale kinaposhindwa, bomu hugeuka kuwa bomu la kawaida linaloanguka moja kwa moja badala ya kuruka kuelekea lengo.

Wataalamu wengine wanasema msongo wa kazi pia una mchango.
Mwandishi wa masuala ya ulinzi wa BBC, Pavel Aksyonov, amesema ndege za mabomu zinaporudi kutoka misheni moja na kutumwa mara moja kwenye nyingine bila kupata matengenezo ya kutosha, ubora hupungua na kusababisha makosa mengi.

Kiongozi wa utawala wa Kharkiv, nchini Ukraine, Oleh Syniehubov, amesema Urusi imefanya mashambulizi 473 kwa kutumia mabomu hayo katika eneo hilo tangu mwanzo wa mwaka 2026 hadi Juni 29.

Mabomu yanayodondoka kwa bahati mbaya mara nyingi hayatangazwi rasmi na mamlaka za Urusi, lakini ripoti zinaonyesha yamesababisha vifo, majeruhi na uharibifu mkubwa wa mali.

Wachambuzi wanasema kwa kuwa mabomu ya kuruka kwa kuelekezwa bado ni silaha kuu katika ghala la silaha la Urusi, basi hasara zinazotokana na kudondoka kwa bahati mbaya zitaendelea kuchukuliwa kama sehemu ya gharama ya vita.

@bbcswahili
1783683456255.jpg
 
Mnamo tarehe 9 Julai 2026, helikopta ya Jeshi la Anga la Zambia iliyokuwa imembeba Makamu wa Rais wa nchi hiyo, Dkt. W.K. Mutale Nalumango, ilipata ajali wakati ikipaa katika mji wa mpaka wa Nakonde uliopo Mkoa wa Muchinga wakati wa ziara yake rasmi ya kikazi.

Makamu wa Rais, abiria wote pamoja na wahudumu wa ndege hiyo walinusurika na kutoka wakiwa salama salimini na bila majeraha yoyote.

Kama hatua ya tahadhari, Dkt. Nalumango alipelekwa katika kituo cha afya kilicho karibu kwa uchunguzi wa kawaida wa kitabibu ambapo aliruhusiwa mara moja na anaendelea na ratiba yake ya kazi kama ilivyopangwa huku kukiwa na uharibifu mkubwa wa helikopta hiyo.

Katibu Mkuu wa Baraza la Mawaziri, Patrick K. Kangwa, amepongeza timu ya marubani, waokoaji wa dharura, na wananchi wa Nakonde kwa msaada wao wa haraka, huku mamlaka husika zikianzisha uchunguzi rasmi kubaini chanzo cha ajali hiyo.
1783685364994.jpg
 
Ndege ya abiria ya shirika la Mahan Air kutoka Iran imelazimika kubadili uelekeo na kutua kwa dharura katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hodeidah baada ya njia ya kurukia na kutua ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa ya Sanaa kushambuliwa kijeshi na kuharibiwa vibaya.

Shambulio hilo limefanywa na majeshi ya serikali ya Yemen inayotambuliwa kimataifa kwa lengo mahususi la kuzuia ndege hiyo ya Irani isitue katika uwanja wa Sanaa unaodhibitiwa na waasi wa Houthi, hatua ambayo serikali imesema imekiuka taratibu za kisheria na uhuru wa anga la nchi hiyo.

Baada ya uharibifu huo mkubwa wa miundombinu ya uwanja huo mkuu, Mamlaka Kuu ya Usafiri wa Anga nchini Yemen imetangaza kufungwa kwa viwanja vyote vya ndege nchini humo kwa usalama, huku kukiwa na sintofahamu kufuatia waasi wa Houthi kuizuia ndege ya shirika la Msalaba Mwekundu (ICRC) pamoja na marubani wake waliokuwa kwenye uwanja huo wa Sanaa.
1784027094570.jpg
 
TEHRAN, IRANI - Ndege ya kijeshi ya Urusi ya amri na uratibu wa juu angani aina ya Tu-214PU inayojulikana zaidi kama ndege ya "Doomsday" (siku ya kiyama/Siku ya mwisho) imewasili jijini Tehran huku kukiwa na ongezeko kubwa la joto la kisiasa na kijeshi katika ukanda wa Mashariki ya Kati.

Ndege hiyo maalumu, inayoendeshwa na kikosi maalum cha "Rossiya Special Flight Squadron," iliondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Vnukovo mjini Moscow na kutua moja kwa moja katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Imam Khomeini nchini Irani.

Data za uratibu wa safari za anga zinaonyesha kuwa ndege hiyo, yenye namba za usajili RA-64531 na jina la utambulisho RSD420, iliepuka anga ya nchi jirani na badala yake kupita juu ya Bahari ya Kaspi.

Ndege hii iliundwa kuhimili mazingira hatarishi ya kimesheheni za vita na mifumo thabiti ya mawasiliano ya satelaiti.

Kazi yake kubwa ni kuratibu shughuli za serikali na jeshi wakati wa majanga makubwa au vita kamili.

Kuwasili kwa ndege hii nchini Irani kunajiri wakati kukiwa na uhasama mkubwa wa kijeshi unaozidi kutokota kati ya Marekani na Irani.

Hatua hii imezua hisia na uvumi mkubwa kimataifa kuhusu uwezekano wa kuwepo kwa mipango ya dharura ya kiwango cha juu, kubadilishana taarifa za kiintelijensia, au uratibu wa karibu wa mizozo kati ya Moscow na Tehran.
1784027795782.jpg
 
WASHINGTON- Jeshi la Anga la Marekani (USAF) limethibitisha siku ya tarehe 9 Julai 2026 kuwa ndege mpya ya kivita ya siri aina ya B-21 Raider itarushwa na marubani wawili badala ya mmoja kama ilivyodaiwa awali.

Pamoja na hilo USAF imeanzisha mpango mpya wa kuwafundisha maafisa wa mifumo ya silaha (Weapons System Officers) na maafisa wa mapigano (Combat Systems Officers) kuwa marubani kabla ya kujiunga na vikosi vya B-21.

Jeshi limesema marubani wawili ni bora kwa usalama, ufanisi wa misheni ndefu na kupunguza mzigo wa kazi katika anga yenye adui.

Ingawa B-21 ina teknolojia ya juu ya AI na kiautomatiki, jeshi limebainisha kuwa AI itasaidia tu ila maamuzi muhimu yatabaki kwa binadamu.

B-21 Raider inatengenezwa na Northrop Grumman na inalenga kuchukua nafasi ya B-1B Lancer na B-2 Spirit kwa ajili ya mashambulizi ya masafa marefu.

Siku hiyo USAF ilitangaza pia kituo cha kwanza cha uendeshaji cha B-21.
1784183856861.jpg
 
𝗡𝗘𝗪 𝗬𝗢𝗥𝗞 - Mshawishi mashuhuri wa mitandao ya kijamii kutoka Ghana, Frederick Kumi anayejulikana kama 'Abu Trica', amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa John F. Kennedy mjini New York siku 6 zilizopita akitoka Accra, Ghana, akiwa ndani ya ndege ya Delta Air Lines.

Baada ya ndege hiyo kutua JFK, Abu Trica alitolewa ndani ya ndege chini ya ulinzi mkali wa maafisa wa FBI. Picha za tukio hilo akiwa ndani ya ndege na aliposhuka zimesambaa kwa kasi mtandaoni zikimuonesha akisindikizwa na maafisa hao.

Kufikishwa kwake Marekani kunafuatia uamuzi wa Mahakama Kuu ya Accra nchini Ghana iliyoidhinisha kurejeshwa kwake ili kukabiliana na mashtaka ya uhalifu wa kifedha nchini Marekani.

Abu Trica anashtakiwa na waendesha mashtaka wa shirikisho huko Ohio kwa makosa ya kula njama ya utapeli wa mtandaoni na utakatishaji fedha.

Anadaiwa kuwa sehemu ya mtandao uliotumia akili mnemba (AI) kutengeneza akaunti feki za mapenzi na kuwaibia wazee wa Kimarekani zaidi ya dola milioni nane kati ya mwaka 2023 na 2025.

Kama akipatikana na hatia, anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 gerezani.
Mali zake zote za kifahari ikiwemo magari ya Lamborghini na Cybertruck pamoja na jumba lake la kifahari nchini Ghana ziko hatarini kutaifishwa na serikali.
1784278963127.jpg
 
Back
Top Bottom