Mada maalum: Tuijadili Tanganyika

Mada maalum: Tuijadili Tanganyika

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,928
Reaction score
828,570
Kwa mapana yake
Tulipotoka
Tulipo na tuendako
Tupopatia tulipokosea na tulipoumizwa
Tulipopotea, tulipokengeuka, tuliporubuniwa na tulipojisahau
Tuwajadili pia wazalendo waliojaribu kuipigiania Tanganyika. Timu ile ya G55 original, Rev. Mtikila na Akina Mwabukusi kwa sasa

Tuyajadili kwa undani yale yanayosemwa kwa sasa.. Utawala wa mamluki .. Watu wasio na huruma na Tanganyika yetu.. Na tuhuma zisizosemwa kwa sauti
Tujadili kwa mapana namna wachache kati yetu walivyokubali kuiua Tanganyika kwa kukosa uzalendo na kupokea mafungu ya shekeli za laana
Hii ni mada ya Tanganyika kwa watanganyika.. Kama wewe ni mamluki kaa pembeni tafadhali

Una lolote la kuiambia Tanganyika? Karibu

Ref: Plato: Myth of the cave
Tanzania 50c Uhuru Issue 1962.jpeg
 
Tatizo linaanzia kwenye TAMBIKO KUU, hapa panatakiwa mahesabu makali sana, wazee warudi round table waone, ili sasa Mtanganyika aweze kuzinduka kutoka huko alikozikwa, aamke, ajitambue, ajue thamani ya alivyonavyo na kumiliki, ni hakika atavilinda kwa wivu mkubwa na tutasonga mbele kwa kasi inayoridhisha. Watu wa ule mkoa uliopo baharini watazamwe kwa jicho makini kabla mambo hayajaharibika zaidi.
 
Deni la Taifa limepaa kutoka Trillioni 62 Mwaka 2021 hadi Trillioni 107 Mwaka 2025.

Yaani ndani ya miaka 4 tayari ongezeko la deni limefikia Trillioni 45 sawa na wastani wa Trillioni 11.25 Kila Mwaka

Ngoja tumpe mitano mingine hadi 2030 deni litafika Trillioni 180 🙌
 
Tatizo linaanzia kwenye TAMBIKO KUU, hapa panatakiwa mahesabu makali sana, wazee warudi round table waone, ili sasa Mtanganyika aweze kuzinduka kutoka huko alikozikwa, aamke, ajitambue, ajue thamani ya alivyonavyo na kumiliki, ni hakika atavilinda kwa wivu mkubwa na tutasonga mbele kwa kasi inayoridhisha. Watu wa ule mkoa uliopo baharini watazamwe kwa jicho makini kabla mambo hayajaharibika zaidi.
Lile kafara la kukimbiza moto na yale matambiko ya Bagamoyo, Lindi na ziwa Tanganyika
 
Back
Top Bottom