Chakula ya watu ile
Wadau hebu leo tutoe ya moyoni kuhusu watangazaji wetu wa redio na televisheni.. Ni yupi anayekuboa zaidi kufikia hatua ya kubadilisha hata channel unapomsikia?
Kwa upande wangu ni watangazaji watatu;
Wa kwanza ni huyu mtangazaji wa Redio one wa habari za Magazeti anaitwa Neema Kindole. Daaaah huyu dada usomaji wake unaniboa na kama amekariri maana lazima atumie maneno yaleyale day in day out hana ubunifu kabisa.. Pia kabla ya kusoma magazeti atachukua kama dakika tatu kuelezea wadhamini as if hao wadhamini hawana matangazo yao ya kujielezea... Too pathetic.
Mtangazi wa pili ni huyu wa Clouds Fm anayeitwa Likuda wa kipindi cha Jahazi. Huyu jamaa mpaka leo sijamsoma rika lake yaani ni mtoto, teenager, rika la kati ama mtu mzima.... Maana ana mambo ya kitoto mpaka anaboa.. Nikimsikia akiongea huwa natamani kutapika. Huyu jamaa alifaa awekwe kwenye kipindi cha XXL ama cha watoto Show sio kwenye Jahazi.
Mtangazaji wa tatu anaitwa Amri Masari wa Radio One Sports Show.... Nafikiri huyu mshikaji ni mfano mzuri wa ukanjanja.. Hivi ushawahi kumsikia akiuliza maswali? Too pathetic, maswali ya kitoto kabisa hapa ndipo una miss maswali ya mtu kama Maulid Kitenge ama Alex Lwambano wanauliza maswali ya ukweli bila kupepesa macho..
Maswali maarufu ya Amri Masari;
1. Unauzungumziaje mchezo huu?
2. Safu yenu ya kiungo ilionekana imepwaya?
3. Mmejipangaje na mechi inakuaje?
Too predictable questions..
Wadau zamu yenu kujimwaga sasa....
Mgetofautisha kati ya Reported na Program enchor Sasa Sielewi mtu anaweza vipi kukuboa kwa kuripoti Sekunde 20 ....?Mimi Binafsi sifurahishwi na Noordin msomaji wa taarifa ya Habari Azam Anapqmba saaana maneno misamiati ya kiunguja kukaza sentesi kama anasoma urojo na mbatata
Salum mkambala
Mimi anayeniudhi ni yule Baba anayetokeaga kwenye muvi za Aunty Ezekiel zinapoanza, anapiga makofi kama anaua Mbu na kusema "haki zote zimehifadhiwa"
Lui nda kidemi wa moxh fm
Sam mahela
huwa ananiboa Sana
Hasa anapotaka kujifanya ni Salim kikeke
Huku akibana pua
Mimi ni Joooooooooojiiiiiiiii maraaaaaaatoooooooo wa iiiiiittttttttvvvvvvv taaaaaarrrrrriiiiimmmmmmeeeee ....yani huyu ndo ana PhD ya kuboa