Mada Huru: Ni Mtangazaji yupi anayekuboa zaidi?

Rio Tinto

JF-Expert Member
Sep 18, 2014
777
450
Wadau hebu leo tutoe ya moyoni kuhusu watangazaji wetu wa redio na televisheni.. Ni yupi anayekuboa zaidi kufikia hatua ya kubadilisha hata channel unapomsikia?

Kwa upande wangu ni watangazaji watatu;

Wa kwanza ni huyu mtangazaji wa Redio one wa habari za Magazeti anaitwa Neema Kindole. Daaaah huyu dada usomaji wake unaniboa na kama amekariri maana lazima atumie maneno yaleyale day in day out hana ubunifu kabisa.. Pia kabla ya kusoma magazeti atachukua kama dakika tatu kuelezea wadhamini as if hao wadhamini hawana matangazo yao ya kujielezea... Too pathetic.

Mtangazi wa pili ni huyu wa Clouds Fm anayeitwa Likuda wa kipindi cha Jahazi. Huyu jamaa mpaka leo sijamsoma rika lake yaani ni mtoto, teenager, rika la kati ama mtu mzima.... Maana ana mambo ya kitoto mpaka anaboa.. Nikimsikia akiongea huwa natamani kutapika. Huyu jamaa alifaa awekwe kwenye kipindi cha XXL ama cha watoto Show sio kwenye Jahazi.

Mtangazaji wa tatu anaitwa Amri Masari wa Radio One Sports Show.... Nafikiri huyu mshikaji ni mfano mzuri wa ukanjanja.. Hivi ushawahi kumsikia akiuliza maswali? Too pathetic, maswali ya kitoto kabisa hapa ndipo una miss maswali ya mtu kama Maulid Kitenge ama Alex Lwambano wanauliza maswali ya ukweli bila kupepesa macho..

Maswali maarufu ya Amri Masari;

1. Unauzungumziaje mchezo huu?
2. Safu yenu ya kiungo ilionekana imepwaya?
3. Mmejipangaje na mechi inakuaje?

Too predictable questions..

Wadau zamu yenu kujimwaga sasa....
 
Clouds Fm inasikilizwa na watoto/ watu wa mjini mjini ndiyo wanawaelewa lakini wewe wa gongo LA mboto utabaki ukililia tu kwenye mitandao nq radio one inasikilizwa sana sana na watu wa vijijini!
 
Back
Top Bottom