Machinga na wafanyabiashara wa Tanzania jifunzeni kufanya biashara mtandaoni, tumieni 'smartphones' zenu vizuri

Hii mbona imejibiwa hapa chini soma vizuri Biashara za mtandaoni zinafanyika Duniani kote kwa nini Tanzania iwengumu?
 
Kiatu Cha elfu Saba utumie gharama za kuconfirm Kisha atoe au ikiwa kiatu hakijakutisha Tena sijui afanyaje Yani huu shauri ni mzuri ila mzee it doesn't apply kwa hizi biashara za faida ya elfu moja
 
Hii ni kweli kabisa halafu angalia faida anayotafuta unakuta ni elfu moja hizi gharama za internet na nyingine za kufuatilia consignment mpaka ufike stage ya confirmation anazilipa Nani? Hapo kiatu ambacho ilipaswa kununua 20 utanunua 25 au 27 sasa Shana nzima ya machinga itaondoka.

Halafu kumbuka machinga halipi Kodi, ukishaweka mfumo rasmi hapo lazima akatwe Kodi so unaweka 27,000+18% ndio bei ya kiatu, sasa si Bora nikanunue dukani tu usumbufu wote wa nini?

In short, kuna biashara ambazo huwezi kuziweka kwenye mfumo fulani sababu ukiweka tu unaondoa Shana nzima ya namna ya kujifanya hiyo biashara ili upate faida na mteja apate bidhaa kwa bei ndogo.
 
Kiatu Cha elfu Saba utumie gharama za kuconfirm Kisha atoe au ikiwa kiatu hakijakutisha Tena sijui afanyaje Yani huu shauri ni mzuri ila mzee it doesn't apply kwa hizi biashara za faida ya elfu moja
Tayari inafanyika mkuu sema kiwango kidogo sana ukisema it does not apply unakosea
 
Tayari inafanyika mkuu sema kiwango kidogo sana ukisema it does not apply unakosea
Well, nimekosea kusema it doesn't apply, nadhani neno sahihi no kwamba it is difficult. Anyway wanaofanya wanaelewa ugumu wake aisee. Biashara ya machinga uchague kitu mtandaoni utafurahi utakutana na mdebwedo hutaamini.

Hizi za kwenye eBay zenyewe pamoja za kuaminika Ila unakutana na mzigo tofauti na ulivyochagua wakati mwingine sembuse nyumba au bidhaa ya Mchina mzee😃😃
 
Mkuu usiogope nfumo kabla ya kutumia kipindi cha nyuma kabla ya Uba watu walikuwa wantumia tx kwa gharama kubwa sana by that time mtu ungemwambia habari uba asingekuelewa kabisa pili kwenye platform anayelipa kodi ni mnunuzi sio muuzaji na gharama zinapungua kulingana wingi wa manunuzi watu au jamii itavyotumia hizo platform
 
kitu cha 1,000 uuze mtadaoni kweli, em jarib kua realistic achana na umotiveshen spika
Ajaribu kuwa realistic pia, bidhaa wanazouza machinga zina upekee upo hadi auze mtandaoni? Bidhaa wanazouza machina nyingi zinapatikana katika maduka ya mangi.

Bidhaa ambazo kibongo bongo tunanunua mtandaoni zinatakiwa ziwe worth your time maana lazima uisubiri na lazima uilipie nauli.

Ukitaka kujua sio realistic kwa maisha yetu angalia walioanzisha magenge ya mboga mboga online, ni aina ya biashara iliyofeli kabla haijaanza unless targeted costumer wako wawe kwenye mitaa fulani hivi ya mageti tupu.
 
Kama ni mnunuzi sasa unadhani Nani anataka anunue kwa bei kubwa? So you see my point? Usiangalie mauzo ya vitu eBay hapa tunaongelea machinga anayeuza vibanio vya Mia tano na ana mtaji wa elfu ishirini au anauza jeans ya mtumba ya 7000.

Binafsi nakuelewa sana Ila wasiwasi wangu ni namna ambayo machinga tunayemuita machinga kuweza kutumia huo mfumo na kuuza kwa bei za kimachinga.

Kuhusu Uber kwakweli wao wameimplement utaratibu ambao tulikuwa tunaupigia kelele sema wameenda mbali kwa kuweka platform ya kuita taxi kwa mtandao tu Ila miaka mingi sana tulikuwa tunataka wafunge mita kama za New York taxi au London taxi so hii imerahisisha zaidi ni Jambo lisilopingika Ila hapa tunaongelea aina ya biashara tofauti kabisa na ya machinga.
 
Ukipokea mzigo halafu usiconfirm?
 
Ukitumiwa mzigo tofauti kuna option kwenye platform za public unaweza fungua dispute badala ya ku-confirm ,Admin kazi yake kulinda platform yake isichafuliwe na watu wachache wenye nia ovu

pia ni muhumu kusoma vizuri policy kabla ya kutumia platform iliujue ikitokea udanganyifu itakuwaje binasi nimetumia sana naelewa vizuri tubadilike Dunia imetuacha ambali sana.

eBay ni worldwide ukipata changamoto imekula kwako,mimi na zunguzia hapa kwetu.

Kunafaida nyingisana tutazipata kama Taifa tukiunga mkona platform zetu za ndani kuna nchi jirani wanategemea sana bidhaa zetu kutoka hapa kwetu tanzania watu wasafiri kutoka Zambia Congo au Zomabwe Malawi Burundi wapanda basi kuja hapa kununa bidhaa na kwenda kuziuza kwao ni wazi kunatatizo kama bidhaa zetu tungezitangaza watu wengi wangepata fursa ya kuziona na baadhi wangeuza nakuongeza kipato cha mtu moja na Taifa kwaujumla.
 
Nimekuelewa kote, lakini nami nimeishi nchi kadhaa ndio maana ulipoanza kuongelea kuuza bidhaa Zambia, Congo nk hapo ndipo umetoka kwenye dhana nzima ya platform kwa wamachinga.

Kama unaongelea platform za ndani za kuuza bidhaa nje na kwingine hiyo sio tatizo kabisa Ila kama utaongelea machinga anayeuza viatu mfano ana pea nne anaziweka mtandaoni auze hiyo ni tofauti sana na ndio nachokiongelea.

Ukimtaja machinga unamtaja road side seller ambae anakuwa na bidhaa mkononi au ana kigenge anauza charger kama kumi za simu, viredio vya kichina nk. Huyu ndiye nayemuongelea Mimi.

So, kama unaongelea platform hizi za ndani kwetu kuuza bidhaa kwa level hiyo unayosema basi usiwataje machinga aisee hapo unaongelea mtu mwenye mtaji mkubwa kidogo hata kama wa milioni tano which nakubaliana nawe kwamba hao ni vema wakatumia hizi platform zetu.

Hata hivyo ni jukumu la wenye hizi platforms kujitangaza ili wauzaji na wanunuzi wazijue pia, unaweza kulaumu watu kutozitumia kumbe sababu ni anayetengeza platform hazitangazi na kufundiaha watu namna ya kuzitumia ku-upload matangazo yao.

Inabidi kufahamu kwamba wengi wa wafanyabiashara wetu sio watu walioenda shule hivyo basi huwa ni wahuni sana kukubali kufanya biashara kwa kuadopt new techniques.
 
Yes, kabisa kikubwa watumie tu mifumo iliyozoeleka
 
Ukipokea mzigo halafu usiconfirm?
Kuna Policy inabidi usome vizuri kabla ya kutumia Platfom kuna makubaliano kati ya mnunuzi na muuzaji

Adimn ana access ya kusama na kuona mawasiliano/ makubalino yao kati ya mnunuzi na muzaji pia Adimin anaweza kuwasiliananao wote ikitokea biashara kuingia kwenye utata au moja kafungua kesi kwake, pia admin anauwezo waku mlipa muzaji akingudua mnunuzi ni mtata kavunja sheri za Platform .
 
Yes, kabisa kikubwa watumie tu mifumo iliyozoeleka
Kosa kubwa sana ukisema watu watumie platform zilizozoeleka ni kudumaza platform changa na kuondoa ushindani wa bei tusikubali kukariri hivi vitu ushindani na ubunifu kwenye kuuza bidhaa zetu ni muhimu sana ushinadi unaongeza ubunifu na kupunguza bei kwa mtumiaji wa mwisho,
 
Mkuu tusifanye umachinga kama kipaji au kitu kizuri ,mtu kuwa machinga sio sifa au cheo ni ugumu wa maisha nikatika hali ya mtu kuangali jinsi ya kujinasua kwenye umasiki nafikiri tuje na mawazo mazuri ya kuwasaidia watanzania kubadili muelekeo na njia bora za kujiajiri nakujiletea mandeleo
 
Wataweza Bei ya bando, watanzania wengi wanafanya biashara mtandaoni ila ndio hivyo bando wamepandisha kuwakomoa
Bando sio tatizo kwani Fb insta tweta ni bure tatizo wabongo kuwatoa kwenye Fb ningumu sana wanatapeliana kila siku lakini hawasikii kabisa.
 

wajue_matapeli_insta​

wajue matapeli insta​


Jukwaa lakuanika Matapeli wa Instagram,Fanya kuwatag marafiki,kupost kwenye pageyako, kupost instastory ili iwafikie wengi tuwaokoe wengi wastapeliwe

Mwenye akaunti halisi ana followers 243,000/= na jina lake ni @lampard_electronicss Hivyo muwe makini wapendwa,,huyu tunaemmention ndio akaunti halali na halisi na ambayo inatambulika,
Asanteni


Kuna baadhi ya watoa mikopo online ni matapeli, wamemtapeli mtu wangu wa karibu
Sasa mwenye hilo jina kwa nini asishughulike na huyo tapeli haoni anamuharibia biashara

Mimi sipendi kumkamata mtu alafu mkachekea piga ngoa meno maana sheria za kitanzania ni za kukenuliana kenuliana tu. Aisee siku nikikutana na tapeli uwiiiiii uwiiiii nafikiri mimi ndo nitaenda jela yeye akiwa kwenye udongo au hospital majeraha kama yote. Sasa ona huyo karudi mtaani

Tapeli analama gani dada yangu utakunaye wapi kwenye daladala au kwenye wendo kasi?


anagalie kinachoendelea mitandaoni
 

Kwa kweli aiseeee . Maana bado tupo na taifa letu la ajabu kweli kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…