Machinga Complex, Is a failure, Mr President Execute Plan B!

Revolutionary

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
456
86
Moja kati ya Vigezo vikuu vya Miradi ya maendeleo ya Jamii ni ushirikishwaji wa wadau husika. Kushirikishwa kwa wadau kuna faida nyingi ikiwemo, kuleta mchango mkubwa kimawazo kutokana na experience yao kubwa katika eneo hili. Pili ushirikishwaji wa wadau huleta urahisi katika utekelezaji wa mradi husika kwa sababu unajenga ownership, wadau wanajisikia kwamba mradi ni wao tofauti kama hawatahusishwa kabisa.

Mradi wa Machinga complex ni mradi mzuri sana, lakini hali ni ya kusikitisha sasa kwani wamachinga wenyewe wamejiondokea zao wako soko lao la zamani la Karume wanaendeleza mchakato.

Waziri husika suala limemshinda, Rais kuona hivyo anaagiza wadau watafutwe mkutano ufanyike kujua tatizo ni nini? Mtazamo wangu ni kwamba angewashirikisha wadau kabla ya kujenga, haya ya leo yasingetokea. wangeweza kupata mwafaka wa nini kifanyike, leo hii mambo yangekua mazuri.

Kwa sasa nadhani kurudi wamachinga pale mjengoni ni ngumu.

Namshauri Rais na waziri husika ku-execute plan B, ambayo ni kuitisha mkutano na wafanyabiashara wakubwa na potential investors wa kitanzania na wataalamu wa fedha na uchumi ili kuona ushauri wa kiufundi na wanawezaji wa kukodishwa kufanya biashara hapo na nani yuko interested, awasilishe pendekezo lake. hakika najua watu watachangamkia fursa hii na wafanyabiashara watapatikana kufanya biashara kubwakubwa kama supermarkets, butiques, shops nk. Baada ya hapo mjengo ubadilishwe jina, maisha yaendelee kuliko kungojea na kuanza kumtafuta mchawi nani sasa wakati serikali inakosa pesa (implicitly and explicitly) kwa kudororesha economic asset ya mjengo huu.

Wakae vikao na wamachinga kutafuta suluhu mpya shirikishi kuona nini kifanyike! kama ni kujenga mjengo mwingine sehemu itakayokubalikana na wote au la!

Au mwaonaje wadau?

Akhsanteni!
 
go to hell....vizimba ni one square meter. Labda wauze karanga na vitumbua. What are you talking about dude!!!!
 
go to hell....vizimba ni one square meter. Labda wauze karanga na vitumbua. What are you talking about dude!!!!

Haaa haa huo ni ushauri wa bure tu, najua vizimba sio permenent structures jengo laweza kuwa kuwa restructured ndani! why not plan B instead of kukaa na jengo tupu bure bure!
 
Watu wasipotoshe dhumuni la kujengwa majengo yale . ni lengo zuri na daima ni mfano wa kuigwa .
lakini wakitaka ufanisi wa majengo haya ni lazima wayaamishe makaburi pembeni yake na wajenge kituo cha mabasi ya daladala yaendayo mbagala na gongo la mboto nadhani wataona idadi ya watu itavyoongezeka masokoni pale
 
hili nalo neno!

Kweli inabidi kituo kiamishiwe pale, na wadau wangeshirikishwa tangu mwanzo hili lingejulikana mapema.
Watu wasipotoshe dhumuni la kujengwa majengo yale . ni lengo zuri na daima ni mfano wa kuigwa .
lakini wakitaka ufanisi wa majengo haya ni lazima wayaamishe makaburi pembeni yake na wajenge kituo cha mabasi ya daladala yaendayo mbagala na gongo la mboto nadhani wataona idadi ya watu itavyoongezeka masokoni pale
 
Wanajamii nina yafuatayo:
1. Mradi wa Majengo ya Machinga Complex ni failure tupu kweli kwa kuwa " wateja wa wamanchinga wako mitaani. Ni kweli kabisa ulibuniwa kwa maslahi binafsi na sio kwa WAMACHINGA. Ushirikishwaji wa wadau ni muhimu sana. Matokeo yake ni kujenga "White Elephants" za miaka ya 70 na 80. Miradi ya kutokana na hotuba za majukwaa; angalia viwanja vya michezo isiyomalizika kila mkoa. Imegeuzwa kuwa viwanja vya maonyesho!
2. Wateja wa Manchinga ni watu wa kipato cha chini wenye kutegemea daladala, baiskeli, miguu yao na wachache bodaboda ili wafike kwenye masoko. Hivyo "location" ya soko la Machinga sio kwa ajili ya biashsara ndogo ndogo za wamachinga. Usitarajie mtu anayetaka kununua suruali au shati la mtumba la sh. 500. 00 au 1,000.00 kutoka Buguruni, Tabata, Tandika au Tegeta apande daladala mpaka Ilala. Kwa mwenye uwezo wa kufikiri wa kati ni HAIWEZEKANI. Binafsi zaidi ya nguo zangu ni mitumba mipya au karibia mipya hununua maeneo ya mitaa yangu. Situmii nauli yeyote. Na ndio wengi wa watu wa kipato cha chini na cha kati.
3. Ujenzi wa Machinga Complex ulipingana na dhana nzima ya kutanua jiji la Dar kwa kujenga miji midogo ya pembezoni - "satellite cities" za Kibamba - Uluguruni, Pugu, Bunju, Kigamboni na sehemu zingine ili kuhudumia wakaazi wa maeneo hayo badala ya kwenda Ilala.
4. Nini kifanyike? Nakubaliana na na wazo la kuwakabidhi majengo hayo wafanyabiashara wa kati na wakubwa wenye uwezo wa kulipa kodi za pango na kuhudumia usafi wa majengo hayo. Wateje wake ni wenye kumudu kupanda daladala na wenye vipando vyao. Sio wanunjua chupi, soksi na sidiria za mitumba kutoka Marekani na Canada. Mamlaka za Halamshauri za Manispaa husika zikabidhiwe majengo hayo ili waweze kupangisha kwa wahusika na sio Wamanchinga! Na sio Halmashauri ya JIJI. Halmashauri ya JIJI haina walipa kodi wala wapiga kura. Wapo Ilala, Kinondoni na Temeke. Fedha zitakazopatikana zipelekwe kujenga masoka mazuri na madogo kwenye maeneo ya miji mipya ya pembezoni mwa jiji -satellite cities". Iwapo kungekuwa na ushirikishwaji sasa hivi tungekuwa na masoko ya aina hii zaidi ya matano kama yalivyo maghorofa ya Manchinga.
5. Kukusanya wadau husika sio rahisi na ni gharama. Tutumie wataalamu wetu kikamilifu wafanye kazi za kupanga maendeleo ya JIJI letu na sio WANASIASA! Tuwatumie maafisa maendeleo ya jamii (sociologists), wachumi, maafisa mipango miji (town planners), madaktari, wanamazingira na kadhalika. Wanasiasa watoe mapendekezo tu!
Akhsanteni!
 
CCM haina nia ya dhati ya kumkomboa Mtz ndio maana hata miradi inayobuni ni ya kitapeli.
Nssf wametumia mamilioni ya pensheni za watu kwenye mradi wa kijinga.
Jengo lenyewe limejengwa chini ya kiwango, saa hizi nyufa kila kona.
 
Wanajamii nina yafuatayo:
1. Mradi wa Majengo ya Machinga Complex ni failure tupu kweli kwa kuwa " wateja wa wamanchinga wako mitaani. Ni kweli kabisa ulibuniwa kwa maslahi binafsi na sio kwa WAMACHINGA. Ushirikishwaji wa wadau ni muhimu sana. Matokeo yake ni kujenga "White Elephants" za miaka ya 70 na 80. Miradi ya kutokana na hotuba za majukwaa; angalia viwanja vya michezo isiyomalizika kila mkoa. Imegeuzwa kuwa viwanja vya maonyesho!
2. Wateja wa Manchinga ni watu wa kipato cha chini wenye kutegemea daladala, baiskeli, miguu yao na wachache bodaboda ili wafike kwenye masoko. Hivyo "location" ya soko la Machinga sio kwa ajili ya biashsara ndogo ndogo za wamachinga. Usitarajie mtu anayetaka kununua suruali au shati la mtumba la sh. 500. 00 au 1,000.00 kutoka Buguruni, Tabata, Tandika au Tegeta apande daladala mpaka Ilala. Kwa mwenye uwezo wa kufikiri wa kati ni HAIWEZEKANI. Binafsi zaidi ya nguo zangu ni mitumba mipya au karibia mipya hununua maeneo ya mitaa yangu. Situmii nauli yeyote. Na ndio wengi wa watu wa kipato cha chini na cha kati.
3. Ujenzi wa Machinga Complex ulipingana na dhana nzima ya kutanua jiji la Dar kwa kujenga miji midogo ya pembezoni - "satellite cities" za Kibamba - Uluguruni, Pugu, Bunju, Kigamboni na sehemu zingine ili kuhudumia wakaazi wa maeneo hayo badala ya kwenda Ilala.
4. Nini kifanyike? Nakubaliana na na wazo la kuwakabidhi majengo hayo wafanyabiashara wa kati na wakubwa wenye uwezo wa kulipa kodi za pango na kuhudumia usafi wa majengo hayo. Wateje wake ni wenye kumudu kupanda daladala na wenye vipando vyao. Sio wanunjua chupi, soksi na sidiria za mitumba kutoka Marekani na Canada. Mamlaka za Halamshauri za Manispaa husika zikabidhiwe majengo hayo ili waweze kupangisha kwa wahusika na sio Wamanchinga! Na sio Halmashauri ya JIJI. Halmashauri ya JIJI haina walipa kodi wala wapiga kura. Wapo Ilala, Kinondoni na Temeke. Fedha zitakazopatikana zipelekwe kujenga masoka mazuri na madogo kwenye maeneo ya miji mipya ya pembezoni mwa jiji -satellite cities". Iwapo kungekuwa na ushirikishwaji sasa hivi tungekuwa na masoko ya aina hii zaidi ya matano kama yalivyo maghorofa ya Manchinga.
5. Kukusanya wadau husika sio rahisi na ni gharama. Tutumie wataalamu wetu kikamilifu wafanye kazi za kupanga maendeleo ya JIJI letu na sio WANASIASA! Tuwatumie maafisa maendeleo ya jamii (sociologists), wachumi, maafisa mipango miji (town planners), madaktari, wanamazingira na kadhalika. Wanasiasa watoe mapendekezo tu!
Akhsanteni!

sidhani ni wazo zuri la kuwachukulia wanyonge jengo lao na kuwakabidhi wakuu cha msingi ni kuweka vitu vitavyoleta ongezeko la watu kama kuweka kituo cha mabasi au Bank ya NMB kwenye jengo hili ili kuongeza idadi ya watu. wakishindwa basi nadhani ni wakati wa jamii kukaa chini na kutafakali nini cha kufanya katika eneo lile
 
Wanajamii nina yafuatayo:

3. Ujenzi wa Machinga Complex ulipingana na dhana nzima ya kutanua jiji la Dar kwa kujenga miji midogo ya pembezoni - "satellite cities" za Kibamba - Uluguruni, Pugu, Bunju, Kigamboni na sehemu zingine ili kuhudumia wakaazi wa maeneo hayo badala ya kwenda Ilala.

5. Kukusanya wadau husika sio rahisi na ni gharama. Tutumie wataalamu wetu kikamilifu wafanye kazi za kupanga maendeleo ya JIJI letu na sio WANASIASA! Tuwatumie maafisa maendeleo ya jamii (sociologists), wachumi, maafisa mipango miji (town planners), madaktari, wanamazingira na kadhalika. Wanasiasa watoe mapendekezo tu!
Akhsanteni!


Hongera mkuu kwa malelezo yako lakini naomba nitofautiane nawe kidogo kwenye blue.
Nahisi nawe utakuwa mmojawapo wa professinal ulizo zitaja hapo juu suala la satellite town bado ni theory tu unafiki Huko Bunju, Buyuni, Mwanagati, twangoma etc.ndio yangeweza kuwa active swali la kujiuliza ni je huko ndio waliko walala hoi wengi?au ndio utarudi na kusema wame locate kusiko husika?suala la mipango miji sio rahisi kama ufikiriavyo.
Pili nadhani hili suala la soko ilikuwa ni concept ya wanasiasa kwenye kutatua matatizo wapiga kura wao wasomi walikuwapo siku nyingi sina hakika kama walisha wahi propose kitu hiki au wanasubiri wanasiasa?Kwenye hili nanyi taalamu mnabidi kulete idea ambazo zitakuwa msaada kwa matatizo tuliyo nayo sio kusubiri concept maofisi.Sambamba la hilo ujenzi huo ulishilisha wataalamu wa jiji nssf na washauri binafsi je wataalamu wote hawa wote hao hawajui nini kinahitajika? kama ni hivyo basi tuko kwenye hatari kubwa
nihayo tu.
 
Hivi nchi yetu imezama kiasi cha kuanzisha mradi mkubwa wa aina hiyo bila ya kuufanyia kwanza upembuzi yakinifu. Maana ni kwemye hatua hiyo hayo yote yanayozungumzwa sasa yangelionekana. Ikumbukwe wateja wengi wanaonunua bidhaa kutoka kwa wamachinga huwa hawakutokea nyumbani na dhamira ya kununua bidhaa hiyo. Ni kwamba huo wanakutana na watu hao wakati wako kwenye shughuli zao nyingine na wamachinga wanatumia fursa hiyo kuwashawishi kununua bidhaa yao. Sasa unapowatenga wamachinga peke yao unawanyima fursa hiyo. Katika hali hiyo, kilichohitajika ni kuwa na jengo moja linalojumuisha wafanya biashara wakubwa na wadogo.
 
Wanajamii nina yafuatayo:
1. Mradi wa Majengo ya Machinga Complex ni failure tupu kweli kwa kuwa " wateja wa wamanchinga wako mitaani. Ni kweli kabisa ulibuniwa kwa maslahi binafsi na sio kwa WAMACHINGA. Ushirikishwaji wa wadau ni muhimu sana. Matokeo yake ni kujenga "White Elephants" za miaka ya 70 na 80. Miradi ya kutokana na hotuba za majukwaa; angalia viwanja vya michezo isiyomalizika kila mkoa. Imegeuzwa kuwa viwanja vya maonyesho!
2. Wateja wa Manchinga ni watu wa kipato cha chini wenye kutegemea daladala, baiskeli, miguu yao na wachache bodaboda ili wafike kwenye masoko. Hivyo "location" ya soko la Machinga sio kwa ajili ya biashsara ndogo ndogo za wamachinga. Usitarajie mtu anayetaka kununua suruali au shati la mtumba la sh. 500. 00 au 1,000.00 kutoka Buguruni, Tabata, Tandika au Tegeta apande daladala mpaka Ilala. Kwa mwenye uwezo wa kufikiri wa kati ni HAIWEZEKANI. Binafsi zaidi ya nguo zangu ni mitumba mipya au karibia mipya hununua maeneo ya mitaa yangu. Situmii nauli yeyote. Na ndio wengi wa watu wa kipato cha chini na cha kati.
3. Ujenzi wa Machinga Complex ulipingana na dhana nzima ya kutanua jiji la Dar kwa kujenga miji midogo ya pembezoni - "satellite cities" za Kibamba - Uluguruni, Pugu, Bunju, Kigamboni na sehemu zingine ili kuhudumia wakaazi wa maeneo hayo badala ya kwenda Ilala.
4. Nini kifanyike? Nakubaliana na na wazo la kuwakabidhi majengo hayo wafanyabiashara wa kati na wakubwa wenye uwezo wa kulipa kodi za pango na kuhudumia usafi wa majengo hayo. Wateje wake ni wenye kumudu kupanda daladala na wenye vipando vyao. Sio wanunjua chupi, soksi na sidiria za mitumba kutoka Marekani na Canada. Mamlaka za Halamshauri za Manispaa husika zikabidhiwe majengo hayo ili waweze kupangisha kwa wahusika na sio Wamanchinga! Na sio Halmashauri ya JIJI. Halmashauri ya JIJI haina walipa kodi wala wapiga kura. Wapo Ilala, Kinondoni na Temeke. Fedha zitakazopatikana zipelekwe kujenga masoka mazuri na madogo kwenye maeneo ya miji mipya ya pembezoni mwa jiji -satellite cities". Iwapo kungekuwa na ushirikishwaji sasa hivi tungekuwa na masoko ya aina hii zaidi ya matano kama yalivyo maghorofa ya Manchinga.
5. Kukusanya wadau husika sio rahisi na ni gharama. Tutumie wataalamu wetu kikamilifu wafanye kazi za kupanga maendeleo ya JIJI letu na sio WANASIASA! Tuwatumie maafisa maendeleo ya jamii (sociologists), wachumi, maafisa mipango miji (town planners), madaktari, wanamazingira na kadhalika. Wanasiasa watoe mapendekezo tu!
Akhsanteni!

Imetulia, naunga mkono hoja, naona tu toka hapa tunapata mapendekezo mazuri kama haya, hakika wadau hawakuhusishwa ujengaji majengo haya!
 
Waambie mzee! Hata UDOM nyufa kibao!
CCM haina nia ya dhati ya kumkomboa Mtz ndio maana hata miradi inayobuni ni ya kitapeli.
Nssf wametumia mamilioni ya pensheni za watu kwenye mradi wa kijinga.
Jengo lenyewe limejengwa chini ya kiwango, saa hizi nyufa kila kona.
 
Waambie mzee! Hata UDOM nyufa kibao!

Na kwenye kampeni jamaa alisema atajenga zingine 5 na wadanganyika kama kawaida wakapiga makofi kibao. Sisi wengine tulikuwa wazito kidogo kwani tuliona kabisa kwamba he spoke too soon. Matokeo yake sasa ni kichekesho pale kwa kweli I'm told usiku linageuka kuwa dangulo. Hii ni aibu sana kutumia michango yetu ya mabilioni kwa miradi ya kiuwendawazimu kama ile wakati nchi ina matatizo kibao ya kusolve. Jk hayo mengine matano ujenzi unaanza lini ili tupate japo tenda ya kuleta mchanga.
 
GAZETI LA MWANANCHI LEO LINASEMA...................

Hadija Jumanne
IMEELEZWA kuwa viongozi wengi na maofisa wa masoko nchini hawapo kwa ajili ya kusaidia wajasiriamali bali wapo kwa ajili ya maslahi yao hali inayozorotesha ukuaji wa uchumi nchini.
Hayo yalisemwa jana na aliyekuwa Mwenyekiti wa Soko la Mchikichini, Muhusini Kiwasha alipokuwa akizungumzia jengo la Machinga Complex.Alisema serikali serikali imepoteza mabilioni ya fedha kujenga jengo la wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kama Machinga Complex na kuwakabidhi viongozi ambao hawana mbinu za kulifanya soko hilo likubalike.
Kiwasha alisema kuwa hatua hiyo inatokana na kupigwa vita kwa soko hilo la Mchikichini ili soko hilo lihamie kwenye jengo la Machinga Complex.
"Wakati nikiwa mwenyekiti wa Soko la Mchikichini nilipata wakati mgumu wa uendeshaji wa biashara zetu kwani wateja wote walikuwa wanakimbilia kwenye Soko la Ilala" alisema Kiwasha.Alisema anasikitishwa na kitendo cha jiji kuteua Meneja wa Machinga Complex, kusimamia soko hilo na tangu apewe madaraka amekuwa akilipiga vita Soko la Mchikichini.
Alisema wakati jengo hilo linajengwa waliambiwa kuwa halitakuwa na uhusiano na lile la Mchikichini lakini wanashangaa kuona likipigwa vita sasa.
Hata hivyo alisema Meneja wa Soko la Machinga Complex amepewa kazi asiyoiweza na kwamba ipo haja kwa aliueteuliwa kuangalia kama kazi imekuwa ngumu ni heri awaachie wengine kuliko kufikiria kuvunjwa kwa Soko la Mchikichini.




.......HAINA USHABIKI WALA NINI, CCM SIO CHOMBO CHA KUTUPELEKA SALAMA WATANZANIA TUNAKOTAKA KWENDA! KINYUME NA HAPO NI NDOTO!
 
KUFA KWA MACHINGA COMPLEX!
1. Hakukuwa na nia ya dhati kulijenga jengo hili
2.Mafisadi walichakachua ujenzi wake
3 Wadau hawakushirikishwa kuplan
4. Ilifanyika hivi makusudi ili machinga wakimbie wao wachukue
5. Wanasubiri machinga wakishindwa kabisa wapeane mafisadi
6. Muda si mrefu litachakachuliwa

Sera Mbovu za chama chao!
Mipango bomu ya chama chao!
Ufisadi wa chama chao!
Uchakachuaji wa chama chao!

WAJIVUE MAGAMBA YOTE HAYA!
 
Back
Top Bottom